Pamoja na Hadithi Tukufu
"MLANGO WA KUIGA NJIA ZA WAYAHUDI NA WAKRISTO"
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha kipindi chenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, basi Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.
Imekuja katika Sahih ya Imamu Muslim "kwa muhtasari" katika "MLANGO WA KUIGA NJIA ZA WAYAHUDI NA WAKRISTO"
SWAID BIN SAID AMETUHADITHIA, AMESEMA: HAFSU BIN MAISARA AMETUHADITHIA, AMESEMA: ZAID BIN ASLAM AMENIHADITHIA, KUTOKA KWA ATA BIN YASAR, KUTOKA KWA ABI SAID AL-KHUDRIY, AMESEMA: MTUME WA MUNGU, REHEMA NA AMANI ZIWE JUU YAKE, AMESEMA: "LAZIMA MTAFUATA NJIA ZA WALE WALIOKUWA KABLA YENU SHIBRI KWA SHIBRI NA DHIRAA KWA DHIRAA HATA WANGEINGIA KATIKA PANGO LA DUB'U MTAWAANDAMA, TUKASEMA EWE MTUME WA MUNGU WAYAHUDI NA WAKRISTO AKASEMA NANI?"
Kauli yake rehema na amani zimshukie: (Hakika mtafuata njia za waliokuwa kabla yenu shibri kwa shibri na dhiraa kwa dhiraa nk.) Sunan kwa fatha ya sin na nun nazo ni njia,
Na linalokusudiwa na shibri na dhiraa na pango la dhabu ni mfano wa ukali wa kufanana nao; yaani kufanana katika maasi na upinzani, sio katika ukafiri. Na katika hili kuna muujiza dhahiri kwa Mtume wa Mungu, rehema na amani zimshukie, kwani yametokea yale aliyo yasema rehema na amani zimshukie, kutoka kwa kukimbilia kwa Waislamu katika kufuata njia za makafiri, na kujifananisha nao katika itikadi zao na ibada zao na desturi zao na sikukuu zao, bali jambo ni hatari zaidi kuliko hivyo, ambapo baadhi ya Waislamu walikwenda katika kupita kiasi, ambapo walishiriki Wakristo katika kuhudhuria kile kinachojulikana kama misa ya usiku wa manane kwao, basi ikija kile kinachojulikana kwao kama sikukuu ya kuzaliwa, utawaona Waislamu wakishindana kuuhuisha mwaka huu wa Kikristo, katika kile kinachojulikana kama Mwaka Mpya wa Miladia, na inakutosha yale yanayo changanyika nayo ya uzinzi na pombe na ufuska, basi utaona nchi za Waislamu zinaangazwa anga lake katika usiku huu, na hukesha nao hadi asubuhi.
Enyi Waislamu: Ikiwa Mtume -rehema na amani zimshukie- ametutaka tusifunge nao, basi vipi leo tunafuata ufuska wao? Laana ya Mungu iwe juu ya watawala wa Waislamu ambao waliifikisha umma katika anguko hili. Basi tufanye kazi enyi Waislamu ili kuondokana na uchafu huu kutoka kwa watawala, na umma urudi katika nafasi yake ambayo Mungu ameridhia kwake, umma bora uliotolewa kwa watu, wakati huo Wayahudi na Wakristo watafuata sunna za Nabii wetu Muhammad -rehema na amani zimshukie.
Ewe Mungu, fanya jambo hili liwe karibu, Ewe Mungu, amina amina.
Wasikilizaji wetu wapendwa, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, na Amani iwe juu yenu na rehema za Mungu na baraka zake.