Mauaji Mapya Gaza, Je, Ujasiri wa Umma Utahamka Lini?!
Licha ya kupanda kwa sauti zinazotoa wito wa kusitishwa kwa vita vya Mayahudi dhidi ya Gaza, jeshi la Mayahudi bado linamwaga damu ya wasio na hatia katika kambi za wakimbizi huko Khan Yunis kusini mwa Ukanda wa Gaza, ambapo limetenda mauaji mapya ambayo yanaongezwa kwenye rekodi yake nyeusi.
Shambulio hili la kikatili lililotokea tarehe 4 Julai 2025, si la kwanza, wala halitakuwa la mwisho. Mfumo wa kimataifa na hasa Amerika, wanajua vizuri kwamba chombo cha Mayahudi hakifuati makubaliano, wala hakizingatii uzito wowote. Hata hivyo, Amerika - mfuasi mkuu wa chombo hicho cha wavamizi - inaendelea kuigiza kama mpatanishi wa uwongo, na mlaghai wa kisiasa, ambaye anamwaga machozi ya mamba, na anaiuzia uvamizi silaha na habari ili iendelee na mauaji yake.
Enyi Waislamu, enyi ambao Mwenyezi Mungu amewaunganisha katika Kitabu chake na Sunnah za Nabii wake, rehema na amani zimshukie yeye na Aali zake, je, mnaamini kwamba kunyamaza kwenu juu ya mauaji haya kutawaweka salama kutokana na hesabu? Je, mnadhani kwamba damu ya watoto, mayowe ya wafiwa, na machozi ya mama hupita bila kurekodiwa katika kurasa za matendo yenu? Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Na mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge...﴾, na anasema Subhanahu: ﴿Hakika Waumini ni ndugu﴾.
Ziko wapi majeshi makubwa? Ziko wapi ndege na makombora ambayo serikali za Kiarabu zinajivunia? Wako wapi wanazuoni ambao walituumiza vichwa vyetu kwa kuzungumzia hekima na mawaidha, lakini hatukuona misimamo yao isipokuwa katika kuwaunga mkono watawala wasaliti?! Wako wapi wafanyabiashara na matajiri? Je, wametoa chochote kwa ajili ya Mwenyezi Mungu kama wanavyotoa katika kulinda mali na mamlaka?!
Hakika heshima ya umma bado inaishi katika vifua vya watu huru, lakini ushindi kamili hautapatikana isipokuwa kwa hatua ya umma wote; kwa harakati za majeshi yake huko Misri, Uturuki, Pakistan na kwingineko.. kwa kubomoa viti vya enzi vya uhaini na usawazishaji ambavyo vimeuza Palestina katika soko la utumwa, kwa kusimamisha Khilafah ya pili iliyoongoka kwa njia ya Utume, ambayo inaunganisha umma katika chombo kimoja, na kubeba Uislamu kwa ulimwengu kwa ulinganiaji na jihad, na kujibu mshambulizi na kukata mkono wa mkaidi.
Suluhisho si katika makongamano wala katika mipango, bali katika kusimamisha mamlaka ya Uislamu, na kila mpango wa kisiasa, kwa upatanishi wa Amerika au Magharibi, si chochote ila ni kisingizio cha kuendeleza uhalifu. Na udhalili hautaondolewa kwa umma, wala Masjid al-Aqsa haitarudishwa, wala damu ya watu wa Gaza na Palestina haitasimama, isipokuwa kwa harakati za umma kwa ufahamu, chini ya uongozi makini na mwaminifu, ambao unakubali mradi wa kimungu ambao haukubali ukafiri, wala haukubali nusu suluhisho. Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alisema: «Kisha kutakuwa na Khilafah kwa njia ya Utume» (Imesimuliwa na Ahmad).
Enyi umma wa Kiislamu: Je, haijafika wakati wa kuamka? Je, haijafika wakati wa sauti ya Al-Mu'tasim na Salah al-Din kusikika tena? Je, haijafika wakati wa kuisafisha ardhi yako kutoka katika uchafu wa Mayahudi na vibaraka? Naapa kwa Mungu kwamba mtaulizwa, na hakika historia haitasamehe, na hakika Mwenyezi Mungu atakuuliza kuhusu kila upungufu na kukukatisha tamaa. ﴿Na watajua wale waliodhulumu ni marejeo gani watarejea﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Bahaa Al-Husseini - Jimbo la Iraq