Pamoja na Hadithi Tukufu
Uuaji wa Yule Anayedhihirisha Kumtukana Mtume ﷺ
Kutoka kwa Ibn Abbas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Kwamba kipofu alikuwa na mama wa mtoto ambaye alikuwa akimtusi Mtume ﷺ na kumdhalilisha, akamkataza lakini hakuacha, akamkemea lakini hakukoma. Akasema: Ilipofika usiku mmoja, alianza kumtukana Mtume ﷺ, akachukua upanga, akauweka tumboni mwake, akajiegemeza juu yake akamuua, mtoto akamwangukia kati ya miguu yake, akachafua sehemu hiyo kwa damu. Alipoamka, hilo lilitajwa kwa Mtume ﷺ, akawakusanya watu, akasema: Namuomba Mwenyezi Mungu mtu aliyefanya alichofanya, nina haki juu yake, ila asimame. Akasimama yule kipofu akiwakanyaga watu huku akitetemeka mpaka akaketi mbele ya Mtume ﷺ, akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi ndiye niliyekuwa naye, alikuwa akikudhihaki na kukudhalilisha, nikamkataza lakini hakuacha, nikamkemea lakini hakukoma, na nina watoto wawili kama lulu kutoka kwake, na alikuwa rafiki yangu. Ilipofika jana usiku, alianza kukutukana na kukudhalilisha, nikachukua upanga, nikauweka tumboni mwake, nikajiegemeza juu yake mpaka nikamuua. Mtume ﷺ akasema: Jueni ya kwamba damu yake ni bure." Imepokewa na Abu Daud na An-Nasa'i na Ahmed alitoa hoja kwayo.
Imam Ash-Shawkani, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema katika An-Nail: Na katika hadithi ya Ibn Abbas kuna dalili kwamba anayemtukana Mtume ﷺ anauawa, na Ibn Al-Mundhir amenukuu makubaliano kwamba yule anayemtukana Mtume ﷺ kwa uwazi lazima auawe. Na Abu Bakr Al-Farisi, mmoja wa maimamu wa madhehebu ya Shafi'i, alinukuu katika kitabu Al-Ijma' kwamba yule anayemtukana Mtume ﷺ kwa kashfa ya waziwazi, amekufuru kwa makubaliano ya wanachuoni. Lau atatubu, adhabu ya kifo haitaondolewa kwake, kwa sababu adhabu ya kashfa yake ni kifo, na adhabu ya kashfa haiondolewi kwa toba. Al-Khattabi alisema: Sijui kuna tofauti yoyote juu ya ulazima wa kumuua ikiwa ni Muislamu.
Ama kuhusu mtu anayemtukana Mtume ﷺ miongoni mwa watu wa ahadi na dhima, Ibn Al-Qasim alisimulia kutoka kwa Malik: Yule anayemtukana Mtume ﷺ miongoni mwao atauawa, isipokuwa akiingia katika Uislamu. Ibn al-Mundhir alinukuu kutoka kwa Al-Layth, Ash-Shafi'i, Ahmad, na Ishaq mfano wake.
Ama kutomuua Mtume ﷺ Wayahudi waliokuwa wakimwambia As-Samu Alaykum, ni kwa sababu hawakuwa na ushahidi wowote juu ya hilo, wala hawakulikiri, kwa hivyo hakuwahukumu kwa ujuzi wake. Na ilisemekana kwamba walipokuwa hawajaidhihirisha na kuipotosha kwa ndimi zao, waliacha kuwaua. Kwa vyovyote vile, ukafiri wa Wayahudi ni mkubwa zaidi, lakini ahadi ilihifadhi damu yao. Na hakuna katika ahadi, na haitakuwepo kamwe kuunga mkono kwamba wanamtukana Mtume ﷺ. Anayemtukana miongoni mwao au kutoka kwa wengine kama vile Wakristo na dini za ukafiri, amevuka ahadi, kwa hivyo inabatilika na anakuwa kafiri bila ahadi, kwa hivyo damu yake inamwagwa na inampasa auawe.
Na kile ambacho makafiri wanafanya leo cha kukiuka utakatifu wa Mtume ﷺ na kumtukana si chochote ila ni utekelezaji wa mpango uliowekwa na nchi za Ulaya na Amerika unaolenga kuchochea roho ya chuki ya msalaba miongoni mwa watu wao dhidi ya Uislamu baada ya kuhakikisha na kugundua kuwa Uislamu unavunja vizuizi vyao na kuingia katika nyumba yao, na kwamba wale wanaoingia katika Uislamu wanakuwa Waislamu kutoka kwa watu wao, na kwamba Uislamu ndio mbadala wa asili na wa kimaumbile kwa itikadi zao potofu, demokrasia yao chafu, na ubepari wao wa kikatili. Na dola ya Kiislamu ijayo, Mwenyezi Mungu akipenda, ndiyo itakayetekeleza kubeba ujumbe wa Uislamu kwa nguvu kwao na kwa ulimwengu mzima kwa njia ya kivitendo, na ndiyo itakayowalipiza kisasi wale waliomtusi Nabii wetu ﷺ. {Na watajua wale waliodhulumu ni marejeo gani watarejea}.