Mpango wa Trump Kuhusu Gaza Ni Mpango Mbaya Unaolenga Kuondoa Kabisa Suala la Palestina
(Imetafsiriwa)
Habari:
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kukubali kwa Waziri Mkuu wa Kiyahudi Netanyahu mpango wenye vipengele ishirini wa kukomesha vita katika Ukanda wa Gaza. Trump na Netanyahu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya kukutana Washington. Trump alisisitiza kwamba amani huko Gaza inakaribia kupatikana, na alimshukuru Netanyahu kwa kukubali mpango huo. (DW Kituruki, 2025/09/29)
Maoni:
Vita vya Wayahudi dhidi ya Gaza vikiingia mwaka wake wa tatu, Trump, mfuasi mkuu wa mauaji haya ya kimbari, alitangaza kile kinachoitwa mpango wa amani kuhusu Gaza mnamo Septemba 29. Msomaji yeyote wake ataona kuwa ni mpango mbaya unaolenga kuondoa kabisa suala la Palestina. Kila kifungu chake kinajumuisha kujisalimisha bila masharti kwa wapiganaji na watu wa Palestina.
Kifungu cha kwanza kinatoa wito wa "kusafisha Gaza kutoka kwa itikadi kali na ugaidi," kwa maneno mengine, Waislamu wa Gaza wanaotetea ardhi yao na maeneo yao matakatifu mbele ya uvamizi wanawekwa kama magaidi. Hakuna marejeleo ya uhalifu wa chombo cha Kiyahudi cha kigaidi cha kweli, muuaji wa watoto. Kifungu cha nne kinahitaji kuachiliwa kwa wafungwa wote wanaoshikiliwa na Hamas. Kwa upande mwingine, inasemekana kuwa wafungwa 1,700 wa Kipalestina wataachiliwa. Lakini hakuna hakikisho katika suala hili pia; kwa kuwa chombo cha Kiyahudi kina uwezo wa kuwakamata wafungwa waliokombolewa wakati wowote kitakapopenda.
Vipengele viwili kuu vinavyounda kiini cha mpango huo ni vifungu vya sita na kumi na tatu. Kwa mujibu wao, vikosi vya Al-Qassam vitasalimisha silaha zao kwa adui, na handaki na vituo vya kuzalisha silaha huko Gaza vitaharibiwa. Hivyo, watu wa Gaza wataachwa chini ya uhalifu wa chombo cha Kiyahudi kabisa. Hili likitokea, misaada ya kibinadamu itaingia Gaza, na shughuli za ujenzi na maendeleo zitaanza. Hata hivyo, misaada hii haitatolewa kulingana na mahitaji ya kibinadamu; lakini itatolewa kwa kiasi kidogo kidogo na polepole. Zaidi ya hayo, haitatolewa kwa Gaza nzima, bali kwa maeneo "yasiyo na ugaidi" kama wanavyoyaita. Wakati huo huo, hakuna hakikisho la kuondoka kwa uvamizi. Suala hilo limeachwa kuwa la utata kwa kusema "ikiwa imethibitishwa kuwa ugaidi umekwisha" huko Gaza, ambayo inamaanisha kuwa uvamizi hautaisha kamwe!
Netanyahu alifupisha maana ya mpango huo baada ya kukutana na Trump, akisema: "Kila kitu kinaenda vizuri. Wakati tulikuwa tukitarajia Hamas itutenge na ulimwengu, tumewatenga sisi." Aliongeza: "Viongozi wa Kiarabu na Waislamu wataishinikiza Hamas kukubali masharti yetu." Jeshi la Kiyahudi halitaondoka Gaza; na Hamas italazimika kurejesha mateka wote. Ndiyo, kama Trump na Netanyahu walivyosema mara kwa mara, lengo la mpango huo ni kudhibiti Gaza na kuendeleza uvamizi na ukatili, bila bei ya kulipwa huko Gaza iliyovuliwa silaha na upinzani.
Sehemu ya kusikitisha zaidi ni usaliti wa wale wanaoitwa viongozi wa Waislamu ambao Netanyahu alisema "wataishinikiza Hamas kwa niaba yetu." Viongozi hawa wanawajibika kwa kupuuzwa kwa Gaza na kiburi cha makafiri, hawamwogopi Mungu wala hawaaibiki mbele ya umma. Haijalishi Trump anawatukana kiasi gani, hawamwachi; wanashindana kukutana naye hata kwa dakika tano na kupata uhalali kutoka kwake. Viongozi hawa walionekana kwanza kwenye meza ya Trump huko New York, kisha mara moja walieleza kuridhika kwao wakati Trump alitangaza mpango wake wa usaliti. Na sasa, viongozi hawa wanajiandaa kwa usaliti mkuu ambao utachukuliwa kuwa doa katika historia, kwa kisingizio cha kusimamisha umwagaji damu huko Gaza na kufikia amani ya kikanda.
Uturuki, Qatar, Jordan, Pakistan, Saudi Arabia na Indonesia zinafanya kazi kwa bidii kuwalazimisha wapiganaji kuweka chini silaha zao, kwa sababu waliwasilisha ahadi iliyoandikwa kwa Trump kuhusu suala hili. Na sio hivyo tu; lakini baadhi ya nchi hizi zitatuma majeshi yao Gaza, si kuwalinda wakaazi wa Gaza, bali kuwalinda wanajeshi wa kigaidi wa chombo cha Kiyahudi dhidi ya Wapalestina Waislamu. Zaidi ya hayo, nchi hizo zinataka kujenga upya Gaza ambayo Wayahudi wameigeuza kuwa magofu, na kugharamia gharama, na hatimaye, wanataka kuwasilisha Gaza kama nyara kwa Trump kafiri kwa kuachana na utajiri wa umma. Kwa upande mwingine, hawataweza kupata chochote ila "umejitahidi" kutoka kwa Trump, kisha watahamia haraka kuelekea kurejesha uhusiano wa kawaida na chombo cha Kiyahudi. Kwa kweli, historia ya umma wa Kiislamu haijawahi kushuhudia unyonge mkuu kama huo.
Kwa hivyo, ni wajibu wa kila Muislamu anayeunga mkono suala la Palestina kukataa mpango huu wa hiana na watetezi wake, ambao unamaanisha kujiua kisiasa, ambayo ni dhambi kubwa mbele ya Mungu, na kuwapinga, na kufanya kazi ya kuutenganisha mpango huo.
Kama alivyosema shahidi Yahya Sinwar, Mungu amrehemu: "Mji huu (Jerusalem - Gaza) utawaweka wazi watu wote wanaokubaliana na uvamizi, utawaweka wazi washirika wote, na utaonyesha uso wa kweli wa waliojisalimisha na walioacha."
Mpaka msaada wa Mungu uwafikie wale wanaovumilia na kumtegemea.
Imeandikwa na Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Muhammad Amin Yildirim