Pamoja na Hadithi Tukufu
Udhuru wa Mtume صلى الله عليه وسلم
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali katika kipindi kipya cha programu yenu ya Pamoja na Hadithi Tukufu na tunaanza na salamu bora kabisa, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
عَنْ أَنَسٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: "لَقَدْ أُخِفْتُ فِي اللَّهِ وَمَا يُخَافُ أَحَدٌ، وَلَقَدْ أُوذِيتُ فِي اللَّهِ وَمَا يُؤْذَى أَحَدٌ، وَلَقَدْ أَتَتْ عَلَيَّ ثَلَاثُونَ مِنْ بَيْنِ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ وَمَا لِي وَلِبِلَالٍ طَعَامٌ يَأْكُلُهُ ذُو كَبِدٍ إِلَّا شَيْءٌ يُوَارِيهِ إِبْطُ بِلَالٍ". قَالَ أَبُو عِيسَى هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ
Imekuja katika Tuhfatul Ahwadhi kwa ufafanuzi wa Jaami'ut-Tirmidhi "kwa mabadiliko kidogo" Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Hakika nimeogopeshwa) Kutoka kwa kuogofya, yaani nilitishiwa na kuahidiwa mateso na kuuliwa.
Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Na haogopi) Yaani kama nilivyoogopeshwa
Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Na hakika nimeudhiwa) Kutoka kuudhi, yaani kwa kitendo baada ya kutishia kwa kauli
Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Katika Mwenyezi Mungu) Yaani katika kudhihirisha dini yake na kuinua neno lake
Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Yeyote) Yaani miongoni mwa watu katika wakati huo
Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Na hakika zimepita) Yaani zimekwisha
Kauli yake صلى الله عليه وسلم (Thelathini kati ya mchana na usiku) Amesema At-Tibi: Ni uthibitisho wa ukamilifu, yaani siku thelathini na usiku mfululizo ambazo hakuna kitu kinachopungua katika wakati
Na maana ni kwamba Bilal alikuwa rafiki yangu wakati huo na hatukuwa na chakula isipokuwa kidogo tu kwa kiasi ambacho Bilal alikuwa akichukua chini ya kwapa lake. Na mazungumzo yamekwisha tangulia katika kukusanya baina ya riwaya tofauti katika dhiki ya maisha ya Mtume صلى الله عليه وسلم na masahaba zake na upana wake katika mlango wa maisha ya Mtume صلى الله عليه وسلم na watu wake."
Wasikilizaji wetu wapenzi: Alipo muhurumia Mama wa Waumini, Khadija binti Khuwailid Radhi za Allah ziwe juu yake, hali ya Mtume صلى الله عليه وسلم alipomuona anabeba ujumbe mpya kwa watu wake na anachoka na kujitahidi na anapata anayopata katika kuubeba; Alimwambia: Pumzika ewe mwana wa ami. Akamjibu صلى الله عليه وسلم: Hakuna raha baada ya leo ewe Khadija.
Jambo hili katika mtazamo wa Mtume صلى الله عليه وسلم ni kubwa zaidi kuliko kuhesabu hesabu ya raha ndani yake, na uzito wa jukumu la da'wah ni kama uzito wa kuibeba, kinyume na raha, ikiwa mbebaji wa da'wah atatambua majukumu yake katika da'wah, na akahisi ukuu wa kazi ambayo yuko tayari kuifanya.
Umefika wakati kwa Waislamu wanaume na wanawake kuunganisha usiku na mchana ili kufanikisha lengo kuu, kusimamisha Khilafa Rashidah ya Pili iliyoahidiwa iliyo karibu kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, hawa hapa maadui zenu, maadui wa Uislamu, wanawaonjesha umma aina mbalimbali za udhalili na adhabu kutoka kwa wanawake Waislamu waliolawitiwa katika magereza ya Uzbekistan na kwingineko hadi wabebaji wa maiti za watoto wachanga huko Gaza.
Hawa hapa maadui zenu wanaunganisha usiku na mchana ili kuondoa dini yetu; wanapeleleza, wanakamata, wanachinja, wanapotosha, na wanatulazimisha watawala Ruwaibidhat waseme kwa jina letu kwa nguvu, na wanadhibiti mapenzi yetu, wanapotosha madai yetu, wanawafuatia watu wetu waaminifu, na wanafanya kazi ya kuzima sauti ya Khilafa kabla haijazaliwa. Je, sisi hatustahili kujitahidi kuliko wao? Je, sisi hatustahili kukunjua mikono yetu kuliko wao? Je, haujafika wakati wa kujiambia sisi wenyewe na familia zetu kama alivyosema صلى الله عليه وآله وسلم baada ya kushukiwa wahyi moja kwa moja na alikuwa anatambua uzito wa amana: "Hakuna raha baada ya leo ewe Khadija", ndio sisi tunastahili kutoa kuliko wao. Wao wako katika kambi ya batili na sisi tuko katika kambi ya haki. Wao ni watu wa ukafiri, ufasiki na unafiki. Na sisi ni watu wa uchamungu, heshima na utukufu. Wao ni watumwa wa dunia, na sisi ni mashujaa wa Khilafa ijayo kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Wanazungumza kwa dhamiri na roho, wanazungumza kwa damu na heshima, lakini sisi tunafanya biashara ambayo haitaharibika. Tunafanya biashara na yule ambaye mkononi mwake kuna ufalme wa mbingu na ardhi, ili tupate kushinda utukufu wa dunia na akhera kutoka kwa Mola mkarimu.
Wasikilizaji wetu wapenzi na mpaka tutakapokutana na hadithi nyingine ya kinabii tunawaacha katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.