Tamasha la Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu lakamilika kwa kusema Qatar na nchi za Kiarabu bado ni waaminifu kwa kuwa
viatu chakavu vya Marekani huku zikibweka kwa ukali juu ya mawingu!
(Imetafsiriwa)
Habari:
Kufuatia shambulio la kombora lililofanywa na taasisi ya Kiyahudi dhidi ya wanachama wa Hamas nchini Qatar, taarifa ya mwisho ya mkutano wa dharura wa Kiarabu na Kiislamu (Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu) uliofanyika Doha tarehe 15 Septemba 2025, ililaani vikali uchokozi wa Wayahudi dhidi ya Qatar, na kuuelezea kama pigo kubwa kwa matarajio yoyote ya amani katika eneo hilo. Taarifa hiyo ilizitaka nchi wanachama kufikiria upya uhusiano wao wa kidiplomasia na kiuchumi na taasisi ya Kiyahudi, na kuchukua hatua za kisheria dhidi yake.
Maoni:
Rasimu ya taarifa ya awali ilionya kuwa hatua hizi zinaweka "hatarini kila kitu kilichokamilishwa katika njia ya kurejesha uhusiano wa kawaida na taasisi ya Kiyahudi, ikiwa ni pamoja na makubaliano ya sasa na yajayo." Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zinaendelea na kulaani na kutoa maonyo kama walivyokuwa wakifanya kwa miaka na miongo kadhaa, hata hivyo, hali bado ni ya kawaida kwa wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.
Kulingana na shirika rasmi la habari la UAE, Waziri wa Mambo ya Nje wa UAE Abdullah bin Zayed alikutana na Waziri Mkuu wa Wayahudi Netanyahu pembezoni mwa mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huko New York, ambapo alisisitiza ulazima wa kukomesha vita dhidi ya Gaza, akisisitiza tena "dhamira ya kudumu ya UAE ya kuunga mkono mipango yote inayolenga kufikia amani ya kina inayotegemea suluhisho la mataifa mawili, ili kukidhi matarajio ya watu wa Palestina na Israeli." Unapofanya kulinganisha kati ya matamshi ya viongozi wa Kiarabu na utawala wa Marekani, hakuna tofauti yoyote inayozingatiwa isipokuwa katika hotuba. Utawala wa Marekani unajivunia upendo wake kwa Wayahudi na uungaji mkono wao wa milele kwa taasisi yao, huku viongozi wa Kiarabu wakilaani uhalifu wa taasisi ya Kiyahudi. Hata hivyo, bwana na vibaraka wake wanakubaliana juu ya ujumuishaji kamili wa taasisi ya Kiyahudi katika eneo hilo, na wanaona mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina kama kikwazo kwa lengo lao la pamoja.
Hata kuhusiana na suluhisho la mataifa mawili, hakuna tofauti. Hata Trump alipunguza baadhi ya shinikizo la ndani kwa Netanyahu kutoka ndani ya serikali yake kwa tangazo lake la umma kwamba kuunganishwa kwa Ukingo wa Magharibi "hakutatokea". Pamoja na au bila taifa la Palestina, Jumuiya ya Nchi za Kiarabu itabaki kuwa puto tupu iliyojaa hewa moto ambayo inadumisha utawala wa Marekani juu ya mamia ya mamilioni ya watu wa Mashariki ya Kati ili wale wanaoitwa viongozi wa nchi wanachama waweze kudumisha viti vyao vya enzi, ambavyo wanakalia kama vibaraka.
Imeandikwa kwa ajili ya idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Dkt. Abdullah Rubin