Pamoja na Hadithi Tukufu
RIKAZI AL-KHUMS
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.
Amehadithia Al-Nisa'i katika Sunan Al-Kubra akasema:
Ametueleza Qutaiba bin Saeed akasema: Abu Awana ametuhadithia kutoka kwa Ubaidullah bin Al-Akhnas kutoka kwa Amru bin Shuaib kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie aliulizwa kuhusu kitu kilicho okotwa akasema: "Kile kilicho katika njia inayopitika au katika kijiji kilichojaa watu, kitangaze kwa mwaka mmoja, akija mwenyewe basi ni chake, la sivyo ni chako, na kile ambacho hakiko katika njia inayopitika wala katika kijiji kilichojaa watu basi humo na katika Rikazi kuna khums"
Maelezo ya Al-Sindi Sharh Sunan Al-Nisa'i, usemi wake: Katika njia inayopitika kama njia iliyo wazi yaani inayopitika
Kitangaze, amri kutoka kwenye utangazaji
Akija mwenyewe: yaani ndiye anayehitajika
La sivyo: yaani asipopatikana basi ni chako yaani ni chako
Al-Suyuti amenukuu kutoka kwa Ibn Malik katika maneno haya, kuondolewa kwa jawabu ya sharti la kwanza, na kuondolewa kwa kitenzi cha sharti baada ya isipokuwa, na kuondolewa kwa mada kutoka katika sentensi ya jawabu ya sharti la pili, na makadirio ni: Akija mwenyewe atachukua, na asipokuja basi ni yako.
Na dhahiri ya hadithi ni kwamba anamiliki anayeokota kwa ujumla, na inaweza kusemwa: Labda muulizaji alikuwa maskini, akamjibu kulingana na hali yake, basi haionyeshi kuwa tajiri anamiliki, na ndani yake kuna kuwa ni wangapi maskini wanakuwa matajiri, basi kutoa jibu kwa ujumla hakifai isipokuwa wakati wa kutoa hukumu kwa ujumla, basi litafakari hilo.
Na ikiwa haiko katika njia inayopitika ... hadi mwisho, Al-Khattabi alisema: Anamaanisha la kawaida ambalo halijulikani mmiliki wake.
Na katika Rikaz kwa kasra ya raa na takhfifu ya kaf na mwisho wake ni zai yenye nukta: kutoka RAKAZA alipoizika, na linalokusudiwa: Hazina ya Kijahili iliyozikwa ardhini, na khums imepatikana ndani yake kwa wingi wa manufaa yake na urahisi wa kuichukua.
Wasikilizaji wetu wapenzi
Hii ni aina nyingine ya matendo ambayo sheria imeyafanya kuwa sababu ya kumiliki, ni kutoa yaliyomo ndani ya ardhi ambayo imeelezewa na hadithi kwa kusema: Na katika Rikazi kuna khums, na Rikaz ni dhahabu iliyozikwa ardhini tangu zamani na tunayoiita leo hazina, basi anayeipata anamiliki aruba khums zake halali na safi kwa mujibu wa sheria, ama khums iliyobaki ni ya dola inaweka katika hazina na inaitumia katika maslahi ya Waislamu kulingana na maoni na juhudi za khalifa, na inahusishwa na Rikaz kutoa madini yaliyomo ndani ya ardhi kwa masharti mawili:
Kwanza: Kiwango chake kiwe kidogo, yaani hakizingatiwi kuwa kiwango kikubwa kwa mtu binafsi, yaani sio katika hesabu isiyoisha.
Pili: Ardhi ambayo Rikaz au madini yametolewa iwe ni mali yake au sio mali ya mtu yeyote kama vile barabara za nje na jangwa na mfano wake, ikiwa ni madini yenye kiwango kidogo na ameyatoa kutoka katika ardhi yake au kutoka katika ardhi isiyo na mmiliki basi itakuwa mali yake.
Ama ikiwa madini yaliyotolewa hayana kiwango kikubwa basi hayamilikiwi na mtu binafsi bali ni mali ya umma kwa ujumla kwa sababu Al-Tirmidhi amehadithia kutoka kwa Abyadh bin Hamal kwamba alifika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie akamkatia chumvi akamkatia, alipoondoka mtu mmoja kutoka katika baraza alisema: Unajua umemkatia nini? Umemkatia mali isiyoisha, akasema akamnyang'anya, na inahusishwa na aina za kutoa yaliyomo ndani ya ardhi kutoa yaliyomo angani kama vile kutoa oksijeni na ozoni na gesi nyingine muhimu kwa tiba au kwa kilimo au kwa viwanda au kutoa chochote ambacho sheria imeruhusu katika yale ambayo Mwenyezi Mungu ameumba na ameruhusu kunufaika nayo kwa ujumla.
Wasikilizaji wetu wapenzi na mpaka tutakapokutana na hadithi nyingine ya Mtume tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu
Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.