Pamoja na Hadithi Tukufu
Subira ni ufunguo wa ushindi na uwezeshaji
Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.
Imekuja katika Fath al-Bari Sharh Sahih al-Bukhari ya Ibn Hajar al-Asqalani - kwa muhtasari - katika mlango wa kuzuru makaburi:
Adam alitusimulia, Shuba alitusimulia, Thabit alitusimulia kutoka kwa Anas bin Malik, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, alisema: Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, alipita karibu na mwanamke aliyekuwa akilia karibu na kaburi, akasema: Mche Mungu na uwe na subira. Akasema: Ondoka kwangu, kwani hukupatwa na msiba wangu, na hukumjua. Akaambiwa kwamba yeye ni Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, hivyo akaenda kwenye mlango wa Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, na hakumpata mlinzi yeyote. Akasema: Sikukujua. Akasema: Subira ni pale msiba unapokufika mara ya kwanza.
Enyi wasikilizaji wapenzi:
Subira ambayo mtu hulipwa kwa ajili yake ni ile subira ambayo hutokea mwanzoni mwa mshtuko, ni subira ambayo mtendaji wake anasifiwa, kwa hivyo anasifiwa na anatarajia thawabu kwa sababu anajua kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anayetoa na Mwenyezi Mungu ndiye anayechukua, na kwamba kila kitu kwake kina kipimo. Ndio maana Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, alisema: Mche Mungu na uwe na subira. Miongoni mwa Waislamu, mtu anapofiwa na maiti, hukaa kwenye kaburi lake asubuhi na jioni akilia, akiwa na huzuni na wasiwasi, hivi kwamba maiti haachi akili na mawazo yake, na hasahau msiba, na hili linapingana na kile ambacho Mwenyezi Mungu Mtukufu alitaka.
Enyi Waislamu:
Subira ... Subira ... Kile ambacho umma unapitia siku hizi cha huzuni, majonzi, mauaji na uhamishaji ili kuusukuma kuwa katika nafasi ya mwanamke huyu ambaye alimwambia Mtume, swallallahu alayhi wa sallam: Ondoka kwangu, kwani hukupatwa na msiba wangu. Hapa tunasema kile ambacho Mtume wetu mtukufu alitufundisha: Usihuzunike, Enyi umma mtukufu, wala usikate tamaa, msikate tamaa enyi Waislamu wa Sham na wala msifadhaike, na mjue kwamba yale yaliyokupata ni ujira na kheri kutoka kwa Mungu, na kwamba subira ni pale msiba unapokufika mara ya kwanza. Na kwamba saa ya mwisho ya usiku ndiyo yenye giza na utata zaidi. Na kwamba dola ya kwanza ya Kiislamu ilisimama katika nyakati ngumu zaidi za njama dhidi ya Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, kwa hivyo ulikuwepo uhamaji na ulikuwepo ufalme na ulikuwepo ushindi na uwezeshaji.
Ewe Mola, tuharakishie ukhalifa ulioongoka kwa njia ya unabii, ambao utakusanya misukosuko ya Waislamu, uwaondolee yale waliyomo ya balaa, Ewe Mola, uangaze ardhi kwa nuru ya uso wako mtukufu. Ewe Mola, Amina Amina.
Wapenzi wetu, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, na Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.
Imeandikwa kwa ajili ya redio: Abu Maryam