Pamoja na Hadithi Tukufu - Haja ya Pesa kwa Ajili ya Maisha
Pamoja na Hadithi Tukufu - Haja ya Pesa kwa Ajili ya Maisha

Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema ya Mungu na baraka zake

0:00 0:00
Speed:
September 19, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - Haja ya Pesa kwa Ajili ya Maisha

Pamoja na Hadithi Tukufu

Haja ya Pesa kwa Ajili ya Maisha

Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema ya Mungu na baraka zake

Amesimulia Ibn Abi Shaybah katika Musannaf yake, akasema:

Ametueleza Yazid bin Harun, akasema ametueleza Al-Asbagh bin Zaid Al-Warraq, akasema ametueleza Abu Al-Zahiriyah kutoka kwa Kathir bin Murrah Al-Hadrami kutoka kwa Ibn Omar kutoka kwa Mtume, rehema na amani ziwe juu yake, alisema: "Yeyote anayeficha chakula kwa siku arobaini, basi amejitenga na Mungu na Mungu amejitenga naye, mkaazi yeyote atakae lala na jirani yake ana njaa basi Mungu amejitenga naye.".

Wasikilizaji wetu wapenzi:

Mungu amemkalifisha mtu binafsi kujilisha mwenyewe na familia yake, na ikiwa hana cha kulisha, ni lazima afanye kazi ili kupata riziki yake na riziki ya familia yake, na ikiwa hapati kazi, ni wajibu wa serikali kumpatia kazi inayofaa. Serikali, inayowakilishwa na Khalifa, ndiye mchungaji na anawajibika kwa raia wake, kwa kauli yake, amani iwe juu yake: "Na Imamu ambaye yuko juu ya watu ni mchungaji na anawajibika kwa kundi lake."

Lakini kuna hali ambazo mtu hawezi kufanya kazi kwa sababu ya ugonjwa au uzee ... au labda anafanya kazi lakini kile anachopata hakitoshi mahitaji yake ya msingi. Mtu kama huyo anastahili kupewa pesa za kutosheleza mahitaji yake ya msingi kikamilifu ..... na hii ni faradhi kwa wale ambao sheria imewalazimu kumtunza kutoka kwa jamaa zake, na ikiwa hawapatikani au wanapatikana lakini hawawezi kumtunza, basi faradhi huhamishiwa kwa Waislamu wote, wa karibu zaidi na wa karibu zaidi, na serikali inachukua nafasi ya Waislamu wote katika kutekeleza haki za hawa masikini, wahitaji, wasafiri na wale walio katika hali kama hiyo, serikali inawatumia kutoka hazina, na haki yao haishii kwa mali ya serikali kutoka kwa ushuru, mateka na mengineyo ..... bali katika zaka na katika mali ya umma.

Ikiwa serikali itashindwa kuwatunza hawa na Waislamu wakashindwa kuwawajibisha na kuwalinda wahitaji (ingawa jambo hili haliwezekani) lakini bado ni uwezekano; wakati huo mhitaji huyu anaweza kuchukua chochote kinachomsaidia kutoka mahali popote anapopata halali na kizuri, iwe ni mali ya watu binafsi au mali ya serikali, na haitaji ruhusa, kwani kuishi ni sababu mojawapo ya kupata pesa, kwani uhai wa mtu hutegemea pesa.

Na inashuhudia hadithi hii, hadithi nyingine: Hajaamini mimi yule anayelala ameshiba na jirani yake ana njaa karibu naye na anajua. Amesimulia Ibn Abi Shaybah, Al-Bazzar na Al-Tabarani, na Al-Albani ameipa daraja ya hasan.

Wasikilizaji wetu wapenzi, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika ulinzi wa Mungu, na Amani iwe juu yenu na rehema ya Mungu na baraka zake.

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh