Mkataba wa Julai Ni Mradi wa Kilimwengu na Ni Usaliti kwa Watu wa Bangladesh
Habari:
Pendekezo la Kamati ya Kitaifa ya Maridhiano la kutoa amri ya utendaji ya kutekeleza Mkataba wa Kitaifa uliotolewa mwezi Julai (Marekebisho ya Katiba), na kufanya kura ya maoni kwa msingi wake, limezua mgawanyiko mkubwa miongoni mwa vyama vya siasa, na kutoelewana miongoni mwa wanasheria kuhusu msingi wake wa kikatiba. Mzozo huo unaelekea pande mbili: kisiasa kuhusu iwapo amri itatolewa na rais au mshauri mkuu wa serikali ya mpito. Na kisheria kuhusu iwapo amri na kura ya maoni kama hiyo inawezekana kabisa ndani ya mfumo wa katiba uliopo.
Maoni:
Kamati ya Kitaifa ya Maridhiano imeshindwa kutatua tofauti kuhusu Mkataba wa Kitaifa uliotolewa mwezi Julai, bali imefichua kasoro zake za kimsingi, hati hiyo badala ya kuunganisha Bangladesh, imekuwa sababu ya mgawanyiko na usaliti kwa matarajio ya watu wake. Mkataba unazingatia mageuzi ya kimuundo katika mfumo wa kidemokrasia na utawala, kana kwamba damu ya watu iliyomwagika dhidi ya utawala wa Hasina ilikuwa kwa ajili ya mageuzi ya kidemokrasia!
Dibaji ya mkataba inatoa wito kwa matakwa ya watu wakati wa uasi wa watu, lakini inapuuza waziwazi kutaja Uislamu ambao ndio kiini cha utambulisho wa watu wa Kibengali. Huu ni upotoshaji wa historia, kwani unaonyesha uasi kama mradi wa kilimwengu tu, na unafuta ukweli kwamba msukumo mkuu nyuma yake ulikuwa matarajio ya vijana na umma kupindua utawala wa kimabavu kutokana na mtazamo wa Kiislamu.
Hii inathibitisha kwamba mkataba si chochote ila chombo mikononi mwa serikali ya mpito inayoungwa mkono na Magharibi ili kuondoa uwepo wowote wa kisiasa wa asili ya Kiislamu kutoka kwenye uwanja wa umma. Na inatuma ujumbe wazi na wa kutisha: Ikiwa unataka kushiriki katika siasa, basi lazima uachane na utambulisho wako wa asili wa Kiislamu kwa niaba ya toleo la kilimwengu ambalo linakubaliwa na Magharibi na serikali!
Mizozo ya sasa ya kisiasa ni dalili tu za kasoro hii kubwa ya kimuundo. Siasa za kilimwengu nchini Bangladesh zina historia ndefu ya mgawanyiko na kushindwa. Zimepunguza utawala kuwa mchezo wa mapambano ya madaraka, na mbio za kichaa kati ya wenye tamaa, ambapo mjadala hauhusu lengo au maadili ya utawala, bali kuhusu taratibu na umbo lake. Mjadala kuhusu mkataba wa Julai si mjadala kuhusu maono ya kitaifa, bali ni mzozo kati ya wasomi kuhusu nani anakaa juu ya meza iliyooza yenyewe.
Kuangushwa kwa Hasina kulikuwa ni lazima, lakini usaliti wa serikali ya mpito, udanganyifu wa vyama vya siasa vya awali na kutokuwa na uwezo kwake, unafichua ukweli wa kina zaidi; ambayo ni kwamba tatizo letu si katika serikali bali katika mfumo wenyewe. Bangladesh haihitaji serikali mpya, bali mfumo mpya. Na hatuwezi kuendelea kuweka kiraka cha kidemokrasia kilichoshindwa kwenye jeraha linalohitaji matibabu ya kimsingi. Bangladesh inatamani siasa mbadala, mfumo mbadala wa utawala, uongozi mbadala, na mtindo mbadala wa maisha. Watu wamechoshwa na ahadi tupu za mifumo ya kidunia ambayo inaweka mamlaka juu ya kanuni, na chama juu ya taifa.
Umefika wakati wa kupita udanganyifu huu wa kidemokrasia. Mabadiliko ya kweli tunayoyatafuta hayatatimia katika vifungu vya mkataba ulioharibika au katika kumbi za bunge la kilimwengu, bali katika kupitisha mfumo unaotuunganisha chini ya bendera ya itikadi yetu, mfumo unaozingatia haki ya kimungu, rehema ya kweli na uongozi unaotumikia taifa si wao wenyewe. Bangladesh haingojei chama kingine cha kilimwengu, bali inangojea mabadiliko ya kweli ambayo hayatatimia ila kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa misingi ya unabii, kwani ndio mkataba wa kweli, na mustakabali pekee unaoahidi ukombozi na heshima.
Imeandikwa kwa Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Irtidaa Chowdhury - Jimbo la Bangladesh