Pamoja na Hadithi Tukufu
Kazi Halisi ya Mabadiliko na Siku ya Kiyama
Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Imekuja katika Fath Al-Bari Sharh Sahih Al-Bukhari cha Ibn Hajar Al-Asqalani "kwa ufupi" katika mlango wa kauli ya Mtume ﷺ "Nimetumwa mimi na Saa kama hizi mbili":
Ametuhadithia Saeed bin Abi Maryam, ametuhadithia Abu Ghassan, ametuhadithia Abu Hazim kutoka kwa Sahl, amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ: "Nimetumwa mimi na Saa kama hivi, na akaashiria kwa vidole vyake viwili akavirefusha."
Enyi wasikilizaji wapenzi:
Qur'an Tukufu haikuacha kutuonya kuhusu kukaribia Siku ya Kiyama, Siku ya Hesabu, siku ambayo mwanadamu atavuliwa kila kitu isipokuwa matendo yake, Anasema Subhaanahu wa Ta’ala: {WATU WAMEKARIBIA NA HESABU YAO NA HALI WAO WAMO KATIKA UZEMBE WANA PUUZA} na Anasema Mtukufu: {SAA IMEKARIBIA NA MWEZI UMEPASUKA}, na Anasema Subhaanahu: {NA NINI YAKUJUA LABDA SAA IKO KARIBU}, na katika hadithi hii anatubainishia Mtume wetu Mtukufu ﷺ kiasi kilichobaki cha wakati mpaka Siku ya Kiyama, nacho ni kiasi cha kidole cha kati kinavyozidi kidole cha shahada.
Enyi Waislamu:
Kutokana na maelezo haya, Muislamu anatambua uhakika wa kuwepo kwake katika ulimwengu huu, na kwamba ni lazima atambue uhakika wa maandalizi kabla ya kukutana na Mwenyezi Mungu, iwe mazungumzo yanahusu Saa kubwa "Siku ya Kiyama", au kuhusu Saa ndogo "kifo cha Muislamu mwenyewe", basi mbele ya hali hii ni lazima kuwe na kazi ya kumuokoa mtu na adhabu ya Mwenyezi Mungu, kazi halisi siyo kazi tu, na hakika kazi yenye kuleta matunda na ya bidii -katika siku hizi ngumu- inaelekezwa katika kubadilisha hali mbovu kwa vipengele vyake vyote, siyo sehemu ndogo hapa au sehemu ndogo pale, basi Muislamu kujiteua kuwa mzungumzaji au mwalimu katika msikiti haitoshi, na kundi la watu kujitokeza kuhifadhisha Qur'an halibadilishi chochote katika hali halisi, na baadhi ya watu kujishughulisha na kuandika vitabu tu hakuna faida, na baadhi ya watu kukimbilia dua tu haitoshi, ingawa yote ni matendo mazuri, lakini siyo njia inayoongoza kwenye lengo na madhumuni, kwenye mabadiliko ya jamii, kwenye mabadiliko ya nchi kutoka nchi ya ukafiri kwenda nchi ya Uislamu; kwa njia ya kusimamisha dola ya Kiislamu ambayo inatekeleza hukumu zake, katika muktadha wa maneno haya tunazungumzia kuhusu Siku ya Kiyama, na kuhusu Siku ya Hesabu, basi ni thamani gani kujua Siku ya Hesabu na kuzungumzia kuhusu hiyo bila ya hofu au kazi au kujitolea?!
Ewe Mwenyezi Mungu, tuharakishie ukhalifa ulioongoka juu ya manhaj ya Utume, ambao utakusanya vipande vilivyotawanyika vya Waislamu, uwaondolee yale waliyonayo ya balaa, Ewe Mwenyezi Mungu, uangaze ardhi kwa nuru ya uso wako Mtukufu. Ewe Mwenyezi Mungu, Amin Amin.
Wapenzi wetu, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio: Abu Maryam