Mohammed bin Salman kwa Bezeshkian: Tunakataa Matumizi ya Nguvu Kutatua Mizozo
Habari:
Mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman alimpigia simu Rais wa Iran Masoud Bezeshkian siku ya Jumamosi, 14/6/2025, na Mwanamfalme wa Saudi Arabia alieleza rambirambi zake na pole zake kwa Mheshimiwa Rais, watu wa Iran ndugu, na familia za marehemu walioanguka kutokana na mashambulizi ya (Israel) dhidi ya Iran. Vile vile, Mwanamfalme Mohammed bin Salman alisisitiza kulaani na kukataa kwa Ufalme mashambulizi haya ambayo yanaathiri uhuru na usalama wa Iran na pia yanakiuka sheria za kimataifa.
Vile vile, Mwanamfalme alisisitiza kuwa mashambulizi haya yamesababisha usumbufu wa mazungumzo yanayoendelea ya kutatua mzozo na kuzuia juhudi za kupunguza mivutano na kufikia suluhisho la kidiplomasia.
Kwa upande wake, Rais wa Iran alimshukuru Mwanamfalme wa Saudi Arabia kwa hisia zake nzuri kwa Iran na watu wa Iran, akithamini msimamo wa Ufalme katika kukataa na kulaani uvamizi huu. (Sky News Arabia)
Maoni:
Hawa watawala wa Ruwaibidha walio tawala shingo za Umma wa Kiislamu, kazi yao imekuwa kama mtu anayetazama mechi ya mpira wa miguu kati ya timu mbili na anasubiri matokeo ya mechi, na mwishoni mwa mechi anamshangilia mshindi, wanaona nyadhifa zao kama nyara na njia ya kupora utajiri wa watu, kumwaga damu, kupigana na Uislamu na wabebaji wa Da'wah, na kuzuia kufika kwake kwenye mamlaka! Hawa Ibn Salman, Ibn Zayed, na mjinga wa Qatar wanatoa mabilioni ya dola kwa adui wa Mungu, Mtume wake, na waumini Trump, wakati watu wa Gaza wanakufa kwa njaa na kushambuliwa na hawachukui hatua yoyote! Lakini ikiwa kuna harakati kutoka kwa watu wao kuwawajibisha na kujaribu kuleta mabadiliko kwao, hata kwa maneno, wako macho kwao, kama ilivyotokea kwa wasomi wengi ambao wengi wao bado wako katika magereza ya dhuluma katika nchi za Hijaz, wao ni wakali kwa waumini, wenye huruma kwa makafiri, kwa sababu si wa jinsi ya Umma na hawakufika kwenye mamlaka kwa bay'ah na mapenzi ya Umma wa Kiislamu, lakini kwa kukabidhiwa na kafiri mkoloni na kulazimishwa kwa nguvu juu ya shingo zao.
Na sasa, kuhusiana na kile kinachoendelea Iran kutoka kwa shambulio la chombo cha Kiyahudi dhidi ya uwezo wa Umma wa Kiislamu wa nguvu za kijeshi na wanasayansi wa nyuklia, Ibn Salman anatosheka tu kuelezea kulaani na kukataa kwake mashambulizi haya, na hahamishi jeshi lake kusimamisha uvamizi huu dhidi ya nchi ya Kiislamu bila kujali mfumo wa utawala ndani yake, kwa sababu Waislamu wanapaswa kuwa kitu kimoja dhidi ya wengine, kama ilivyokuja katika Hadith tukufu, na wao ni umma tofauti na watu wengine, na pia Muislamu ni ndugu wa Muislamu, hamdhulumu, wala hamsalimishi, wala hamtelekezi.
Kwa hivyo, ni lazima kwa wana wa Umma wa Kiislamu, watu binafsi na vikundi, kufanya kazi ya kupata mawazo haya katika ardhi ya uhalisia kwa kuanzisha tena maisha ya Kiislamu kwa kupata dola ya Khilafah Rashidah juu ya manhaj ya Utume ambayo inaandaa nguvu iwezavyo ya kuwatisha adui, na kuondoa mipaka bandia kati ya nchi za Kiislamu na kutumia Uislamu kikamilifu katika masuala yote ya maisha ndani na kuubeba kama ujumbe wa uongofu na nuru kwa ubinadamu wote, na vile vile kwa watu wa nguvu na kinga katika majeshi ya Waislamu kuunga mkono Hizb ut-Tahrir, painia ambaye watu wake hawadanganyi, ambaye anaunganisha usiku wake na mchana wake ili kufikisha Uislamu kwenye mamlaka, na wajiondoe mbele ya Mwenyezi Mungu siku ambayo mali wala wana hawatafaidika isipokuwa yule atakayemjia Mungu na moyo safi, na ili wasiwe miongoni mwa wale ambao Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema kuwahusu: ﴿Hakika Firauni na Haman na majeshi yao walikuwa wakosefu.﴾
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Abdullah Abdul Hamid - Wilaya ya Iraq