Pamoja na Hadithi Tukufu - RIKAZI AL-KHUMS
Pamoja na Hadithi Tukufu - RIKAZI AL-KHUMS

Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.

0:00 0:00
Speed:
June 20, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - RIKAZI AL-KHUMS

Pamoja na Hadithi Tukufu

RIKAZI AL-KHUMS


Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.

Amehadithia Al-Nisa'i katika Sunan Al-Kubra akasema:

Ametueleza Qutaiba bin Saeed akasema: Abu Awana ametuhadithia kutoka kwa Ubaidullah bin Al-Akhnas kutoka kwa Amru bin Shuaib kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake akasema: Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie aliulizwa kuhusu kitu kilicho okotwa akasema: "Kile kilicho katika njia inayopitika au katika kijiji kilichojaa watu, kitangaze kwa mwaka mmoja, akija mwenyewe basi ni chake, la sivyo ni chako, na kile ambacho hakiko katika njia inayopitika wala katika kijiji kilichojaa watu basi humo na katika Rikazi kuna khums"

Maelezo ya Al-Sindi Sharh Sunan Al-Nisa'i, usemi wake: Katika njia inayopitika kama njia iliyo wazi yaani inayopitika

Kitangaze, amri kutoka kwenye utangazaji

Akija mwenyewe: yaani ndiye anayehitajika

La sivyo: yaani asipopatikana basi ni chako yaani ni chako

Al-Suyuti amenukuu kutoka kwa Ibn Malik katika maneno haya, kuondolewa kwa jawabu ya sharti la kwanza, na kuondolewa kwa kitenzi cha sharti baada ya isipokuwa, na kuondolewa kwa mada kutoka katika sentensi ya jawabu ya sharti la pili, na makadirio ni: Akija mwenyewe atachukua, na asipokuja basi ni yako.

Na dhahiri ya hadithi ni kwamba anamiliki anayeokota kwa ujumla, na inaweza kusemwa: Labda muulizaji alikuwa maskini, akamjibu kulingana na hali yake, basi haionyeshi kuwa tajiri anamiliki, na ndani yake kuna kuwa ni wangapi maskini wanakuwa matajiri, basi kutoa jibu kwa ujumla hakifai isipokuwa wakati wa kutoa hukumu kwa ujumla, basi litafakari hilo.

Na ikiwa haiko katika njia inayopitika ... hadi mwisho, Al-Khattabi alisema: Anamaanisha la kawaida ambalo halijulikani mmiliki wake.

Na katika Rikaz kwa kasra ya raa na takhfifu ya kaf na mwisho wake ni zai yenye nukta: kutoka RAKAZA alipoizika, na linalokusudiwa: Hazina ya Kijahili iliyozikwa ardhini, na khums imepatikana ndani yake kwa wingi wa manufaa yake na urahisi wa kuichukua.

Wasikilizaji wetu wapenzi

Hii ni aina nyingine ya matendo ambayo sheria imeyafanya kuwa sababu ya kumiliki, ni kutoa yaliyomo ndani ya ardhi ambayo imeelezewa na hadithi kwa kusema: Na katika Rikazi kuna khums, na Rikaz ni dhahabu iliyozikwa ardhini tangu zamani na tunayoiita leo hazina, basi anayeipata anamiliki aruba khums zake halali na safi kwa mujibu wa sheria, ama khums iliyobaki ni ya dola inaweka katika hazina na inaitumia katika maslahi ya Waislamu kulingana na maoni na juhudi za khalifa, na inahusishwa na Rikaz kutoa madini yaliyomo ndani ya ardhi kwa masharti mawili:

Kwanza: Kiwango chake kiwe kidogo, yaani hakizingatiwi kuwa kiwango kikubwa kwa mtu binafsi, yaani sio katika hesabu isiyoisha.

Pili: Ardhi ambayo Rikaz au madini yametolewa iwe ni mali yake au sio mali ya mtu yeyote kama vile barabara za nje na jangwa na mfano wake, ikiwa ni madini yenye kiwango kidogo na ameyatoa kutoka katika ardhi yake au kutoka katika ardhi isiyo na mmiliki basi itakuwa mali yake.

Ama ikiwa madini yaliyotolewa hayana kiwango kikubwa basi hayamilikiwi na mtu binafsi bali ni mali ya umma kwa ujumla kwa sababu Al-Tirmidhi amehadithia kutoka kwa Abyadh bin Hamal kwamba alifika kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu rehema na amani zimshukie akamkatia chumvi akamkatia, alipoondoka mtu mmoja kutoka katika baraza alisema: Unajua umemkatia nini? Umemkatia mali isiyoisha, akasema akamnyang'anya, na inahusishwa na aina za kutoa yaliyomo ndani ya ardhi kutoa yaliyomo angani kama vile kutoa oksijeni na ozoni na gesi nyingine muhimu kwa tiba au kwa kilimo au kwa viwanda au kutoa chochote ambacho sheria imeruhusu katika yale ambayo Mwenyezi Mungu ameumba na ameruhusu kunufaika nayo kwa ujumla.

Wasikilizaji wetu wapenzi na mpaka tutakapokutana na hadithi nyingine ya Mtume tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu

Na Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh