Ni lini Umma wa Kiislamu utagundua kuwa vita ni vita ya kuwepo?
Habari:
Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu ilitangaza siku ya Ijumaa kwamba Wapalestina 1,373 wameuawa, wengi wao kwa risasi za jeshi la Wayahudi, wakati wakisubiri misaada katika Ukanda wa Gaza, ambapo watu wake wanakabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula tangu mwishoni mwa Mei. Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Maeneo ya Palestina ilisema katika taarifa kwamba "Kwa jumla, tangu Mei 27, Wapalestina wasiopungua 1,373 wameuawa walipokuwa wakijaribu kupata chakula, 859 kati yao karibu na maeneo ya Shirika la Kibinadamu la Gaza linaloungwa mkono na Amerika na taasisi ya Kiyahudi, na 514 kando ya njia za msafara wa chakula." (Sky News Arabia, kwa muhtasari)
Maoni:
Habari zinaendelea kuenea kuhusu uhalifu wa taasisi ya Kiyahudi ambayo inafanya dhidi ya watu wa Gaza kwa kuwalenga kila mahali (nyumba - masoko - kambi na hata hospitali) katika ukiukaji mkubwa wa sheria na mikataba yote ya kimataifa, na inaendelea na ukaidi wake kuwazuia kupata misaada ya chakula na matibabu ili mateso yao yaongezeke, na kufa kwa njaa wale ambao wamenusurika kifo kwa mabomu na makombora.
Watu wa Gaza leo wana njaa na watoto wao wanakufa kwa njaa na hakuna wa kuwalilia. Watoto, vijana, na hata wanawake hutoka kupata misaada ambayo taasisi hiyo wahalifu wanawafanyia hisani kwa kuruhusu kuingia, si kwa sababu nyingine ila kutuliza hasira na chuki yao kwao na kugeuza vituo hivi - ambavyo wasio na hatia hawa wanadhani kuwa ni boti zao za kuokoka kutoka kwa kifo cha njaa - kuwageuza kuwa mitego ambayo ni rahisi kwao kuwinda idadi kubwa ya wahasiriwa, na kuwageuza kuwa vituo ambavyo maporomoko ya damu ya wasio na hatia hutoka, ambao walifikiri kwamba watapata tonge la mkate linalowahakikishia maisha, lakini - kwa ukatili wote - wananyang'anywa.
Mashirika haya ya kimataifa yanaendelea kuwadanganya watu ili kujitokeza mbele yao wakilaani, hawawezi kukubali kile ambacho taasisi ya Kiyahudi inafanya ya vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Gaza, ambayo inafanya kazi chini ya bendera ya nchi kubwa zinazoiunga mkono taasisi hiyo vamizi. Lakini vinyago vimeanguka mbele ya vita hivi ambavyo vimefunua ukweli, na kuonyesha watawala ambao hawasiti kuhalalisha ukiukaji na uhalifu wa taasisi hii, wakidai kwamba ni kujitetea na kwamba ni vita dhidi ya ugaidi na magaidi, ili ionekane kwamba wao ni dini moja inayoungana kuondoa Waislamu, kwa hivyo ni vita ya kuwepo ambayo lazima wapigane na kusaidiana.
Ukweli pia umeonyesha watawala wa Kiarabu wenye njama ambao hawajibu wito wa watu wao wanaopiga kelele kuwasaidia watu wao, na wanalinda mipaka iliyoundwa na maadui kudhoofisha taifa na kulifanya liwe limegawanyika na lisilo na umoja. Mipaka hii ambayo ilirarua mwili mmoja ambao Mtume ﷺ aliuacha ukiwa salama na wenye afya njema unaongoza ulimwengu, uliurarua na ilikuwa rahisi kuushambulia na kuushinda.
Hali ya watu wa Gaza, Palestina kwa ujumla, na nchi zote za Waislamu inataka ulazima wa kuunganisha utengano na kuleta pamoja umoja ili juhudi ziunganishwe na kushinda dini ya ukafiri ambayo inaruhusu damu yao, heshima zao, na kupora utajiri wao, na wamekusanyika na kuungana katika vita dhidi ya Uislamu na watu wake.
Je, umma wa Kiislamu utagundua lini kwamba vita ni vita ya kuwepo na ni lazima kuungana chini ya bendera ya Uislamu na kupigana na maadui, kuvunja nguvu zao, na kuinua neno la Mungu?!
Imeandikwa kwa ajili ya Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Zina Al-Samet