Pamoja na Hadithi Tukufu - Hakika mja atasema neno bila kulifikiria
Tunakusalimu nyote wapenzi wasikilizaji kila mahali katika kipindi kipya cha programu yenu pamoja na Hadithi Tukufu na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh,
Kutoka kwa Abu Huraira, kutoka kwa Nabii, rehma na amani zimshukie, alisema: Hakika mja atasema neno la kumridhisha Mwenyezi Mungu, bila kulifikiria, Mwenyezi Mungu atamnyanyua kwa daraja, na hakika mja atasema neno la kumkasirisha Mwenyezi Mungu, bila kulifikiria, ataliangusha katika Jahannam.
Imekuja katika Fath al-Bari kwa maelezo ya Sahih al-Bukhari
Neno lake (bila kulifikiria) yaani halifikirii katika akili yake wala halifikirii mwisho wake wala halidhani kuwa linaathiri chochote, na hilo ni kama neno Lake Taala: ((Na mnahesabu kuwa ni jambo dogo, lakini mbele ya Mwenyezi Mungu ni kubwa)).
Neno lake (anaanguka) Iyadh alisema: Maana yake anaanguka ndani yake akiwa ameanguka.
Wasikilizaji wetu wapenzi:
Miongoni mwa mafunzo yanayopatikana kutokana na hadithi hii tukufu, ni kwamba Muislamu anapaswa kupima maneno yake kabla hayajapimwa, na asiseme ila yaliyo mazuri na mema. Na aya tukufu na hadithi tukufu zimekusanyika katika mlango huu:
Mwenyezi Mungu amesema: ((Na wameongozwa kwenye maneno mazuri))
Na Mwenyezi Mungu Taala amesema: - ((Na semeni na watu kwa wema))
Na Yeye Subhaanahu amesema: - ((Na waambie waja wangu waseme yaliyo mazuri zaidi))
Na Yeye Subhaanahu amesema: - ((Kwake Yeye hupanda neno zuri na amali njema huinyanyua))
Na Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Ogeni moto hata kwa kipande cha tende, na ikiwa hamkupata basi kwa neno zuri))
Na alisema: ((Yeyote anayemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho basi aseme mema au anyamaze))
Na alisema: ((Zuia ulimi wako))
Na alisema: ((Je, ni nini kinachowabwaga watu motoni kwa nyuso zao au alisema kwa pua zao ila ni mavuno ya ndimi zao))
Na kutoka kwa Abdullah bin Amr, Mwenyezi Mungu awaridhie, kutoka kwa Nabii, rehma na amani zimshukie, alisema: ((Katika pepo kuna chumba ambacho nje yake inaonekana kutoka ndani yake, na ndani yake kutoka nje yake)) Abu Malik Al-Ash'ari akasema: Ni cha nani ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu? Alisema: "Kwa yule anayezungumza vizuri, na anayelisha chakula, na analala watu wamelala))
Na kutoka kwa Abdullah bin Masoud, Mwenyezi Mungu amridhie, alisema (Naapa kwa Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu ila Yeye, hakuna kitu kinachohitaji kifungo kirefu kuliko ulimi wangu)
Na alikuwa akisema (Ewe ulimi sema mema upate faida na ukae kimya kutokana na shari kabla hujajuta)
Ajabu kubwa wasikilizaji wetu wapenzi, ni kwa yule anayetamka maneno machafu bila ya kuyafikiria
Na ajabu kubwa ni kwa Muislamu anayemkufurisha ndugu yake Muislamu bila ya kuyafikiria maneno yake
Na ajabu kubwa ni kwa yule anayesema uongo juu ya makundi ya Kiislamu na kuyasemesha yale ambayo hayajasema bila ya kufikiria anachokieneza
Na ajabu kubwa ni kwa yule anayefisidi kati ya watu
Na ajabu kubwa ni kwa kila msengenyaji na mfitini
Tahadhari tahadhari wasikilizaji wetu wapenzi kutokana na ghadhabu ya Mwenye nguvu Mjabar, naye ndiye asemaye Subhaanahu (Hatamki neno ila yuko naye mwangalizi aliye tayari)
Wasikilizaji wetu wapenzi na mpaka tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya Nabii tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh