Pamoja na Hadithi Tukufu - Subira ni ufunguo wa ushindi na uwezeshaji
Pamoja na Hadithi Tukufu - Subira ni ufunguo wa ushindi na uwezeshaji

   Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.

0:00 0:00
Speed:
November 08, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - Subira ni ufunguo wa ushindi na uwezeshaji

Pamoja na Hadithi Tukufu

Subira ni ufunguo wa ushindi na uwezeshaji

   Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.

   Imekuja katika Fath al-Bari Sharh Sahih al-Bukhari ya Ibn Hajar al-Asqalani - kwa muhtasari - katika mlango wa kuzuru makaburi:

   Adam alitusimulia, Shuba alitusimulia, Thabit alitusimulia kutoka kwa Anas bin Malik, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, alisema: Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, alipita karibu na mwanamke aliyekuwa akilia karibu na kaburi, akasema: Mche Mungu na uwe na subira. Akasema: Ondoka kwangu, kwani hukupatwa na msiba wangu, na hukumjua. Akaambiwa kwamba yeye ni Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, hivyo akaenda kwenye mlango wa Nabii, swallallahu alayhi wa sallam, na hakumpata mlinzi yeyote. Akasema: Sikukujua. Akasema: Subira ni pale msiba unapokufika mara ya kwanza.

Enyi wasikilizaji wapenzi:

   Subira ambayo mtu hulipwa kwa ajili yake ni ile subira ambayo hutokea mwanzoni mwa mshtuko, ni subira ambayo mtendaji wake anasifiwa, kwa hivyo anasifiwa na anatarajia thawabu kwa sababu anajua kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anayetoa na Mwenyezi Mungu ndiye anayechukua, na kwamba kila kitu kwake kina kipimo. Ndio maana Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wa sallam, alisema: Mche Mungu na uwe na subira. Miongoni mwa Waislamu, mtu anapofiwa na maiti, hukaa kwenye kaburi lake asubuhi na jioni akilia, akiwa na huzuni na wasiwasi, hivi kwamba maiti haachi akili na mawazo yake, na hasahau msiba, na hili linapingana na kile ambacho Mwenyezi Mungu Mtukufu alitaka.

Enyi Waislamu:

   Subira ... Subira ... Kile ambacho umma unapitia siku hizi cha huzuni, majonzi, mauaji na uhamishaji ili kuusukuma kuwa katika nafasi ya mwanamke huyu ambaye alimwambia Mtume, swallallahu alayhi wa sallam: Ondoka kwangu, kwani hukupatwa na msiba wangu. Hapa tunasema kile ambacho Mtume wetu mtukufu alitufundisha: Usihuzunike, Enyi umma mtukufu, wala usikate tamaa, msikate tamaa enyi Waislamu wa Sham na wala msifadhaike, na mjue kwamba yale yaliyokupata ni ujira na kheri kutoka kwa Mungu, na kwamba subira ni pale msiba unapokufika mara ya kwanza. Na kwamba saa ya mwisho ya usiku ndiyo yenye giza na utata zaidi. Na kwamba dola ya kwanza ya Kiislamu ilisimama katika nyakati ngumu zaidi za njama dhidi ya Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, kwa hivyo ulikuwepo uhamaji na ulikuwepo ufalme na ulikuwepo ushindi na uwezeshaji.

   Ewe Mola, tuharakishie ukhalifa ulioongoka kwa njia ya unabii, ambao utakusanya misukosuko ya Waislamu, uwaondolee yale waliyomo ya balaa, Ewe Mola, uangaze ardhi kwa nuru ya uso wako mtukufu. Ewe Mola, Amina Amina.

   Wapenzi wetu, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, na Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.

Imeandikwa kwa ajili ya redio: Abu Maryam

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh