Pamoja na Hadithi Tukufu
Watawala wa zama hizi ni mbwa mwitu wenye kichaa
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali katika kipindi kipya cha programu yenu: Pamoja na Hadithi Tukufu, na tunaanza na salamu bora kabisa, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
KUTOKA KWA IBN KABU BIN MALIK AL-ANSARI KUTOKA KWA BABA YAKE AMESEMA: AMESEMA MTUME WA ALLAH SALLA ALLAHU ALAYHI WA SALAM: "MBWA MWITU WAWILI WENYE NJAA WAKIACHILIWA KATIKA KUNDI LA KONDOO HAWATALIFISIDI ZAIDI KULIKO UCHOYO WA MTU JUU YA MALI NA HESHIMA KWA DINI YAKE". Imesimuliwa na Tirmidhi na amesema ni hadithi nzuri sahihi.
Amesema Ibn Taymiyyah Mwenyezi Mungu amrehemu: [Mtume صلى الله عليه وسلم amelaumu uchoyo juu ya mali na heshima nazo ni uongozi na mamlaka na amehabarisha kuwa hilo ni zaidi ya uharibifu wa mbwa mwitu wawili wenye njaa kwa zizi la kondoo na hiyo ni pale wanapompelekea mwenye nazo kuchelewa kumtii Mwenyezi Mungu na kumpenda na kufuata matamanio yake katika aliyompa Mwenyezi Mungu, na kukataa wakati wa vita na mapigano katika njia ya Mwenyezi Mungu basi kwa sifa hizi anapata dharau na lawama katika dunia na akhera, ama ikiwa anatafuta kwa mali na mamlaka radhi za Mwenyezi Mungu na kusimamisha haki na akhera na kusaidiwa nazo katika kumtii Mwenyezi Mungu na kupigania dini yake basi hili ni katika neema kubwa za Mwenyezi Mungu kwa waja wake].
Wasikilizaji wetu waheshimiwa
Hali ya umma leo ni kama hali ya zizi la kondoo ambalo wameingia mbwa mwitu wenye njaa nao ni watawala, wao ni mbwa mwitu wenye kichaa wanaudhi na kuua na kufanya uharibifu katika ardhi, wanaangamiza mazao na vizazi, wameteka mali ya umma na utajiri wake na wamefuta mamlaka yake na wamekataa kufuata njia ya Mwenyezi Mungu na kutawala kwa sheria yake na wamezuia jihadi katika njia yake kwa kufuata amri za mabwana zao wakoloni basi dharau na unyonge vimewazunguka kama bangili inavyozunguka mkono, na ili umma upumzike na uwe salama juu ya dini yake na dunia yake lazima kuwe na ukombozi kutoka kwa mbwa mwitu hao, lazima kung'olewa kundi hilo bovu la watawala kutoka mizizi yao, na hili halitakuwa isipokuwa kwa kufanya kazi kwa bidii kusimamisha dola ya Khilafa Rashida na kwa kusonga mbele vituo vya nguvu katika umma, basi upanga wa khilafa utaanguka juu ya shingo hizo na kuukata basi wanadharauliwa katika dunia na katika akhera wana adhabu kubwa, basi uwanja wa umma utakuwa mtupu kutoka kwa mbwa mwitu na hawabaki isipokuwa simba wanashambulia na kuzunguka kulinda dini ya Mwenyezi Mungu na kuifikisha kwa ulimwengu.
Wasikilizaji wetu waheshimiwa
Na mpaka tutakapokutana na hadithi nyingine ya kinabii tunawaacha katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh