Pamoja na Hadithi Tukufu - Haki ya Muislamu kwa Muislamu Akiwa Hai na Mfu
Pamoja na Hadithi Tukufu - Haki ya Muislamu kwa Muislamu Akiwa Hai na Mfu

    Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha kipindi chenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

0:00 0:00
Speed:
June 22, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - Haki ya Muislamu kwa Muislamu Akiwa Hai na Mfu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Haki ya Muislamu kwa Muislamu Akiwa Hai na Mfu

    Tunawasalimu nyote wapenzi wetu kila mahali, katika kipindi kipya cha kipindi chenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh. 

   Kutoka kwa Abu Hurairah radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu صلى الله عليه وسلم amesema: «Yeyote anayeshuhudia mazishi mpaka iswaliwe, basi anapata qirat, na anayeshuhudia mpaka yazikwe, anapata qirat mbili, Ikaulizwa: na nini hizo qirat mbili? Akasema: Ni sawa na milima miwili mikubwa». Imepokewa na Muslim namba 1633.

Enyi wasikilizaji wema:   

   Hakika kusindikiza maiti ni haki miongoni mwa haki za Muislamu kwa ndugu yake Muislamu, bali ni jambo la kumkurubisha mtu kwa Mwenyezi Mungu ambalo mtu hulipwa thawabu, na lengo la kujikurubisha huku kwa Mwenyezi Mungu سبحانه وتعالى ni kuchukua mazingatio na kukumbuka Akhera, na pia unyenyekevu na kuhudhurisha moyo na utulivu na kutafakari na kuzingatia, na Masahaba wa Mtume wetu Mtukufu صلى الله عليه وسلم walikuwa wanaishi maana hizi, hivyo walikuwa wanyenyekevu na wanazingatia, kiasi kwamba huwezi kuwasikia sauti isipokuwa ya kulia.

Enyi Waislamu:

   Hakika sisi tunapozungumzia kuhusu ukuu wa dini hii ambayo Mwenyezi Mungu ameweka haki ya maiti kwa aliye hai, basi tunajiuliza: Haki hii iko wapi leo katika sheria za dunia? Haki za maiti kwa walio hai ziko wapi katika ulimwengu wa ustaarabu wa Magharibi ambao unajigamba na haki za binadamu? Bali haki za walio hai kwa watawala waliokufa ziko wapi? Uislamu kama ulivyoweka haki za maiti, umeweka haki za walio hai, na aliye hai ana haki zaidi kuliko maiti, kwani kuswalia maiti ni faradhi ya kutosheleza kwa Waislamu, ilhali haki za Waislamu kwa watawala wao ni faradhi na wajibu kwa mtawala, na muhimu zaidi ya haki hizi ni kuwatawala kwa Qur'an na Sunnah kwa kubadilishana na kusikia na kutii, lakini tuseme nini hali watawala vibaraka wamechukua utawala katika ulimwengu wa Waislamu kwa nguvu na wameikana umma? Hawajaenda na haki zao tu; bali wameziingiza katika tanuru ya ujinga na upotevu, ndio; hatusemi isipokuwa wajibu wa kuwaondoa na kumsimamisha Imamu juu ya magofu yao, anayehukumu kwa Kitabu na Sunnah na kusimamisha uadilifu kati ya raia, na anajua haki zao wakiwa maiti na wakiwa hai.

    Ewe Mola, tuharakishie ukhalifa ulioongoka juu ya njia ya Utume ambao utakusanya yaliyotawanyika ya Waislamu, Uwaondolee yale waliyomo ya balaa, Ewe Mola, nurisha ardhi kwa nuru ya uso wako Mtukufu. Ewe Mola, amiin amiin.

   Wapenzi wetu, na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.  

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Abu Mariam

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh