Pamoja na Hadithi Tukufu
Haki ya Muislamu kwa Muislamu Akiwa Hai na Mfu
Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha kipindi chenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Kutoka kwa Abu Hurairah radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم amesema: «Yeyote anayeshuhudia mazishi mpaka iswaliwe, basi anapata qirat, na anayeshuhudia mpaka yazikwe, anapata qirat mbili, Ikaulizwa: na nini hizo qirat mbili? Akasema: Ni sawa na milima miwili mikubwa». Imepokewa na Muslim namba 1633.
Enyi wasikilizaji wema:
Hakika kusindikiza maiti ni haki miongoni mwa haki za Muislamu kwa ndugu yake Muislamu, bali ni jambo la kumkurubisha mtu kwa Mwenyezi Mungu ambalo mtu hulipwa thawabu, na lengo la kujikurubisha huku kwa Mwenyezi Mungu سبحانه وتعالى ni kuchukua mazingatio na kukumbuka Akhera, na pia unyenyekevu na kuhudhurisha moyo na utulivu na kutafakari na kuzingatia, na Masahaba wa Mtume wetu Mtukufu صلى الله عليه وسلم walikuwa wanaishi maana hizi, hivyo walikuwa wanyenyekevu na wanazingatia, kiasi kwamba huwezi kuwasikia sauti isipokuwa ya kulia.
Enyi Waislamu:
Hakika sisi tunapozungumzia kuhusu ukuu wa dini hii ambayo Mwenyezi Mungu ameweka haki ya maiti kwa aliye hai, basi tunajiuliza: Haki hii iko wapi leo katika sheria za dunia? Haki za maiti kwa walio hai ziko wapi katika ulimwengu wa ustaarabu wa Magharibi ambao unajigamba na haki za binadamu? Bali haki za walio hai kwa watawala waliokufa ziko wapi? Uislamu kama ulivyoweka haki za maiti, umeweka haki za walio hai, na aliye hai ana haki zaidi kuliko maiti, kwani kuswalia maiti ni faradhi ya kutosheleza kwa Waislamu, ilhali haki za Waislamu kwa watawala wao ni faradhi na wajibu kwa mtawala, na muhimu zaidi ya haki hizi ni kuwatawala kwa Qur'an na Sunnah kwa kubadilishana na kusikia na kutii, lakini tuseme nini hali watawala vibaraka wamechukua utawala katika ulimwengu wa Waislamu kwa nguvu na wameikana umma? Hawajaenda na haki zao tu; bali wameziingiza katika tanuru ya ujinga na upotevu, ndio; hatusemi isipokuwa wajibu wa kuwaondoa na kumsimamisha Imamu juu ya magofu yao, anayehukumu kwa Kitabu na Sunnah na kusimamisha uadilifu kati ya raia, na anajua haki zao wakiwa maiti na wakiwa hai.
Ewe Mola, tuharakishie ukhalifa ulioongoka juu ya njia ya Utume ambao utakusanya yaliyotawanyika ya Waislamu, Uwaondolee yale waliyomo ya balaa, Ewe Mola, nurisha ardhi kwa nuru ya uso wako Mtukufu. Ewe Mola, amiin amiin.
Wapenzi wetu, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Abu Mariam