Pamoja na Hadithi Tukufu - Thawabu ya Mjitihadi
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali katika kipindi kipya cha programu yenu Pamoja na Hadithi Tukufu, na tunaanza na salamu bora kabisa, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Kutoka kwa Amru bin Al-Aas kwamba yeye alisikia Mtume wa Allah, Swalla Allahu Alayhi wa Sallam, akisema: "Hakimu anapohukumu na akajitahidi kisha akapatia, basi anapata thawabu mara mbili, na anapohukumu na akajitahidi kisha akakosea, basi anapata thawabu moja."
Imekuja katika Sahih Muslim kwa maelezo ya An-Nawawi
Kauli yake, Swalla Allahu Alayhi wa Sallam: (Hakimu anapohukumu na akajitahidi kisha akapatia, basi anapata thawabu mara mbili, na anapohukumu na akajitahidi kisha akakosea, basi anapata thawabu moja)
Wanavyuoni wamesema: Waislamu wamekubaliana kuwa hadithi hii inahusu hakimu mjuzi, mwenye uwezo wa kuhukumu, akipatía anapata thawabu mbili: thawabu kwa jitihada zake, na thawabu kwa kupatia kwake, na akikosea anapata thawabu kwa jitihada zake.
Na katika hadithi kuna sehemu iliyoondolewa, makadirio yake: Anapotaka hakimu, basi ajitahidi, wamesema: Ama yule ambaye hana uwezo wa kuhukumu, basi hairuhusiwi kwake kuhukumu, akihukumu hana thawabu, bali yeye ni mwenye dhambi, na hukumu yake haitekelezeki, sawa na ikipatana na haki au la, kwa sababu kupatia kwake ni bahati tu, hakutokani na msingi wa kisheria, hivyo yeye ni muasi katika hukumu zake zote, sawa na ikipatana na sawa au la, na yote imekataliwa wala hawi na udhuru katika chochote katika hilo, na imekuja katika hadithi katika Sunan "Mahakimu ni watatu: Hakimu mmoja yuko Peponi, na wawili wako Motoni, hakimu aliyefahamu haki na akahukumu nayo huyo yuko Peponi, na hakimu aliyefahamu haki na akahukumu kinyume nayo huyo yuko Motoni, na hakimu aliyekata kwa ujinga huyo yuko Motoni", na wanavyuoni wamekhitalifiana katika kwamba kila mjitahidi amepatia au mpatiji ni mmoja, naye ni yule aliyeafikiana na hukumu iliyo kwa Allah Taala, na mwingine amekosea hana dhambi kwa udhuru wake? Na lililo sahihi zaidi kwa Imam Shafi'i na masahaba zake ni kwamba mpatiji ni mmoja, na kila kundi limetoa hoja kwa hadithi hii, ama wale wa mwanzo wasemao: (Kila mjitahidi amepatia) wamesema: Mjitahidi amefanywa kuwa na thawabu, lau kama haku patia basi asingekuwa na thawabu, ama wale wengine wamesema: Amemwita mkoseaji, lau kama angekuwa amepatia asingemwita mkoseaji, ama thawabu basi yeye amepata kwa sababu ya uchovu wake katika ijtihadi, wamesema wale wa mwanzo: Yeye amemwita mkoseaji kwa sababu yeye amebebwa na yule aliyekosea nas, au amefanya ijtihadi katika yale ambayo haifai kufanya ijtihadi kama vile yaliyokubaliwa na wote na mengineyo, na khilafa hii ni katika ijtihadi katika matawi, ama misingi ya tauhidi mpatiji ndani yake ni mmoja kwa itifaki ya anayeaminika, na hakuna aliyepinga isipokuwa Abdallah bin Al-Hasan Al-Abteri na Daud Al-Dhahiri wao wameona kuwa wajitahidi wamepatia katika hilo pia, wanavyuoni wamesema: Lililo dhahiri ni kwamba wao wamemkusudia mjitahidi katika Waislamu sio makafiri na Allah ndiye mjuzi zaidi.
Na imekuja katika Fath Al-Bari kwa maelezo ya Sahih Al-Bukhari
Kauli yake (Hakimu anapohukumu na akajitahidi kisha akapatia)
Katika riwaya ya Ahmad "akapatia" Al-Qurtubi amesema: Hivi ndivyo imetokea katika hadithi imeanza na hukumu kabla ya ijtihadi, na jambo lenyewe ni kinyume kwa sababu ijtihadi inatangulia hukumu kwa sababu haijuzu kuhukumu kabla ya ijtihadi kwa itifaki, lakini makadirio katika kauli yake "Anapohukumu" ni anapotaka kuhukumu hapo ndipo anafanya ijtihadi, amesema na inaiunga mkono kwamba watu wa misingi wamesema: Inampasa mjitahidi kufanya upya nadhari anapotokea mtafaruku, wala hatagemezeki na yale yaliyomtangulia kwa uwezekano wa kumdhihirikia kinyume na yeye. Imekwisha. Na inawezekana kuwa "fa" ni tafsiri wala sio ya kufuatia na kauli yake "akapatia" yaani amekubaliana na lile lililo katika nafsi ya amri katika hukumu ya Allah Taala.
Wasikilizaji wetu wapenzi:
Ijtihadi katika lugha ni kumaliza uwezo katika kutimiza jambo katika mambo yenye ulazima wa gharama na mashaka. Ama katika istilahi ya wanazuoni wa Usuli imekusudiwa kwa kumaliza uwezo katika kutafuta dhana katika kitu katika hukumu za kisheria kwa namna ambayo mtu anahisi nafsi yake kushindwa katika ziada yake. Na ijtihadi ni fardhi ya kutosheleza kwa Waislamu. Na katika darsa tunazozifaidi kutokana na hadithi hii tukufu na maelezo yake yaliyotangulia:
Kwanza: Inampasa hakimu kuwa mjuzi na mwenye uwezo wa kuhukumu. Na ili awe hivyo inampasa yeye kutimiza masharti mawili nayo ni utimilifu wa maarifa ya lugha na maarifa ya kisheria, la sivyo hakimu anatenda dhambi kwa hukumu yake bila ya elimu.
Pili: Kwamba ijtihadi haikuwa katika yale yaliyokuja na nas ya kisheria yenye kukata dalili kama vile kuharamisha riba, zinaa na kuua, bali inakuwa katika nas za kisheria zilizofupishwa au zenye dhana kama hukumu ya kumgusa mwanamke na hukumu ya uzalishaji (cloning) na mengineyo.
Tatu: Haijuzu kuhukumu kabla ya ijtihadi. Haijuzu kufanya uamuzi katika masuala fulani, kisha kutafuta katika nas za kisheria, na kuzipinda wakati mwingine, kwa kuonyesha kile ambacho kimechukuliwa uamuzi ndani yake asili. Bali inampasa kufahamu uhalisia wa suala na kisha kuangusha nas za kisheria katika uhalisia ili tutoke na hukumu ya Allah katika suala.
Wasikilizaji wetu wapenzi, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya Mtume tunawaacha katika uangalizi wa Allah na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.