Damu za wasio na hatia zinammwagika kwa manufaa ya nani na uhalifu unafanyika Sudan?!
Habari:
Waziri wa Nchi wa Ustawi wa Jamii nchini Sudan, Salima Ishaq, amefichua kuwa Vikosi vya Msaada wa Haraka viliwaua takriban wanawake 300 katika siku mbili za kwanza za kuingia kwao mji wa El Fasher, kituo cha jimbo la Darfur Kaskazini, magharibi mwa nchi, akisisitiza kwamba wanawake walifanyiwa unyanyasaji wa kingono na aina mbalimbali za unyanyasaji na mateso. Ishaq alisema kuwa hali katika El Fasher ni mbaya, akionyesha kwamba kila anayeondoka mjini yuko hatarini, kwani barabara inayoenda mji wa Tawila imekuwa njia ya kifo. Aliongeza kuwa familia nyingi bado zimezingirwa katika El Fasher, na zinafanyiwa kuburutwa, kuteswa, kudhalilishwa na unyanyasaji wa kingono, akizingatia kwamba kinachoendelea mjini ni "utakaso wa kikabila uliopangwa na uhalifu mkuu ambao kila mtu anashiriki kwa kunyamaza." (TRT Kiarabu)
Maoni:
Inaumiza mioyo na kuliza macho kuona damu za wasio na hatia zikimwagika Sudan, heshima ya wanawake ikikiukwa, maelfu wakihamishwa kutoka makazi yao na nchi yao, na njaa na magonjwa yakienea ili Amerika ivune matunda ya haya yote baada ya kuchochea vita hivi kati ya vibaraka wake, Burhan na Hemedti, ili kufikia maslahi yake na malengo yake kwa kuwaondoa vibaraka wa Uingereza madarakani, kunyakua utajiri wa Sudan na kuigawanya katika majimbo madogo yaliyochorwa mipaka yake kwa damu kama ilivyotokea wakati Sudan Kusini ilipotenganishwa, na kama inavyotokea sasa ya uhalifu katika eneo la Darfur, haswa huko El Fasher, na mambo yanaelekea kuwa mabaya zaidi katika maeneo mengine ya Sudan, na hakuna uwezo wala nguvu ila kwa Mungu.
Licha ya ukatili na uhalifu wote uliofanywa na unaoendelea kufanywa katika vita hivi, na licha ya mzozo mkubwa wa kibinadamu huko, haujaangaziwa vya kutosha; kwa upande mmoja, hali ya mambo ardhini kutokana na kukatika kwa mtandao na ukosefu wa vifaa na hali zingine za uwanjani ambazo zimewafanya watu kuwa vigumu kusambaza kinachoendelea, na kwa upande mwingine, usiri wa vyombo vya habari uliokusudiwa na kushindwa kuonyesha mateso ya watu na kueleza sababu halisi ya kinachoendelea, kiasi kwamba watu wengi hawajasikia kinachoendelea ila kupitia mitandao ya kijamii, na kupitia kile kilichoenea hivi karibuni cha matukio na picha zilizotangazwa na wale waliofanya mauaji haya wakijigamba kwa uhalifu wao na kuwatisha watu, na kupitia kuangazia vyombo vya habari matukio hivi karibuni, haswa vyombo vinavyohudumia ajenda za Ulaya, ambavyo utangazaji wao unakuja katika muktadha wa mzozo wao na Amerika juu ya ushawishi huko ili kumwaibisha na kuwaaibisha vibaraka wake na kuwashinikiza kujaribu kupata hata makombo.
Jambo muhimu zaidi kwa Waislamu kwa ujumla na kwa watu wa Sudan haswa kulitambua ni uelewa wa asili ya mzozo Sudan, na asili ya mipango inayotekelezwa na Hemedti na Burhan na upande wanaoutumikia, na malengo yanayokusudiwa kufikiwa kutoka kwa vita hivi, ili waweze kuzishindwa na kurejesha udhibiti wa mambo yao, na vijana wa Hizb ut Tahrir wamefanya juhudi kubwa katika muktadha huu, na wamewaonya mara kwa mara juu ya kile kinachopangwa kwa Sudan na watu wake, na wamewaelezea njia ya ukombozi, kwa hivyo hakuna wokovu kwa watu wa Sudan ila kwa kufanya kazi na Hizb ut Tahrir, na kwa kuwashinikiza wazalendo kutoka kwa wana wao katika jeshi kuunga mkono upande wa watu wao na umma wao na kuwafanya hila za wakoloni ziwarudie wenyewe.
Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut Tahrir
Baraa Munasara