Mlima ulizaa panya!
Habari:
Baada ya siku ndefu ya kazi iliyodumu kwa saa kumi, mawaziri wa mambo ya nje wa Kiarabu walitoka katika mkutano wao wa kawaida huko Cairo na uamuzi muhimu, ambao unajumuisha makubaliano ya Kiarabu kwamba mpango wa shirika la Kiyahudi unazidi vita vya mauaji ya halaiki huko Gaza hadi jaribio la kumaliza suala la Palestina kwa uhamishaji au kuunganisha Ukingo wa Magharibi, hivi ndivyo alivyosema Abu El-Gheit, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, na pia alisema kwamba "Saudi Arabia na Misri zimeandaa rasimu ya azimio maalum kuhusu ushirikiano wa Kiarabu katika Mashariki ya Kati ambayo inasisitiza kanuni ya uhuru wa nchi za Kiarabu na inakataa dalili zozote za kuathiri uhuru huu" (Russia Leo - kwa marekebisho madogo, 2025/09/05).
Maoni:
Jumuiya ya Kiarabu haijasimama na haijawahi kuunga mkono suala lolote la Waislamu, lakini kinyume chake, ni chombo kutoka kwa vyombo vya Magharibi makafiri wakoloni ili kutawanya umoja wa Waislamu na kuimarisha mgawanyiko wao, na kumaliza suala la Palestina na kulifanya suala la Wapalestina pekee baada ya kuwa suala la taifa. Na kama nchi za Kiarabu wanachama wa jumuiya hii zingekuwa na nia ya dhati ya kutafuta suluhisho au kusimamisha vita vya mauaji ya halaiki huko Gaza, isingechukua masaa kumi ya kazi ngumu kama ilivyoelezwa na Abu El-Gheit. Amri ya kusimamisha mauaji haya ambayo hayajawahi kutokea katika historia haihitaji ila uamuzi wa ujasiri unaohitaji kusogeza majeshi yanayozunguka Palestina, kwa hivyo yashambulie kama mtu mmoja kwa shirika hili haramu na kung'oa mizizi yake. Jambo hilo ni rahisi, Ee Abu El-Gheit, na halihitaji mikutano au makumi ya masaa ya kazi, hii ni ikiwa kweli mnataka kukomboa Palestina, lakini ukweli unaoonekana na unaohisiwa ni kwamba mnashirikiana na Wayahudi na hata mnazuia aina yoyote ya msaada kwa watu wa Gaza. Na kile ambacho serikali za Misri na Jordan zinafanya cha kubadilishana kibiashara na mikataba ya kiuchumi na shirika hili la uhalifu ni ushahidi bora.
Kisha Abu El-Gheit anazungumzia rasimu ya azimio maalum iliyoandaliwa na Saudi Arabia na Misri, kuhusu ushirikiano wa Kiarabu katika Mashariki ya Kati, akisisitiza kanuni ya uhuru wa nchi za Kiarabu na kukataa dalili zozote za kuathiri uhuru huu, Mungu awaangamize nyinyi watawala vibaraka! Na tangu lini shirika la Kiyahudi limejali uhuru wenu ilhali daima mmeinama vichwa vyenu mbele yake na mnasimama wanyonge na watiifu? Na ni mara ngapi uhuru wenu unaodaiwa umevunjwa na Wayahudi hawakusikia kutoka kwenu ila kukemea na kulaani?! Na kama wangejua kuwa kuna wanaume ndani yenu, wasingethubutu Gaza na watu wake, na kama wangepata ndani yenu mtu anayenguruma kama simba, wangewaheshimu sana, lakini nyinyi hamko ila wachache wa vibaraka wanyonge, na huu ni ukweli ambao Wayahudi wanaujua vizuri, na kwa hivyo hawajali nyinyi na wala hawakuheshimu. Na ukweli huu huo huo umefahamika na watu wa Kiislamu na wameanza kutamani mabadiliko na wanaangalia njia ya utukufu na ufufuo.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Walid Buleibel