Pamoja na Hadithi Tukufu
Hukumu ya Ukodishaji katika Uislamu
Tunawasalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali katika kipindi kipya cha programu yenu ya "Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora kabisa, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh,
Imepokewa kutoka kwa Abdullah bin Umar ambaye amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehema na amani zimshukie: "Mmpeni mfanyakazi ujira wake kabla jasho lake halijakauka"
Imekuja katika maelezo ya Sunan Ibn Majah ya As-Sindi
Kauli yake: (Mmpeni mfanyakazi) yaani inatakiwa kuharakishwa kumpa haki yake baada ya kumaliza mahitaji
Kauli yake: (kabla jasho lake halijakauka) linalopatikana kwa kushughulika na mahitaji
Wasikilizaji wetu wapenzi:
Ukodishaji ni mkataba juu ya manufaa kwa malipo, na unajumuisha aina tatu:
Aina ya kwanza - ni pale mkataba unahusu manufaa ya vitu, kama vile kukodisha nyumba, wanyama, vyombo vya usafiri na mfano wa hivyo.
Aina ya pili - ni pale mkataba unahusu manufaa ya kazi, kama vile kukodisha mafundi na wataalamu kwa kazi maalum, ambapo kinachokubaliwa ni manufaa yanayopatikana kutokana na kazi, kama vile kukodisha mpaka rangi, mhunzi, seremala na mfano wa hivyo.
Aina ya tatu - ni pale mkataba unahusu manufaa ya mtu, kama vile kukodisha watumishi na wafanyakazi na mfano wa hivyo.
Na ukodishaji kwa aina zake zote ni halali kisheria, Mwenyezi Mungu Amesema: [Na tumewainua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja ili baadhi yao wawatumikishe wengine] na Amesema: [Wakikunyonyesheni basi wapeni ujira wao] na Bukhari amesimulia: «Kwamba Nabii r na Swiddiq walimkodisha mtu kutoka Bani Al-Diil kuwaongoza».
Wasikilizaji wetu wapenzi, hadi tutakapokutana nanyi katika hadithi nyingine ya Mtume tunawaacha katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.