Pamoja na Hadithi Tukufu
"Pombe ni ufunguo wa kila uovu"
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Imekuja katika maelezo ya Sindi, katika maelezo ya Sunan Ibn Majah "kwa muhtasari" katika sura ya "Pombe ni ufunguo wa kila uovu"
Alitusimulia Al-Hussein bin Al-Hasan Al-Marwazi, alitusimulia Ibn Abi Adi h na alitusimulia Ibrahim bin Saeed Al-Jawhari, alitusimulia Abdul Wahab wote kutoka Rashid Abi Muhammad Al-Himmani kutoka Shahr bin Hawshab kutoka Umm Al-Darda kutoka Abi Al-Darda akisema: Rafiki yangu Sallallahu Alayhi Wasallam aliniusia: "Usinywe pombe kwani ni ufunguo wa kila uovu.
Maneno yake: (kwani ni ufunguo wa kila uovu) kwani inaondoa akili, basi hajali chochote, mlango wa uovu umefunguliwa kwake baada ya kufungwa na kizuizi cha akili.
Enyi wasikilizaji tukufu:
Imesemekana katika kisa hiki, kwamba mtu alipewa hiari ya kuchagua mambo matatu: ama kuzini, ama kuua nafsi, ama kunywa pombe, akaona kwamba zinaa ni miongoni mwa madhambi makubwa hakuthubutu kuifanya, na kwamba kuua nafsi ni kubwa zaidi na kubwa zaidi hakukubali kwa hiari yake, na akaona ni rahisi kunywa pombe, na pombe ilipoanza kumzunguka kichwani, aliua nafsi isiyo na hatia na akazini, kwa sababu alipopoteza akili yake, aliona ni rahisi na halali kufanya madhambi mengine. Kwa hivyo - enyi Waislamu - basi kunywa pombe ni miongoni mwa mambo makubwa, na miongoni mwa madhambi makubwa, pamoja na hayo, na laana ya Mtume - صلى الله عليه وسلم - kwa pombe na muuzaji wake na mnywaji wake, lakini tunaona uwepo wake katika nchi za Waislamu, na tunaona anayekunywa na anayefanya biashara nayo, kana kwamba inatokea katika nchi zisizo za Waislamu, na lililo baya zaidi kuliko hilo, ni kwamba watawala wetu wanaipigia debe, na wanafungua baa zake, mpaka imekuwa kuona maeneo ya kuuza pombe ni miongoni mwa mandhari ya kawaida katika nchi za Waislamu. Na kwa kuwa hili ni miongoni mwa mambo maovu ya dola, na kwa kuwa dola katika nchi za Waislamu hazifanyi kazi ya kuyaondoa, la; bali wanafanya kazi ya kuyaanzisha miongoni mwa Waislamu, basi kuiondoa dola hii na anayetawala ndani yake ni wajibu wa kisheria, na jambo ambalo halitimizwi wajibu isipokuwa nalo, basi ni wajibu, kwa hivyo tunawaomba enyi Waislamu, kufanya kazi na wafanyikazi kurejesha hukumu ya Mungu duniani, kupitia dola ya Kiislamu (Ukhalifa wa pili kwa manhaj ya Utume) ambayo tumeahidiwa na Mtume wetu Mtukufu صلى الله عليه وسلم.
Wasikilizaji wetu tukufu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.