Kwa Nini Tony Blair?
Habari:
Rais wa Marekani Trump alitoa mpango wake wa kumaliza vita huko Gaza, akizungumzia kuanzisha shirika la usimamizi wa kimataifa linaloitwa "Baraza la Amani" litakalojumuisha watu mashuhuri na viongozi wa kimataifa, akiwemo Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Tony Blair.
Maoni:
Haishangazi kwamba Trump anamchagua mtu yuleyule ambaye nchi yake ilishiriki katika uvamizi wa Iraq miongo miwili iliyopita, ili kuwa mwendelezo wa utawala wa Magharibi juu ya ulimwengu wa Kiislamu chini ya bendera ya "Amani na Ujenzi".
Uteuzi wa Tony Blair sio kwa sababu yeye ni mjumbe wa Kamati ya Nne katika Mashariki ya Kati (Amerika, Urusi, Umoja wa Ulaya na Umoja wa Mataifa) kutatua matatizo ya kisiasa yaliyopo kati ya mamlaka na taasisi ya Kiyahudi, kama maandalizi ya kuanzisha taifa la Palestina, au kwa sababu ana uzoefu na mahusiano katika Mashariki ya Kati, lakini kuna mwelekeo mwingine nyuma ya hili ambao wengi hauwataji, ambalo ni kile Blair anachokikuza mwenyewe kama mmiliki wa mafanikio ya kusimamia mzozo wa Ireland ya Kaskazini, ambao uliendelea kwa miongo mitatu ya vurugu na mgawanyiko, ambapo alikusanya pande za mzozo, wazalendo na wanaharakati, kwenye meza moja katika makubaliano ya Ijumaa Kuu mwaka 1998, na alipendekeza mfumo wa vitendo wa mpito kutoka mapambano ya silaha hadi suluhu ya kisiasa na dhamana za kimataifa, na hii ndiyo Magharibi inajaribu kuiga huko Gaza.
Enyi Waislamu, chaguzi zilizo mbele yetu ni wazi: ama taasisi ya Kiyahudi na wale walio nyuma yake watakamilisha mradi wa utakaso wa kikabila kama ulivyotokea Amerika, Australia, na Afrika Kusini, au wataondoka kama Uingereza ilivyoondoka India na Ufaransa kutoka Algeria. Na siku zimeonyesha kwamba watu wa Gaza peke yao, haijalishi wanavyosimama imara na kuwa thabiti, hawataweza kulazimisha Wayahudi wavamizi kuondoka, na wanawezaje kuondoka bila kusogeza majeshi ya Waislamu ili kuwateketeza kabisa kutoka ardhi iliyobarikiwa, hili ndilo suluhisho la kivitendo, enyi Waislamu!
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Jaber Abu Khater