Picha Yenye Maneno Elfu Moja
Habari:
Tukio la Ahmed Al-Sharaa (Al-Jawlani) akiingia Ikulu ya White House kupitia mlango wa nyuma bila Trump kumlaki mlangoni.
Picha yake na waziri wake wa mambo ya nje wakiwa wameketi kuelekeana na Trump kama wafanyakazi wengine wa Ikulu ya White House badala ya kuketi kando yake.
Picha ya Ahmed Al-Sharaa amesimama kando ya ofisi ya Rais wa Marekani aliyekuwa ameketi kwenye kiti chake.
Ama zawadi ya Trump kwa Al-Jawlani ni kofia iliyoandikwa MAGA yaani "Tuifanye Amerika kuwa kuu tena."

Maoni:
Rais wa mwisho wa Syria kuzuru Amerika alikuwa mwaka 1946, na baada ya karibu miaka 80 Washington inampokea rais wa sasa wa Syria. Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Wahamiaji ya Syria ilisema "kwa maelekezo ya Rais Trump, mkutano wa kazi ulifanyika uliowajumuisha Waziri wa Mambo ya Nje na Wahamiaji Bw. Asaad Hassan Al-Shibani na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Bw. Marco Rubio na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Bw. Hakan Fidan, kufuatilia yaliyokubaliwa kati ya marais hao wawili na kuweka njia wazi za utekelezaji."
Kwa hivyo ambaye alichagua umbo la mkutano, maelezo yake na nani ahudhurie (ikiwa ni pamoja na waziri wa mambo ya nje wa Uturuki) ni Trump. Trump hamtazami Ahmed Al-Sharaa kama mkuu wa nchi kwa maana ya neno, bali fomyula na umbo la mapokezi linathibitisha kuwa anampokea kijana wa Erdogan si zaidi, na kwa sababu hii kila picha iliyorushwa ilikusudiwa na inabeba ujumbe mwingi kwa kila mwenye macho. Kwa upande mwingine, Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria ilichapisha picha ya Trump akisalimiana na Ahmed Al-Sharaa mbele ya ofisi yake katika Ikulu ya White House, ama picha nyingine haionekani katika injini za utafutaji, je, ilikuwa ni kosa tu?
Swali linaloulizwa ni jinsi gani Ahmed Al-Sharaa anakubali kudhalilishwa huku?! Mtu anaweza kusema kuwa hizi ni taratibu tu na mapambo ambayo hayakanushi kiasi cha maslahi ambayo Syria itapata baada ya kuondolewa vikwazo dhidi ya Al-Jawlani katika Baraza la Usalama na kusimamisha kazi katika sheria ya Kaisari kwa siku 180. Na wamesahau au wamepuuza kwamba gharama ni kubwa sana na haitaleta Syria ila ole na uharibifu; iwe kukubali uanzishwaji na kuendeleza misingi ya kijeshi ya Marekani nchini Syria na maana yake ya udhibiti wa moja kwa moja wa nchi, au kujiunga na muungano dhidi ya Uislamu, au ilikuwa hiyo kwa kufungua nchi kwa makampuni ya kibepari ili kunyakua utajiri wake kwa kisingizio cha kuhimiza uwekezaji na kwenda kwa hatua za haraka kuelekea kurejesha uhusiano na shirika la Kiyahudi na kuachana na Golan.
Al-Jawlani anafanya yote hayo na kinyume chake haruhusiwi hata picha ya kumbukumbu akiwa amesimama kama mkuu wa nchi kando ya Trump, ikizingatiwa kuwa picha kama hiyo si heshima hata kidogo kwa Muislamu, vipi picha hizo ambazo karibu zinatamka Ahmed Al-Sharaa ni nani, kazi yake ni nini na jinsi Trump anavyomwangalia!
Ama kofia ya Maga, hiyo ni dharau nyingine na ujumbe mkuu... lau wangejua!
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Hossam El-Din Mustafa