Tunawezaje Kuunga Mkono Yule Anayeunga Mkono Vita vya Mauaji ya Kimbari?!
Habari:
Trump: (Hakuna mtu aliyefanya kwa ajili ya Israel zaidi ya nilivyofanya). (Al Jazeera Net، 2 Septemba 2025)
Maoni:
Haiko siri tena kwa mtu yeyote kuhusu msaada kamili wa Amerika kwa shirika la wavamizi, na kuzungumzia hilo imekuwa jambo la kawaida, lakini jambo limefikia hatua kwamba Trump anashughulika na Gaza kama kipande cha jibini au nyama! Baadhi ya habari ziliripoti juu ya Netanyahu katika mkutano wa Baraza la Mawaziri dogo (Baraza la Mawaziri) siku chache zilizopita akisema, akinukuu kutoka kwa Trump "Acheni mikataba ya sehemu. Halafu ikate vipande vipande zaidi, vipande vipande zaidi. Ingieni kwa nguvu zote na mmalize jambo hilo".
Katika kivuli cha uhalifu huu na msaada huu kwa mauaji ya kimbari, kukata, kuua, kubomoa na kufukuzwa, imekuwa lazima kwa Waislamu; wasomi wao na watu wao kwa ujumla, kutoa wito wa wazi, wenye nguvu na ulioimarishwa wa kuvunja muungano wa kiusalama na kijeshi na Amerika, na kutoa wito wa kukomesha aina zote za uwepo wake wa kijeshi katika nchi zote za Waislamu.
Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu anawakataza wale waliokupigeni vita katika dini, na wakakutoeni majumbani mwenu, na wakasaidia katika kukufukuzeni, kuwafanya marafiki. Na watakao wafanya marafiki hao, basi hao ndio madhalimu﴾ Yaani: Anawakataza kuwapenda wale waliokuwa maadui zenu, wakakupigeni na kuwatoa na kusaidia katika kuwatoa, Mwenyezi Mungu anawakatalia kuwapenda na anawaamrisha kuwachukia, kisha akasisitiza ahadi juu ya kuwapenda akisema: ﴿Na watakao wafanya marafiki hao, basi hao ndio madhalimu﴾ Tafsiri ya Ibn Kathir.
Je, mtu mwenye akili leo atasema kwamba Amerika haikuunga mkono shirika la wavamizi kuua watu wa Gaza, kuangamiza na kuwafukuza kutoka majumbani mwao?!
Imeandikwa kwa ajili ya Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Mh. Osama Al-Thuaini