Shirika la Fedha la Kimataifa Lapanda Miiba kwa Watu wa Imani
Hivyo Wasitarajie Kuvuna Tendegu
Habari:
Tovuti ya Yemen Press iliripoti mnamo Novemba 11 habari yenye kichwa "Shirika la Fedha la Kimataifa lawabashiria Wayemen na kufichua habari njema na za furaha ambazo Waarabu wote wamesubiri kuzisikia!!" ambayo ilisema: "Katika ripoti mpya, shirika hilo lilifichua matarajio ya ukuaji wa kiuchumi kwa Yemen kwa asilimia 0.5 kwa mwaka 2026, ambayo ni asilimia inayoonekana kuwa ya kawaida lakini ina maana kubwa ya ishara: mwanzo wa mabadiliko kutoka uchumi ulioharibika hadi mwingine unaosonga kwa hatua polepole kuelekea maisha.
Katika mji mkuu wa Jordan, Amman, ambako mashauriano yanaendelea kati ya ujumbe wa shirika hilo na maafisa wa Yemen, kuna hali ya tahadhari na matumaini".
Maoni:
Ripoti hii ilikuja siku mbili baada ya mkutano wa Rashad al-Alimi na Waziri Mkuu na Waziri wa Fedha Salem bin Buraik, na Gavana wa Benki Kuu huko Aden, Ahmed Al-Ma'abaqi, kuanza mchakato wa utekelezaji wa mageuzi kamili ya kiuchumi ambayo waliidhinisha badala ya Shirika la Fedha la Kimataifa kutoa mikopo iliyoelekezwa na masharti kutoka kwa jumuiya ya wafadhili, muhimu zaidi ikiwa ni pamoja na ukombozi wa dola ya forodha na kufuata viwango vya kimataifa, na kufungua nchi kwa Mamlaka ya Uwekezaji wa Kimataifa, kama sharti la msingi kwa mchakato wa kufufua uchumi nchini Yemen.
Ufufuo gani wa kiuchumi tunatarajia, wakati Shirika la Fedha la Kimataifa linakiri wazi katika ripoti yake kwamba "uboreshaji wa maisha ya raia wa kawaida bado haufikiki"?!
Hii hapa wizara ya Bin Buraik, kama ilivyokuwa hapo awali, bado haiwezi kulipa mishahara ya wafanyakazi wa serikali kwa miezi, na hapa mko kwenye hatihati ya kuhamisha umeme kwa makampuni binafsi, ambayo bei zao zitawaua, na kesho itakuwa zamu ya taasisi ya maji na afya... na kadhalika, huku rasilimali za mali yenu ya umma zikiporwa?!
Shirika la Fedha la Kimataifa halijaingia nchi yoyote isipokuwa limeiharibu, na limefanya uchumi wake uwe chini ya udhibiti wa makampuni ya matajiri wa ulimwengu wa Magharibi, kama ilivyotokea Ecuador na dada zake, Indonesia, Misri na wenzao. Hakika Rashad al-Alimi, Salem bin Buraik na Ahmed Al-Ma'abaqi, na Gavana wa Yemen katika Kundi la Benki ya Dunia, Wa'ed Badheeb, wanaingiza Yemen kwenye madeni. Hivyo msingoje nchi yenu iharibiwe huku mkiangalia, simameni imara mbele yao, kwa sababu lengo ni kuzamisha Yemen katika makumi ya mabilioni ya madeni badala ya dola bilioni 7! Na aminini kwamba mpango wa Mola wenu katika mfumo wa kiuchumi katika Uislamu chini ya dola ya Khilafa Rashidun ya pili kwa njia ya utume, ndio mwokozi wenu kutoka kwa matatizo ya kiuchumi mnayoyakabili. Amesema Mtukufu: ﴿Na utafute kwa yale aliyokupa Mwenyezi Mungu makazi ya Akhera, wala usisahau fungu lako la dunia, na fanya wema kama Mwenyezi Mungu alivyokufanyia wema, wala usitafute uharibifu katika ardhi. Hakika Mwenyezi Mungu hawapendi waharibifu﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Mhandisi Shafiq Khamis – Wilaya ya Yemen