Pamoja na Hadithi Tukufu - Kuharakisha katika Utii
Pamoja na Hadithi Tukufu - Kuharakisha katika Utii

   Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake.

0:00 0:00
Speed:
November 05, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - Kuharakisha katika Utii

Pamoja na Hadithi Tukufu

Kuharakisha katika Utii

   Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake.

   Imekuja katika Sahih Muslim, katika maelezo ya Imamu Nawawi "kwa muhtasari" katika mlango wa kuhimiza kuharakisha matendo kabla ya kuonekana fitina:

   Amenisimulia Yahya bin Ayoub na Qutaiba na Ibn Hajar wote kutoka kwa Ismail bin Jaafar, Ibn Ayoub alisema: Alitusimulia Ismail akasema: Alinikhbarisha Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Huraira kwamba Mtume wa Mungu, swallallahu alayhi wasallam, alisema: Harakisheni na matendo, fitina kama vipande vya usiku wa giza, mtu huamka akiwa muumini na hufika jioni akiwa kafiri, au hufika jioni akiwa muumini na huamka akiwa kafiri, anauza dini yake kwa faida ndogo ya dunia.

Enyi wasikilizaji tukufu:

   Hakika fitina ambazo Waislamu wanaishi nazo siku hizi hazifichiki kwa mtu yeyote, na zimewaathiri watu wa kawaida na watu maalum, wameishi kati ya maneno na uvumi, na kati ya nimesikia kutoka kwa fulani na nimesoma kutoka kwa fulani, na kila mtu anauliza kuhusu usahihi na kuhusu njia ya kutoka na kuhusu njia, na katikati ya vurugu hizi inakuja hadithi ya Mtume wetu Mtukufu, swallallahu alayhi wasallam, harakisheni na matendo, fitina kama vipande vya usiku wa giza.

Enyi Waislamu:

   Kuharakisha ni kushindana na kuwania, lakini si katika mambo ya dunia; bali katika mambo ya Akhera. Hii ndiyo njia, hii ndiyo njia ya kutoka, harakisheni na shindanenI na wengine katika kufanya kazi ili kutoka katika fitina hizi, kwa ufahamu wa hali halisi, kwa kujua ukweli na usahihi, kwa kuwalingania watu kwenye kheri na uadilifu, kwa kufanya kazi ya kuheshimu dini hii, kwa kufanya kazi na wafanyakazi ili kurejesha hukumu ya Kitabu cha Mungu na Sunnah za Mtume wake miongoni mwa watu, wale wanaoharakisha na kuharakisha matendo mema wapo katika wakati huu kama vile walivyokuwepo katika zama za Mtume wetu Mtukufu, swallallahu alayhi wasallam, lakini wale ambao wamelala kuhusu kazi na hawakuharakisha na hawakuwania na hawakuelewa ukweli wa hali halisi wanayoishi, watayumba katika fitina hizi, watatoka kutoka giza moja hadi giza lingine, wanaamka wakiharimisha yale ambayo Mungu ameyaharamisha na wanafika jioni wakiya halalisha, na wao hawajui ladha ya haki wala njia.

   Ee Mungu, tuharakishie ukhalifa ulioongoka juu ya njia ya Utume ambao unakusanya yaliyotawanyika ya Waislamu, unawaondolea yale waliyo nayo ya balaa, Ee Mungu, nurisha ardhi kwa nuru ya uso wako Mtukufu. Ee Mungu, Amina Amina.

   Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Abu Mariam

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh