Pamoja na Hadithi Tukufu - "Mlango wa Wajibu wa Kumtii Viongozi katika Yasiyo Maasi na Uharamu Wake katika Maasi"
Pamoja na Hadithi Tukufu - "Mlango wa Wajibu wa Kumtii Viongozi katika Yasiyo Maasi na Uharamu Wake katika Maasi"

 

0:00 0:00
Speed:
August 29, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - "Mlango wa Wajibu wa Kumtii Viongozi katika Yasiyo Maasi na Uharamu Wake katika Maasi"

Pamoja na Hadithi Tukufu

"Mlango wa Wajibu wa Kumtii Viongozi katika Yasiyo Maasi na Uharamu Wake katika Maasi"


Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Sahih Muslim ya Imam An-Nawawi katika maelezo "kwa muhtasari" katika "Mlango wa Wajibu wa Kumtii Viongozi katika Yasiyo Maasi na Uharamu Wake katika Maasi"

Ametuhadithia Yahya bin Yahya ametuhadithia Al-Mughira bin Abdurrahman Al-Hizami kutoka kwa Abi Zinad kutoka kwa Al-Araj kutoka kwa Abi Huraira kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: "Mwenye kunitii mimi amemtii Mungu, na mwenye kuniasi mimi amemuasi Mungu, na mwenye kumtii Amiri amemtii mimi, na mwenye kumuasi Amiri ameniasi mimi"

Kauli yake: Mwenye kunitii mimi amemtii Mungu na mwenye kumtii Amiri wangu amemtii mimi, na amesema katika maasi mfano wake; kwa sababu Mwenyezi Mungu ameamrisha kumtii Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم, na yeye صلى الله عليه وسلم ameamrisha kumtii Amiri, basi utiifu ukaambatana.

Enyi wasikilizaji wangu waheshimiwa:

Hakika utukufu wa dini hii unatokana na itikadi na hukumu zake, ambazo zikitekelezwa katika uhalisia wa maisha, atafurahi anayezitekeleza na atatulizika, na atakuwa mtu anayehisi ubinadamu wake, na atapanda nao katika ngazi ya maadili, ili kufikia radhi. Na labda historia yetu ya Kiislamu inashuhudia hilo, Waislamu waliishi katika kivuli cha hukumu zake, na wakafurahia vivuli vyake, na wakaokota matunda yake, basi utulivu na raha ya moyo na akili, ndio ulikuwa kichwa cha habari cha uwepo wao katika maisha haya, basi walifanya ubunifu ndani yake kwa ubunifu wowote, na wametuachia hazina za fiqhi, fikra, lugha, sayansi na mengine mengi mengi ...

Enyi Waislamu: Hakika hilo lisingetokea bila kuwepo jambo la muhimu sana, nalo ni utiifu. Naam ni utiifu enyi Waislamu, ndio jambo ambalo Waislamu wanalikosa siku hizi, ndio siri ya ushindi wao, juu ya nafsi zao kwanza na juu ya adui yao pili. Na katika Hadithi Tukufu kuna uhusiano mzuri kati ya kumtii Mungu na kumtii Mtume - صلى الله عليه وسلم - na kati ya kuwatii wenye mamlaka, basi kuwatii wenye mamlaka ni kumtii Mungu na Mtume, na kumuasi mwenye mamlaka ni kumuasi Mungu na Mtume, lakini wako wapi wenye mamlaka leo ambao ni wajibu kuwatii? Bila shaka hawapo, kwa sababu kila anayewatawala Waislamu leo ​​hawezi kuchukuliwa kuwa miongoni mwa wenye mamlaka, kwa sababu wao ni genge au tuseme majambazi waliotawala kwa nguvu na kwa msaada wa mabwana zao makafiri katika uzembe wa umma, na wameitawala bila yale ambayo Mungu ameyateremsha, wameitawala kwa sheria ya Waingereza, Wafaransa na Wamarekani, na hakuna ushahidi zaidi wa tunachosema kuliko yale tuliyo yaona na tunayaona siku hizi za kuuliwa kwa umma wao na watawala hawa katika nchi za mapinduzi. Na hii ina maana kwamba umma leo una wajibu na fardhi kubwa, nayo ni kumsimika mtawala anayetawala kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha. Kwa hivyo Mwenyezi Mungu anawahutubia Waislamu katika kauli yake: "Na mtiini Mungu na mtiini Mtume na wenye mamlaka katika nyinyi" na fardhi hii - fardhi ya utiifu - inabaki kuwa fardhi na haichelewi au kufutwa au kusitishwa kwa kukosekana kwa mtawala. Hii inamaanisha kuwa Waislamu wana wajibu wa kufanya kazi ili kumpata mtawala ambaye kwa uwepo wake fardhi ya utiifu inatimia. Na kile ambacho wajibu hautatimia isipokuwa kwacho, basi ni wajibu. Basi simameni enyi Waislamu .. Enyi ambao bado hamjafanya kazi ili kumpata mtawala huyu, simameni kufanya kazi na wafanyakazi waaminifu wenye ufahamu ili kumpata fardhi huyu mkuu, tunamtii Mungu na Mtume wake - صلى الله عليه وسلم - kwa kumpata na kwa kumtii. Ee Mwenyezi Mungu, tuharakishie hilo na utujaalie miongoni mwa wale wanaosikiliza kauli kisha wanafuata bora yake. Aamiin.

Wasikilizaji wetu wapenzi, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh