Pamoja na Hadithi Tukufu - Uuaji wa Yule Anayedhihirisha Kumtukana Mtume ﷺ
Pamoja na Hadithi Tukufu - Uuaji wa Yule Anayedhihirisha Kumtukana Mtume ﷺ

 

0:00 0:00
Speed:
July 10, 2025

Pamoja na Hadithi Tukufu - Uuaji wa Yule Anayedhihirisha Kumtukana Mtume ﷺ

Pamoja na Hadithi Tukufu 

Uuaji wa Yule Anayedhihirisha Kumtukana Mtume ﷺ

Kutoka kwa Ibn Abbas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake: Kwamba kipofu alikuwa na mama wa mtoto ambaye alikuwa akimtusi Mtume ﷺ na kumdhalilisha, akamkataza lakini hakuacha, akamkemea lakini hakukoma. Akasema: Ilipofika usiku mmoja, alianza kumtukana Mtume ﷺ, akachukua upanga, akauweka tumboni mwake, akajiegemeza juu yake akamuua, mtoto akamwangukia kati ya miguu yake, akachafua sehemu hiyo kwa damu. Alipoamka, hilo lilitajwa kwa Mtume ﷺ, akawakusanya watu, akasema: Namuomba Mwenyezi Mungu mtu aliyefanya alichofanya, nina haki juu yake, ila asimame. Akasimama yule kipofu akiwakanyaga watu huku akitetemeka mpaka akaketi mbele ya Mtume ﷺ, akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, mimi ndiye niliyekuwa naye, alikuwa akikudhihaki na kukudhalilisha, nikamkataza lakini hakuacha, nikamkemea lakini hakukoma, na nina watoto wawili kama lulu kutoka kwake, na alikuwa rafiki yangu. Ilipofika jana usiku, alianza kukutukana na kukudhalilisha, nikachukua upanga, nikauweka tumboni mwake, nikajiegemeza juu yake mpaka nikamuua. Mtume ﷺ akasema: Jueni ya kwamba damu yake ni bure." Imepokewa na Abu Daud na An-Nasa'i na Ahmed alitoa hoja kwayo.

Imam Ash-Shawkani, Mwenyezi Mungu amrehemu, alisema katika An-Nail: Na katika hadithi ya Ibn Abbas kuna dalili kwamba anayemtukana Mtume ﷺ anauawa, na Ibn Al-Mundhir amenukuu makubaliano kwamba yule anayemtukana Mtume ﷺ kwa uwazi lazima auawe. Na Abu Bakr Al-Farisi, mmoja wa maimamu wa madhehebu ya Shafi'i, alinukuu katika kitabu Al-Ijma' kwamba yule anayemtukana Mtume ﷺ kwa kashfa ya waziwazi, amekufuru kwa makubaliano ya wanachuoni. Lau atatubu, adhabu ya kifo haitaondolewa kwake, kwa sababu adhabu ya kashfa yake ni kifo, na adhabu ya kashfa haiondolewi kwa toba. Al-Khattabi alisema: Sijui kuna tofauti yoyote juu ya ulazima wa kumuua ikiwa ni Muislamu.

Ama kuhusu mtu anayemtukana Mtume ﷺ miongoni mwa watu wa ahadi na dhima, Ibn Al-Qasim alisimulia kutoka kwa Malik: Yule anayemtukana Mtume ﷺ miongoni mwao atauawa, isipokuwa akiingia katika Uislamu. Ibn al-Mundhir alinukuu kutoka kwa Al-Layth, Ash-Shafi'i, Ahmad, na Ishaq mfano wake.

Ama kutomuua Mtume ﷺ Wayahudi waliokuwa wakimwambia As-Samu Alaykum, ni kwa sababu hawakuwa na ushahidi wowote juu ya hilo, wala hawakulikiri, kwa hivyo hakuwahukumu kwa ujuzi wake. Na ilisemekana kwamba walipokuwa hawajaidhihirisha na kuipotosha kwa ndimi zao, waliacha kuwaua. Kwa vyovyote vile, ukafiri wa Wayahudi ni mkubwa zaidi, lakini ahadi ilihifadhi damu yao. Na hakuna katika ahadi, na haitakuwepo kamwe kuunga mkono kwamba wanamtukana Mtume ﷺ. Anayemtukana miongoni mwao au kutoka kwa wengine kama vile Wakristo na dini za ukafiri, amevuka ahadi, kwa hivyo inabatilika na anakuwa kafiri bila ahadi, kwa hivyo damu yake inamwagwa na inampasa auawe.

Na kile ambacho makafiri wanafanya leo cha kukiuka utakatifu wa Mtume ﷺ na kumtukana si chochote ila ni utekelezaji wa mpango uliowekwa na nchi za Ulaya na Amerika unaolenga kuchochea roho ya chuki ya msalaba miongoni mwa watu wao dhidi ya Uislamu baada ya kuhakikisha na kugundua kuwa Uislamu unavunja vizuizi vyao na kuingia katika nyumba yao, na kwamba wale wanaoingia katika Uislamu wanakuwa Waislamu kutoka kwa watu wao, na kwamba Uislamu ndio mbadala wa asili na wa kimaumbile kwa itikadi zao potofu, demokrasia yao chafu, na ubepari wao wa kikatili. Na dola ya Kiislamu ijayo, Mwenyezi Mungu akipenda, ndiyo itakayetekeleza kubeba ujumbe wa Uislamu kwa nguvu kwao na kwa ulimwengu mzima kwa njia ya kivitendo, na ndiyo itakayowalipiza kisasi wale waliomtusi Nabii wetu ﷺ. {Na watajua wale waliodhulumu ni marejeo gani watarejea}.  

More from Sheria

Pamoja na Hadithi Tukufu - Je, mnajua ni nani mfilisi?

Pamoja na Hadithi Tukufu

Je, mnajua ni nani mfilisi?

Karibuni wasikilizaji wetu wapendwa, wasikilizaji wa redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir. Tunakutana nanyi tena na kipindi chetu pamoja na Hadithi Tukufu, na bora tuanzie nayo kipindi chetu ni salamu ya Kiislamu, basi Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imekuja katika Musnad Ahmad - sehemu iliyobaki ya Musnad ya Al-Mukthirin - Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga na swala na zaka, na anakuja hali amemtukana huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu 

  Ametuhadithia Abdurrahman kutoka Zuhair kutoka Al-Alaa kutoka kwa baba yake kutoka kwa Abu Hurairah kutoka kwa Mtume, swallallahu alayhi wasallam, amesema: "Je, mnajua ni nani mfilisi?" Wakasema: Mfilisi kwetu, ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa. Akasema: "Hakika mfilisi katika umma wangu ni yule anayekuja Siku ya Kiyama na funga, swala na zaka, na anakuja hali amemtukana heshima ya huyu, amemsingizia huyu, na amekula mali ya huyu, basi anakaa, na huyu analipwa kutokana na mema yake, na huyu kutokana na mema yake, na yakimalizika mema yake kabla ya kulipa madeni yake ya makosa, huchukuliwa kutoka katika makosa yao na kuwekwa juu yake, kisha anatupwa motoni."

Hakika hadithi hii, kama zilivyo hadithi zingine muhimu, ni lazima ieleweke maana yake na itambulike. Kwa sababu kuna watu ambao ni mafilisi licha ya swala zao, funga zao na zaka zao, kwani huyu alimtukana huyu, akamsingizia huyu, akala mali ya huyu, akamwaga damu ya huyu, na akampiga huyu  

Na ufilisi wake ni kwamba huchukuliwa kutoka kwa mema yake ambayo ni mtaji wake na hupewa huyu na hulipa kwa huyu thamani ya kumsingizia, kumtukana na kumpiga, na baada ya mema yake kwisha kabla ya kulipa madeni yake, huchukuliwa kutoka kwa makosa yao na kuwekwa juu yake kisha anatupwa motoni. 

Na alipowauliza Mtume, rehema na amani zimshukie, masahaba zake, je, mnajua ni nani mfilisi? Maana ya je, mnajua ni kutoka katika kujua na kujua ni elimu ya mambo ya ndani, je, mnajua, yaani mnajua nani hasa mfilisi? Hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Ali, Mwenyezi Mungu aukurimishe uso wake: "Utajiri na umaskini ni baada ya kuonyeshwa kwa Mwenyezi Mungu." Walipoulizwa swali hili, walijibu jibu kutokana na uzoefu wao, mfilisi kwetu ni yule ambaye hana dirham wala bidhaa, huyu ndiye mfilisi kwa mtazamo wa masahaba wa Mtume wa Mwenyezi Mungu, basi akasema, rehema na amani zimshukie: Hapana,... AKASEMA: HAKIKA MFILISI KATIKA UMMATI WANGU NI YULE ANAYEKUJA SIKU YA KIYAMA NA FUNGA, SWALA NA ZAKA... 

Na hili linathibitisha kauli ya Sayyidina Umar: Anayetaka afunge na anayetaka aswali lakini ni uadilifu, kwa sababu swala, funga, hijja na zaka hizi ni ibada ambazo mtu anaweza kuzifanya na katika nafsi yake kuna ikhlasi kwa ajili yake, na anaweza kuzifanya kwa unafiki, lakini kitovu cha uzito ni kujidhibiti kwa amri ya Mwenyezi Mungu 

Tunamuomba Mwenyezi Mungu atuthibitishe juu ya haki, na atufanye miongoni mwa waja wake wachaMungu, na atubadilishie maovu yetu kuwa mema, na asituhuzunishe siku ya kuonyeshwa Kwake, Ee Mwenyezi Mungu, Amina 

Wasikilizaji wetu wapendwa, na mpaka tukutane nanyi na hadithi nyingine ya Mtume, tunawaachia amana kwa Mwenyezi Mungu ambaye haipotezi amana zake, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh 

Nimeiandika kwa ajili ya redio 

Afraa Turab

Pamoja na Hadithi Tukufu - Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Pamoja na Hadithi Tukufu

Wanafiki na Matendo Yao Maovu

Tunawasalimu nyote wapenzi mahali popote mlipo, katika kipindi kipya cha programu yenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imepokewa kutoka kwa Buraida Radhi za Allah ziwe juu yake kwamba Mtume ﷺ amesema: “Usimwite mnafiki bwana, kwa sababu ikiwa yeye ni bwana, basi mmemkasirisha Mola wenu Mlezi.” Imepokewa na Abu Daud kwa isnadi sahihi.

Enyi wasikilizaji wapenzi

Hakika maneno bora ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na uongofu bora ni uongofu wa Nabii wake Muhammad bin Abdullah, rehma na amani zimshukie, Ama baada ya hayo, 

Hakika hadithi hii tukufu inatuongoza jinsi ya kushughulika na wanafiki tunaowajua, kwani Mtume ﷺ alikuwa ndiye pekee anayewajua wanafiki wote kwa majina yao, lakini tunaweza kuwajua baadhi yao kutokana na sifa zao, kama wale ambao Qur'ani imewaelekeza kuwa wanafanya faradhi kwa uvivu na kwa kulazimishwa, na kama wale wanaowafanyia vitimbi Uislamu na Waislamu, wanahamasisha fitina, wanafanya uharibifu katika ardhi, wanapenda uovu uenee kwa kuualika, kuutetea na kuuchunga, na kama wale wanaosema uongo juu ya Uislamu na Waislamu ... na wengineo walio na sifa za unafiki. 

Kwa hivyo, lazima tutambue kile ambacho sheria imeona ni kizuri na kile ilichoona ni kibaya, ili tumjue mnafiki kutoka kwa mkweli, na tuchukue hatua inayofaa dhidi yake. Hatupaswi kuamini upande wa mtu ambaye anafanya kinyume na sheria na anaonekana kuwa anafanya anachokifanya kwa sababu ya bidii yake kwa Uislamu na Waislamu, na hatupaswi kumfuata au kumunga mkono, au hata chini ya hapo kwa kumuelezea kama bwana, vinginevyo Mwenyezi Mungu atatukasirikia.

Sisi Waislamu lazima tuwe watu wenye bidii zaidi kwa Uislamu na Waislamu, na tusimruhusu mnafiki yeyote kuingilia dini yetu na familia zetu, kwani wao ndio hatari zaidi tunayoweza kukumbana nayo siku hizi kwa sababu ya wingi wao na nyuso zao nyingi. Lazima tukumbuke mizani ya kisheria ya kupima matendo ya anayedai Uislamu, kwani Uislamu kwetu ni kinga dhidi ya watu hawa waovu. 

Tunamuomba Mungu aulinde umma wetu kutokana na wahalifu kama hao, na atuongoze kwenye njia iliyonyooka na mizani sahihi ambayo tunapima tabia za watu nayo, ili tujiepushe na wale ambao hawapendwi na Mungu, Aamin. 

Wapenzi wetu, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mungu, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.

Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dkt. Maher Saleh