Pamoja na Hadithi Tukufu - "Mlango wa Ulazima wa Kuandamana na Jamaa ya Waislamu Wakati wa Fitna Zinapotokea"
Pamoja na Hadithi Tukufu - "Mlango wa Ulazima wa Kuandamana na Jamaa ya Waislamu Wakati wa Fitna Zinapotokea"

Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

0:00 0:00
Speed:
August 30, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - "Mlango wa Ulazima wa Kuandamana na Jamaa ya Waislamu Wakati wa Fitna Zinapotokea"

Pamoja na Hadithi Tukufu

"Mlango wa Ulazima wa Kuandamana na Jamaa ya Waislamu Wakati wa Fitna Zinapotokea"


Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Sahih ya Imam Muslim katika maelezo ya Al-Nawawi "kwa muhtasari" katika "Mlango wa Ulazima wa Kuandamana na Jamaa ya Waislamu Wakati wa Fitna Zinapotokea"                                              

Alitusimulia Ubaidullah bin Muadh Al-Anbari, alitusimulia baba yangu, alitusimulia Asim, naye ni Ibn Muhammad bin Zaid kutoka kwa Zaid bin Muhammad kutoka kwa Nafi' alisema: Abdullah bin Umar alimjia Abdullah bin Muti', wakati kulikuwa na jambo la Harra, wakati wa Yazid bin Muawiya, akasema: Wamsambazie Abu Abd Al-Rahman mto, akasema: Mimi sikukujia ili nikae, nimekujia nikusimulie hadithi, nimesikia Mtume wa Allah, rehema na amani zimshukie, akisema, nimesikia Mtume wa Allah, rehema na amani zimshukie, akisema: "Yeyote atakayeondoa mkono wake kutoka kwa utiifu, atakutana na Allah Siku ya Kiyama bila hoja, na yeyote atakayekufa na hana ahadi ya utiifu shingoni mwake, amekufa kifo cha kijahili."                                 

Kauli yake, rehema na amani zimshukie: Yeyote atakayeondoa mkono wake kutoka kwa utiifu, atakutana na Allah Mtukufu Siku ya Kiyama bila hoja, yaani: Hana hoja katika kitendo chake, wala udhuru kwake haumfaidi.

Enyi wasikilizaji tukufu:

Tahadhari, tahadhari... Katika zama hizi, umma unaishi bila imamu, bila Qur'an inayotekelezwa ndani yake, bila maisha ya Kiislamu, na Mwenyezi Mungu Mtukufu ameutofautisha umma huu na mataifa mengine, kwa kuwalazimisha kuishi kulingana na njia yake na sunna za Mtume wake, na hakuna maana ya kuwepo kwake bila kutekeleza kitabu. Mwenyezi Mungu anasema: "Sikuumba majini na watu ila waniabudu", hivyo hekima ya uumbaji ni ibada. Lakini leo tunaona maisha yaliyo mbali kabisa na yale ambayo Mungu alitaka, bali maisha yanayomkasirisha Mungu Mtukufu, vipi isiwe hivyo na umma hauna ahadi ya utiifu kwa imamu kwa kusikia na kutii, na Mtume wetu mpendwa - rehema na amani zimshukie - ameonya vikali dhidi ya kukosekana kwa imamu na kutokuwepo kwa ahadi ya utiifu.

Hivyo Mtume hapa alimlazimu kila Muislamu kuwa na ahadi ya utiifu shingoni mwake kwa Khalifa, lakini hakulazimisha moja kwa moja ahadi ya utiifu kutoka kwa kila Muislamu kwa Khalifa. Kinacholazimu ni kuwepo ahadi ya utiifu shingoni mwa Muislamu. Kuwepo kwa Khalifa ndiko kunakoleta ahadi ya utiifu shingoni mwa Waislamu, iwe wamefanya ahadi ya utiifu au hawajafanya. Kwa hivyo hadithi ilikuwa ni dalili ya ulazima wa kumsimamisha Khalifa na sio dalili ya ulazima wa kila mtu kutoa ahadi ya utiifu kwa Khalifa. Kwa sababu ambaye Mtume alimlaumu ni kukosekana kwa ahadi ya utiifu shingoni mwa Muislamu mpaka afe, na hakulaumu kutotoa ahadi ya utiifu. Na kukaa bila kumsimamisha Khalifa kwa Waislamu ni maasi miongoni mwa maasi makubwa kwa sababu ni kukaa bila kutekeleza faradhi miongoni mwa faradhi muhimu za Uislamu, ambazo utekelezaji wa hukumu za dini unategemea, bali uwepo wa Uislamu katika uwanja wa maisha unategemea. Waislamu wote wana dhambi kubwa kwa kukaa kwao bila kumsimamisha Khalifa kwa Waislamu. Ikiwa wataafikiana juu ya kukaa huku, dhambi itakuwa juu ya kila mmoja wao katika pande zote za dunia. Na ikiwa baadhi ya Waislamu watafanya kazi ya kumsimamisha Khalifa na baadhi yao hawafanyi hivyo, basi dhambi itaondoka kwa wale ambao wamefanya kazi ya kumsimamisha Khalifa na faradhi inabaki juu yao mpaka Khalifa asimame. Kwa sababu kushughulika na kusimamisha faradhi na kujishughulisha nayo huondoa dhambi ya kuchelewesha kusimamishwa kwake kutoka wakati wake na kutokukamilishwa kwake. Ama wale ambao hawajajishughulisha na kazi ya kusimamisha faradhi, basi dhambi baada ya siku tatu tangu aende Khalifa inabaki inawaendea mpaka wamteue atakayemfuata, kwa sababu Mungu amewalazimisha faradhi wao wamekataa kuifanya na hawajajishughulisha na matendo ambayo yanaweza kuisimamisha, na kwa hivyo wamestahiki dhambi na wamestahiki adhabu ya Mungu na fedheha Yake katika dunia na akhera. Hivyo kustahiki adhabu kwa kuacha faradhi yoyote miongoni mwa faradhi ambazo Mungu amezilazimisha ni dhahiri kabisa, hasa faradhi ambayo kwayo faradhi zinatimizwa, na kwayo hukumu za dini zinasimamishwa, na kwayo amri ya Uislamu inakuwa juu, na neno la Mungu linakuwa ndilo la juu katika nchi za Kiislamu, na katika sehemu zote za ulimwengu.

Wasikilizaji wetu wapenzi, na mpaka tutakapokutana na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh