Pamoja na Hadithi Tukufu
Kuharakisha katika Utii
Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake.
Imekuja katika Sahih Muslim, katika maelezo ya Imamu Nawawi "kwa muhtasari" katika mlango wa kuhimiza kuharakisha matendo kabla ya kuonekana fitina:
Amenisimulia Yahya bin Ayoub na Qutaiba na Ibn Hajar wote kutoka kwa Ismail bin Jaafar, Ibn Ayoub alisema: Alitusimulia Ismail akasema: Alinikhbarisha Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Huraira kwamba Mtume wa Mungu, swallallahu alayhi wasallam, alisema: Harakisheni na matendo, fitina kama vipande vya usiku wa giza, mtu huamka akiwa muumini na hufika jioni akiwa kafiri, au hufika jioni akiwa muumini na huamka akiwa kafiri, anauza dini yake kwa faida ndogo ya dunia.
Enyi wasikilizaji tukufu:
Hakika fitina ambazo Waislamu wanaishi nazo siku hizi hazifichiki kwa mtu yeyote, na zimewaathiri watu wa kawaida na watu maalum, wameishi kati ya maneno na uvumi, na kati ya nimesikia kutoka kwa fulani na nimesoma kutoka kwa fulani, na kila mtu anauliza kuhusu usahihi na kuhusu njia ya kutoka na kuhusu njia, na katikati ya vurugu hizi inakuja hadithi ya Mtume wetu Mtukufu, swallallahu alayhi wasallam, harakisheni na matendo, fitina kama vipande vya usiku wa giza.
Enyi Waislamu:
Kuharakisha ni kushindana na kuwania, lakini si katika mambo ya dunia; bali katika mambo ya Akhera. Hii ndiyo njia, hii ndiyo njia ya kutoka, harakisheni na shindanenI na wengine katika kufanya kazi ili kutoka katika fitina hizi, kwa ufahamu wa hali halisi, kwa kujua ukweli na usahihi, kwa kuwalingania watu kwenye kheri na uadilifu, kwa kufanya kazi ya kuheshimu dini hii, kwa kufanya kazi na wafanyakazi ili kurejesha hukumu ya Kitabu cha Mungu na Sunnah za Mtume wake miongoni mwa watu, wale wanaoharakisha na kuharakisha matendo mema wapo katika wakati huu kama vile walivyokuwepo katika zama za Mtume wetu Mtukufu, swallallahu alayhi wasallam, lakini wale ambao wamelala kuhusu kazi na hawakuharakisha na hawakuwania na hawakuelewa ukweli wa hali halisi wanayoishi, watayumba katika fitina hizi, watatoka kutoka giza moja hadi giza lingine, wanaamka wakiharimisha yale ambayo Mungu ameyaharamisha na wanafika jioni wakiya halalisha, na wao hawajui ladha ya haki wala njia.
Ee Mungu, tuharakishie ukhalifa ulioongoka juu ya njia ya Utume ambao unakusanya yaliyotawanyika ya Waislamu, unawaondolea yale waliyo nayo ya balaa, Ee Mungu, nurisha ardhi kwa nuru ya uso wako Mtukufu. Ee Mungu, Amina Amina.
Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake.
Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Abu Mariam