Ukimya wa Al-Azhar na Mwangwi wa Mauaji: Taarifa ya Mnyonge Haiokoi Gaza
Ukimya wa Al-Azhar na Mwangwi wa Mauaji: Taarifa ya Mnyonge Haiokoi Gaza

Mitandao ya kijamii ilizuka kwa mjadala kati ya watumiaji kufuatia kitendo cha Al-Azhar Al-Sharif kufuta taarifa yake ndefu ambayo Sheikh wa Al-Azhar Ahmed Al-Tayeb alielekeza wito wa kimataifa wa hatua za haraka kuokoa Gaza kutoka kwa njaa kali. Taarifa ya Al-Azhar ilisisitiza kuwa dhamiri ya kibinadamu iko hatarini kutokana na mauaji yanayoendelea ya Wapalestina huko Gaza, ikionya kwamba yeyote anayeunga mkono Israel kwa silaha au anaiunga mkono kwa maamuzi anachukuliwa kuwa mshiriki wa moja kwa moja katika mauaji hayo.

0:00 0:00
Speed:
July 27, 2025

Ukimya wa Al-Azhar na Mwangwi wa Mauaji: Taarifa ya Mnyonge Haiokoi Gaza

Ukimya wa Al-Azhar na Mwangwi wa Mauaji: Taarifa ya Mnyonge Haiokoi Gaza

Habari:

Mitandao ya kijamii ilizuka kwa mjadala kati ya watumiaji kufuatia kitendo cha Al-Azhar Al-Sharif kufuta taarifa yake ndefu ambayo Sheikh wa Al-Azhar Ahmed Al-Tayeb alielekeza wito wa kimataifa wa hatua za haraka kuokoa Gaza kutoka kwa njaa kali. Taarifa ya Al-Azhar ilisisitiza kuwa dhamiri ya kibinadamu iko hatarini kutokana na mauaji yanayoendelea ya Wapalestina huko Gaza, ikionya kwamba yeyote anayeunga mkono Israel kwa silaha au anaiunga mkono kwa maamuzi anachukuliwa kuwa mshiriki wa moja kwa moja katika mauaji hayo. Lakini taarifa hii haikuchapishwa kwa dakika chache tu kabla ya kufutwa kutoka kwa akaunti za Al-Azhar kwenye majukwaa ya mawasiliano ya elektroniki, ambayo ilizua mshangao mkubwa kati ya waendeshaji wa ulimwengu wa mtandao. (Al-Jazeera)

Maoni:

Baada ya ukimya mrefu kutoka kwa Al-Azhar na wasomi wake kuhusu mauaji ambayo watoto wachanga huzeeka kutokana nayo, ambayo yanatokea karibu nao, na baada ya kupita takriban miaka miwili tangu kuuawa na kulazimishwa njaa watu wa Gaza, hadi hali ilipofikia hivi karibuni kufa kwa njaa juu ya vifo vyao kwa mauaji na unyanyasaji, na baada ya sauti za watu wa Gaza kupotea huku wakiwasihi majirani zao kuwasaidia, na walipoteza matumaini ya msaada wao, walitosheka kwa kutoa wito wa kufunguliwa kwa kivuko cha Rafah... Na baada ya... Baada ya... Uchungu ulizuka katika Al-Azhar na wasomi wake, hivyo wakatoa taarifa hafifu ambayo hutolewa tu na mtu asiye na uwezo!

Al-Azhar ilitoa wito wa dharura wa kimataifa kwa "nguvu huru na zenye ushawishi za dhamiri" kuchukua hatua mara moja kuokoa watu wa Gaza kutoka kwa njaa kali na kubwa iliyoanzishwa na Wayahudi, kana kwamba Al-Azhar inajiweka nje ya wito huu, haihusiani nao, na haivutiwi nao, lakini kama taasisi ya kibinadamu iliyo mbali na Gaza kama umbali wa mashariki! Na taarifa yake inakaribia kufanana na matamshi ya mnafiki wa Uturuki, Erdogan, ambaye alisema: "Ubinadamu unakata roho huko Gaza, na watoto wanakabiliwa na njaa kali katikati ya uhaba wa misaada, akiomba jamii kuimarisha msimamo wa kimaadili wa haraka na endelevu", na akachukulia hilo kama "mauaji ya kimbari kamili".

Msimamo huu wa woga unafanana na msimamo wa Al-Azhar, ambao ulisisitiza kwamba "kulenga maeneo ya makazi ya wakimbizi na vituo vya usambazaji wa misaada kwa risasi za moto ni uhalifu". Pia ilithibitisha kuwa "yeyote anayeunga mkono Israel kwa silaha au uamuzi anachukuliwa kuwa mshiriki katika uhalifu huu", ikionya kwa misemo ya marudio kama vile: "Wenye dhuluma watajua ni mgeuko gani watageukia". Msimamo huu unaendana na msimamo wa Erdogan mshiriki katika njama dhidi ya Gaza na mfuasi wa Wayahudi, ambaye pia alisema: "Yeyote anayenyamaza juu ya mauaji ya kimbari huko Gaza anakuwa mshiriki wa Israel katika uhalifu wake dhidi ya ubinadamu", akiomba msimamo wa kimataifa wa kibinadamu wazi "kuonyesha kukataa dhuluma".

Wote wawili, Al-Azhar na mnafiki Erdogan, wanazungumza kwa lugha ya mtu wa tatu na mtumaji, kana kwamba uhalifu unaotendeka huko Gaza hauwahusu, na sio jukumu lao, lakini jukumu la wengine walioshiriki katika njama dhidi ya watu wa Gaza, katika mfumo wa kimataifa na mashirika yake! Na Al-Azhar ilitosheka na kushambulia ukimya wa kimataifa na ukosefu wa uwajibikaji wa kibinadamu, na ililaani kupuuzwa kwa ulimwengu kwa kile kinachotokea huko Gaza, bila kushambulia ukimya wa serikali ya Misri, na usingizi wa jeshi lake, na ukimya wa wasomi wake kuhusu kuchochea jeshi la Kinana kupigana na Wayahudi, kana kwamba hawajasoma kauli Yake Mwenyezi: ﴿EWE NABII, WACHEKENI WAUMINI KUPIGANA﴾!

Licha ya matamshi haya hafifu, taarifa za ulegevu, na misimamo ya woga, Wayahudi na washirika wao kutoka kwa watawala wa Misri hawakufurahishwa hata na kiwango hiki cha kukata tamaa na woga, hivyo waliamuru wasomi wa mamlaka katika Al-Azhar Al-Sharif kurudi kwenye usingizi na ukimya wao, na kutoa maneno yao ambayo yanaweza kumfanya mtu afikiri kuwa yana moto, hivyo wakameza ndimi zao bila aibu kutoka kwa Mungu au kutoka kwa waja Wake. Vipi sivyo, wanawaogopa makafiri zaidi kuliko wanavyomuogopa Mwenyezi Mungu! Kama Alivyosema Mwenyezi: ﴿JE, HUWAONI WALE WALIOAMBIWA ZUIENI MIKONO YENU NA SIMAMISHENI SWALA NA TOENI ZAKA, ULIPOANDIKWA JUU YAO PIGANO, TAZAMA, KUNDI KATIKA HAO LAWAOGOPEA WATU KAMA WANAVYOMUOGOPEA MWENYEZI MUNGU AU ZAIDI KATIKA UOGA﴾.

Sababu ya kukataliwa na kulaaniwa na Wayahudi hata kwa misimamo hii hafifu sio kwa sababu ni ya ujasiri au ya kutisha kwao, wanajua kuwa ni taarifa tu za kulinda heshima, zilizotolewa tu baada ya shinikizo kutoka mitaani ya Waislamu, ambao wana hasira kali kwa ndugu zao huko Gaza. Ilikuwa lazima kwa watoleaji wa taarifa hizi kutoa kitu ambacho kingetuliza watu, sio kwa nia ya kuchochea majeshi kufanya jihad, ambayo ndiyo inawatisha Wayahudi kweli. Hawakuuelekeza hotuba isipokuwa kwa pande zisizojulikana, au zenye msimamo upande wa Wayahudi, lakini Wayahudi wanaogopa kwamba minong'ono hii inaweza siku moja kuwa sauti za kweli za uaminifu ambazo zinatoa wito kwa majeshi ya Waislamu kuchukua hatua mara moja, kuondoa viti vya enzi, kupigana na Wayahudi, na kukomboa nchi na watu kutoka kwa maovu yao. Hili ndilo linalowaogopesha Wayahudi na watawala wa Waislamu.

Lau kama wasomi wa Al-Azhar wangekuwa wazito na waaminifu kwa Mungu kweli, wangewaeleza watu hukumu ya kisheria, na njia iliyo wazi ambayo inaongoza kweli kuvunja mipaka, na imekuwa wazi kwa kila mwenye kuona na busara, nayo ni: kuondoa viti vya enzi vya watawala wanaounga mkono Wayahudi na Wakristo, na kumsimika Khalifa mwadilifu ambaye anahukumu kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha, na kuhamasisha majeshi kusafisha ardhi iliyobarikiwa kutoka kwa uchafu wa Wayahudi.

Lakini hayawi... hayawi... Wasomi wa Al-Azhar - isipokuwa yule ambaye Mola wangu amemrehemu - wameridhia kuwa pamoja na watawala wa madhara, hivyo wakawa wasomi wa mamlaka, sio wasomi wa dini, na wakawa kama makasisi kutoka kwa watu wa Kitabu, ambao Mwenyezi Mungu amesema kuwahusu: ﴿NA MOLA ALIPOCHUKUA AHADI KUTOKA KWA WALE WALIOPEWA KITABU KUWA MTAUFAFANUA KWA WATU WALA MSIIFICHE, LAKINI WAO WAKAITUPA NYUMA YA MIGONGO YAO, NA WAKAUNUNUA KWA THAMANI NDOGO; BASI NI MABAYA YANAYO YANUNUA﴾!

Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Bilal Al-Muhajir – Jimbo la Pakistan

More from Habari na Maoni

Uturuki na Serikali za Kiarabu Zilitaka Hamas Iache Silaha

Uturuki na Serikali za Kiarabu Zilitaka Hamas Iache Silaha

(Imetafsiriwa)

Habari:

Mkutano wa ngazi ya juu wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa ulifanyika New York mnamo Julai 29 na 30, wenye kichwa "Kupata Suluhu ya Amani kwa Suala la Palestina na Utekelezaji wa Suluhu la Mataifa Mawili," ukiongozwa na Ufaransa na Saudi Arabia. Kufuatia mkutano huo, ambao ulikusudia kuitambua Palestina kama nchi na kumaliza vita huko Gaza, tamko la pamoja lilitiwa saini. Pamoja na Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Uturuki pia ilitia saini tamko hilo pamoja na nchi zingine 17. Tamko hilo, lililokuwa na vifungu 42 na kiambatisho, lililaani operesheni ya Al-Aqsa iliyofanywa na Hamas. Nchi zilizoshiriki ziliitaka Hamas iache silaha na kuwataka wakabidhi utawala wao kwa serikali ya Mahmoud Abbas. (Mashirika ya habari, Julai 31, 2025).

Maoni:

Kwa kuzingatia nchi zinazoendesha mkutano, ni wazi kuwepo kwa Amerika, na licha ya kutokuwa na mamlaka au ushawishi wa kufanya maamuzi, kuandamana kwa utawala wa Saudi, mtumishi wake, kwa Ufaransa ni ushahidi dhahiri wa hilo.

Katika suala hili, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema mnamo Julai 24 kwamba Ufaransa itatambua rasmi taifa la Palestina mnamo Septemba, na itakuwa nchi ya kwanza kutoka kwa kundi la nchi saba kufanya hivyo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Faisal bin Farhan Al Saud na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noël Barot walifanya mkutano na waandishi wa habari katika mkutano huo, wakitangaza malengo ya tamko la New York. Kwa kweli, katika taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo, mauaji ya kimbari ya chombo cha Kiyahudi yalilaaniwa bila kuchukua uamuzi wowote wa adhabu dhidi yake, na Hamas iliombwa kuacha silaha zake na kukabidhi utawala wa Gaza kwa Mahmoud Abbas.

Katika mkakati mpya wa Amerika wa Mashariki ya Kati ambao inataka kutekeleza kwa kuzingatia makubaliano ya Abraham, utawala wa Salman unawakilisha kichwa cha mkuki. Utawala wa kawaida na chombo cha Kiyahudi utaanza baada ya vita, na Saudi Arabia; kisha nchi zingine zitafuata, na wimbi hili litageuka kuwa muungano wa kimkakati unaoenea kutoka Afrika Kaskazini hadi Pakistani. Pia, chombo cha Kiyahudi kitapata dhamana ya kiusalama kama sehemu muhimu ya muungano huu; kisha Amerika itatumia muungano huu kama mafuta katika mapambano yake dhidi ya China na Urusi, na kujumuisha Ulaya yote chini ya mabawa yake, na kwa kweli, dhidi ya uwezekano wa kuanzishwa kwa Ukhalifa.

Kizuizi kwa mpango huu kwa sasa ni vita vya Gaza na kisha hasira ya umma, ambayo inaongezeka, na inakaribia kulipuka. Kwa hivyo, Marekani ilipendelea Umoja wa Ulaya, tawala za Kiarabu na Uturuki kuchukua hatamu katika tamko la New York. Ikidhani kwamba kukubalika kwa maamuzi yaliyomo kwenye tangazo itakuwa rahisi.

Ama serikali za Kiarabu na Uturuki, kazi yao ni kumridhisha Marekani, na kulinda chombo cha Kiyahudi, na badala ya utiifu huu, kujilinda na hasira ya watu wao, na kuishi maisha ya unyonge na makombo ya mamlaka duni hadi watupwe au kuadhibiwa kwa mateso ya akhera. Hifadhi ya Uturuki juu ya tangazo, mradi tu utekelezaji wa kile kinachoitwa mpango wa suluhisho la mataifa mawili, ni jaribio tu la kufunika lengo halisi la tangazo na kupotosha Waislamu, na haina thamani yoyote ya kweli.

Kwa kumalizia, njia ya ukombozi wa Gaza na Palestina yote sio kupitia taifa la uwongo ambalo Wayahudi wanaishi. Suluhisho la Kiislamu kwa Palestina ni utawala wa Uislamu katika ardhi iliyoporwa, na ni kupigana na mporaji, na kuhamasisha majeshi ya Waislamu kuwang'oa Wayahudi kutoka ardhi iliyobarikiwa. Na suluhisho la kudumu na la msingi ni kuanzisha Ukhalifa Uongofu na kulinda ardhi ya Israa na Mi'raj iliyobarikiwa na ngao ya Ukhalifa. Mungu akipenda, siku hizo haziko mbali.

Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alisema: «Saa haitasimama mpaka Waislamu wapigane na Wayahudi, na Waislamu watawaua, mpaka Myahudi atajificha nyuma ya jiwe na mti, kisha jiwe au mti utasema: Ewe Muislamu, Ewe mja wa Mwenyezi Mungu, huyu Myahudi yuko nyuma yangu, njoo umuue» (Imesimuliwa na Muslim)

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Muhammad Amin Yildirim

Kile ambacho Amerika inataka ni kutambuliwa rasmi kwa taifa la Kiyahudi, hata kama silaha itabaki

Kile ambacho Amerika inataka ni kutambuliwa rasmi kwa taifa la Kiyahudi, hata kama silaha itabaki

Habari:

Habari nyingi za kisiasa na kiusalama nchini Lebanon zinahusu suala la silaha inayolenga taifa la Kiyahudi, bila silaha nyingine yoyote na kulizingatia na wachambuzi wengi wa kisiasa na wanahabari.

Maoni:

Amerika inaomba kukabidhiwa silaha iliyopigana na Wayahudi kwa jeshi la Lebanoni, na haijalishi silaha yoyote itakayobaki mikononi mwa watu wote ambayo inaweza kutumika ndani ya nchi itakapoona faida yake au kati ya Waislamu katika nchi jirani.

Amerika, adui yetu mkuu sisi Waislamu, ilisema waziwazi, bali kwa ukosefu wa adabu, wakati mjumbe wake Barrack alipotamka kutoka Lebanon kwamba silaha ambayo lazima ikabidhiwe kwa serikali ya Lebanoni ni silaha ambayo inaweza kutumika dhidi ya taifa la Kiyahudi linalonyakua Palestina iliyobarikiwa, na sio silaha nyingine yoyote ya mtu binafsi au ya kati kwa sababu hii haidhuru taifa la Kiyahudi, bali inawahudumia na inahudumia Amerika na nchi zote za Magharibi katika kuhamasisha mapigano kati ya Waislamu kwa kisingizio cha watu wenye msimamo mkali au wenye itikadi kali au watu wa kale au walio nyuma, au maelezo mengine ambayo wao huyaeneza kati ya Waislamu kwa kisingizio cha madhehebu au utaifa au ukabila, au hata kati ya Waislamu na wengine ambao wameishi nasi kwa mamia ya miaka na hawakupata kutoka kwetu ila kuhifadhi heshima, mali na roho, na kwamba tulikuwa tunatumia sheria juu yao kama tunavyozitumia juu yetu wenyewe, wanayo yao na wanayo juu yao. Hukumu ya kisheria ndiyo msingi wa hukumu kwa Waislamu, iwe kati yao, au kati yao na raia wengine wa dola.

Na maadamu adui yetu mkuu Amerika anataka kuharibu au kutoa upande silaha ambayo inaumiza taifa la Kiyahudi, kwa nini wanasiasa na wanahabari wanaangazia hilo?!

Na kwa nini mada muhimu zaidi zinaibuliwa kwenye vyombo vya habari na katika baraza la mawaziri, kwa ombi la adui wa Kimarekani, bila kuzichunguza kwa kina na kufafanua ukubwa wa hatari yake kwa umma, na hatari zaidi kati yao ni kuchora mipaka ya nchi kavu na taifa la Kiyahudi, ambayo ni kutambua taifa hili la wanyang'anyi rasmi, na kwa namna ambayo hakuna mtu atakayeweza kubeba silaha baada ya hapo, silaha yoyote kwa ajili ya Palestina, ambayo ni mali ya Waislamu wote na sio watu wa Palestina pekee, kama wanavyojaribu kutushawishi kana kwamba inawahusu watu wa Palestina pekee?!

Hatari ni katika kuibua suala hili mara moja chini ya kichwa cha amani, na mara nyingine chini ya kichwa cha upatanisho, na nyingine chini ya kichwa cha usalama katika eneo hilo, au chini ya kichwa cha ustawi wa kiuchumi, utalii na kisiasa, na ustawi ambao wanaahidi Waislamu ikiwa watatambua chombo hiki kilichopotoka!

Amerika inajua vizuri kwamba Waislamu hawawezi kukubali kutambua taifa la Kiyahudi kamwe, na ndiyo maana unaiona inawapenyeza kupitia mambo mengine ili kuwatoa akili zao kutoka kwa jambo muhimu zaidi la hatima. Ndiyo, Amerika inataka tuangazie suala la silaha, lakini inajua kwamba silaha, haijalishi ni yenye nguvu kiasi gani, haitafaa na haiwezi kutumika dhidi ya taifa la Kiyahudi ikiwa Lebanon rasmi itatambua kwa kuchora mipaka nayo, na kwa kufanya hivyo itakuwa imetambua na kustahili kwake ardhi ya Palestina iliyobarikiwa, ikisingizia watawala wa Kiislamu, na mamlaka ya Palestina.

Utambuzi huu wa taifa la Kiyahudi ni usaliti kwa Mungu na Mtume wake na kwa waumini, na kwa damu yote ya mashahidi ambayo ilimwagwa na bado inamwagwa kwa ajili ya ukombozi wa Palestina, na licha ya yote hayo bado tunatumai mema katika taifa letu ambalo baadhi yao wanapigana huko Gaza Hashem na Palestina, na wanatuambia kwa damu yao: Hatutatambua taifa la Kiyahudi kamwe, hata kama itatugharimu haya yote na zaidi... Je, tunakubali nchini Lebanon kutambua taifa la Kiyahudi haijalishi hali ni ngumu kiasi gani?! Na je, tunakubali kuchora mipaka nalo, yaani, kulikubali, hata kama silaha itaachwa nasi?! Hili ni swali ambalo lazima tulijibu kabla halijachelewa.

Imeandikwa kwa ajili ya idhaa ya ofisi ya habari kuu ya Hizb ut-Tahrir

Dkt. Muhammad Jaber

Mkuu wa kamati ya mawasiliano kuu ya Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Lebanon