Je, mikutano yako yote na mabalozi wa Marekani haikukufaidi, Ee Sultan?!
Habari:
Tovuti ya habari ya Yemeni Al-Bawaba Al-Ikhbariya iliripoti mnamo Septemba 28 habari yenye kichwa "Marekani Yamuadhibu Sultan Al-Arada" ambayo ilisema: "Marekani ilikataa kumpa mwanachama wa Baraza la Urais visa ya kuingia katika ardhi yake ili kushiriki katika mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York.
Vyanzo vilisema kuwa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilikataa kumpa Sultan Al-Arada visa ya kuingia kama sehemu ya ujumbe wa Baraza la Urais ukiongozwa na Rashad Al-Alimi na mwanachama wa baraza Aidaroos Al-Zubaidi, kwa sababu ya uhusiano wake na watu wenye itikadi kali za kigaidi katika shirika la Al-Qaeda, mashuhuri zaidi kati yao ni kaka yake, kiongozi Khalid Al-Arada.
Maoni:
Ingawa Sultan Al-Arada, ambaye aliteuliwa na Abd Rabbuh Mansur mnamo Aprili 2012 kuwa gavana wa mkoa wa Marib, alikutana huko Marib mara kwa mara na mabalozi wa Marekani waliofuatana huko Yemen, waliokaa Jeddah, kama vile Matthew Tueller, Christopher Henzel, Steven Fagen, na mkuu wa masuala ya ubalozi Jonathan Peccia, lakini mikutano yote hiyo haikumfaidi na Marekani kuingia katika ardhi yake!!
Mikutano hii inakiuka itifaki za sheria ya sasa ya kimataifa, ambayo ilitambua Wizara ya Mambo ya Nje kama njia pekee ya shughuli na mikutano ya mabalozi katika nchi wanazofanyia kazi.
Chini ya sheria ya kimataifa inayotegemea Mkutano wa Westphalia mwaka 1648, kukataa kuingia kwa mtu kutoka kwa ujumbe wa Yemen kwenda Marekani ni tusi na kofi kwa uso wa Baraza la Urais lenye wanachama wanane, na ilistahili kujibu kukataa huku kwa kughairi ziara hiyo, au kusubiri kujibu kwa njia sawa. Lakini Baraza la Urais, lililozaliwa kutokana na tumbo la sheria ya kimataifa likiwa na wanachama wanane huko Riyadh, ni mfano wa mifumo ya utawala kama hiyo iliyokalia vifua vya Waislamu, wakati ilibadilisha hukumu za Uislamu na hukumu za sheria ya kimataifa na wanachama wake wakawa marafiki, na wao ni wapiganaji dhidi ya Uislamu na Waislamu!
Uislamu hauruhusu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia na Marekani, taifa linalopigana na Uislamu na Waislamu kwa vitendo, iliyotangaza vita vya msalaba dhidi yetu tangu mwaka 2001, na mikono yake inatona damu yetu leo huko Gaza.
Je, unalinganisha ukiukwaji mbaya wa haki za binadamu katika magereza ya Marib, na kukamatwa kiholela, na kile ambacho Marekani ilifanya kwa Wahindi Wekundu kwa karne nyingi mfululizo?! Hakika, haifikii 0.01%. Vitabu vitatu vya Munir Al-Akkash kuhusu Marekani na mauaji ya kimbari, ngono na kitamaduni ya Wahindi Wekundu vinakutosha, na vinaifanya Marekani kuwa kimya kwa muda mrefu kuhusu kuimba kuhusu haki za binadamu.
Enzi ya mauaji ya kimbari ya mataifa imekwisha, kama vile Stalin alivyowafukuza mamilioni ya watu kutoka nchi zao, na kuwaua katika jangwa la Siberia katika enzi ya Soviet, na ulimwengu utapokea, kwa idhini ya Mungu, nuru ya ujumbe wa mwisho katika enzi ya dola ya pili ya Khilafa iliyoongoka kwa msingi wa njia ya Utume.
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Mhandisi Shafiq Khamis - Jimbo la Yemen