Pamoja na Hadithi Tukufu za Kinabii
Mja Muumini Kati ya Hofu na Matumaini!!
Tunakusalimu nyote wapenzi wasikilizaji tukufu kila mahali, tunakutana nanyi katika kipindi kipya cha kipindi chenu "Pamoja na Hadithi Tukufu za Kinabii" na tunaanza na salamu bora na safi zaidi, kwa hivyo Amani iwe juu yenu pamoja na Rehema ya Mungu na Baraka Zake na baada ya hayo:
Imepokewa na Tirmidhiy katika Sunan yake kutoka kwa Anas bin Malik, Mwenyezi Mungu amridhie, kwamba Nabii, swallallahu alayhi wasallam, alimuingia kijana mmoja akiwa katika hali ya kufa, akasema: "Unajisikiaje?", akasema: "Naapa kwa Mungu, Ewe Mjumbe wa Mungu, hakika ninamtarajia Mungu, na ninaziogopa dhambi zangu," Mjumbe wa Mungu, swallallahu alayhi wasallam, akasema: "Haviungani katika moyo wa mja katika mahali kama hapa isipokuwa Mwenyezi Mungu humpa anachokitarajia na humuepusha na anachoogopa." Na Tirmidhiy amepokea katika Sunan yake kutoka kwa Anas bin Malik, Mwenyezi Mungu amridhie, akasema: Nilimsikia Mjumbe wa Mungu, swallallahu alayhi wasallam, akisema: "Mwenyezi Mungu alisema: Ewe mwana wa Adamu, hakika kila unaponiomba na kunitarajia, mimi hukusamehe kwa yale yaliyokuwa ndani yako na wala sijali, Ewe mwana wa Adamu, lau dhambi zako zingefika mawinguni kisha ukaniomba msamaha ningekusamehe na wala sijali, Ewe mwana wa Adamu, hakika lau ungenijia na karibu ya ardhi dhambi kisha ukanikuta hunishirikishi na chochote ningekujia na karibu yake msamaha."
Na imekuja katika dua ya Al-Tabarani katika mlango wa kauli katika kunuti ya witri: "Ewe Mwenyezi Mungu, Wewe pekee tunakuabudu, na kwa ajili Yako tunasali na kusujudu, na kwako tunakimbilia na kufanya bidii, tunatarajia rehema Yako, na tunaogopa adhabu Yako kali, hakika adhabu Yako inawafikia makafiri." Na Mwenyezi Mungu Amesema: (Hakika wale wanaosoma kitabu cha Mwenyezi Mungu, na wakasimamisha swala, na wakatoa katika tulivyowaruzuku kwa siri na dhahiri, wanatarajia biashara isiyoharibika; ili awalipe ujira wao na awazidishe katika fadhila yake. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe, Mwenye shukrani). (Fatir 30) Na Mwenyezi Mungu Amesema: (Je, yule anayesujudu usiku kucha na kusimama, akiihofia Akhera na akitarajia rehema ya Mola wake Mlezi... Sema: Je, wata sawa wale wanaojua na wale wasiojua? Hakika wanao kumbuka ni wenye akili). (Az-Zumar 9) Na Mwenyezi Mungu Amesema: (Hakika wale walio amini na wale walio hama na wakapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, hao ndio wanaotarajia rehema ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu). (Al-Baqara 218)
Hofu na matarajio kwa muumini ni kama mabawa mawili ya ndege! Hawezi kuruka, wala kupanda kwenda angani na moja wapo, isipokuwa yawe yameambatana pamoja, hapo ndipo hawezi kuruka tu, bali na kupaa juu angani! Na hofu inajulikana kwa watu wote. Imesalia tujue maana ya matarajio. Matarajio ki lugha ni chanzo cha msemo wao: "Nilimtarajia fulani", na imechukuliwa kutoka katika mzizi wa "R, J, W" ambao unaashiria matumaini ambayo ni kinyume cha kukata tamaa, kitenzi cha wakati uliopita "Rajaa" kinaishia na alifu iliyonyooshwa. Husemwa: Nilimtarajia fulani rajwa na rajaa na rajawa. Na husemwa: Sijakujia isipokuwa kwa matarajio ya kheri, na nilimtarajia tarjia kwa maana nilimtarajia. Hili, na kwa matarajio kimatamshi kuna maana mbili za kisheria:
Ya kwanza: Matarajio ya msamaha wa Mungu na maghfira yake kwa mwanadamu, basi mwanadamu anapaswa kuwa daima katika hali ya kati ya matarajio kwa Mungu Mtukufu na hofu kutoka kwake Yeye Subhanah: Anatarajia kwamba atamsamehe yale yanayotokea kwake katika madhambi na makosa, na anaogopa kwamba atamuadhibu adhabu kali juu yake. Na kwa uwiano huu kati ya hofu na matarajio anachangamka kwa ajili ya matendo na utiifu, na haimpati kukata tamaa na kukata tamaa ikiwa amekosea au ameingia katika uasi; kwa sababu anajua kwamba Mungu Mtukufu akitubu toba sahihi, na akatoa haki za viumbe juu yake, basi Mungu humsamehe na kumrehemu.
Na ya pili: Kusubiri faraja na kuondolewa kwa balaa, na kuondoka kwa msiba na tatizo ambalo mwanadamu anasumbuliwa nalo, na kutarajia kupatikana kwa bora. Lakini kuna tofauti kati ya matumaini na matarajio, basi matarajio ni mhemko uliolingana, unakusanya kati ya tahadhari na matumaini, na unakusanya kati ya matamanio na matendo. Ama matumaini: Basi ni mhemko ambao hushinda ndani yake matumaini. Na kuna tofauti kati ya matarajio na matamanio nayo ni kwamba matamanio huandamana na uvivu, ama matarajio basi ni pamoja na kujitolea na matendo.
Amesema Ibn Al-Qayyim, Mwenyezi Mungu amrahamu: "Matarajio ni kutazama upana wa rehema ya Mwenyezi Mungu." Na imesemwa: "Ni kufurahia ukarimu na fadhila za Mola Mlezi Mkuu." Na amesema Ibn Al-Qayyim pia: "Matarajio ni ibada, na kujishikiza na Mungu kwa upande wa jina lake: Mwenye ihsani." Na akasema: "Lau si roho ya matarajio viungo visingehamasika kwa utiifu. Na lau si upepo wake mzuri jahazi za matendo zisingetembea katika bahari ya makusudio."
Na amesema Al-Hafidh Ibn Hajar, Mwenyezi Mungu amrahamu: "Makusudio ya matarajio ni kwamba yule ambaye amefanya upungufu basi awe na dhana nzuri kwa Mungu, na atarajie kwamba atamfutia dhambi yake, na hivyo hivyo yule ambaye amefanya utiifu atarajie kukubaliwa kwake, ama yule ambaye amejitumbukiza katika uasi akitarajia kutochukuliwa hatua bila majuto, wala kuacha basi huyu yumo katika ghururi."
Na ni uzuri ulioje wa kauli ya Abu Uthman Al-Jizi: "Miongoni mwa alama za furaha ni kutii, na kuogopa kwamba hautakubaliwa, na miongoni mwa alama za uovu ni kuasi, na kutarajia kwamba utaokoka. Na katika Risala Al-Qushairiyya: Matarajio ni kuambatanisha moyo na kipenzi katika mustakabali. Na amesema Al-Raghib: Matarajio ni dhana ambayo inahitaji kupatikana yale ambayo ndani yake kuna furaha. Na amesema Al-Manawi: Matarajio ni kusubiri kunufaika na yale ambayo yametangulia kwake sababu fulani. Na amesema Al-Shafi'i, Mwenyezi Mungu amrahamu, katika maradhi yake ya kufa:
Moyo wangu ulipokauka na njia zangu zikawa nyembamba Nimefanya matarajio kutoka kwangu kwa msamaha Wako ngazi
Dhambi yangu ilinizidi nilipoilinganisha Kwa msamaha Wako, Mola wangu, msamaha Wako ulikuwa mkuu zaidi
Na amesema Sufyan, Mwenyezi Mungu amrahamu: "Yeyote anayefanya dhambi kisha akajua kwamba Mungu Mtukufu amelikadiria kwake, na akatarajia msamaha wake, Mungu humsamehe dhambi yake." Na amesema Abu Imran Al-Sulami akiimba:
Na mimi huja kwa dhambi nikijua kiwango chake Na najua kwamba Mungu husamehe na hughufiria
Lau watu wangezikweza dhambi basi hakika yazo Na ingawa zimekuwa kubwa katika rehema ya Mungu hudunishwa
Wasikilizaji wetu wapenzi: Tunawashukuru kwa usikilizaji wenu mzuri, miadi yetu pamoja nanyi katika kipindi kijacho Inshaallah, mpaka wakati huo na mpaka tukutane daima, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu na hifadhi yake na amani yake, na Amani iwe juu yenu pamoja na Rehema ya Mungu na Baraka Zake.
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Mwalimu Muhammad Ahmad Al-Nadi - Wilaya ya Jordan - 2014/9/22 BK