Mmeshutumu kwa miaka 77, haitoshi?!
Na je, mmebaki na mistari myekundu ambayo haijavukwa?
Habari:
Mkuu wa Idara ya Mawasiliano katika Ikulu ya Uturuki, Burhanettin Duran, alilaani vikali uvamizi uliofanywa na baadhi ya mawaziri katika shirika la Kiyahudi pamoja na makundi yenye misimamo mikali katika Msikiti wa Al-Aqsa chini ya ulinzi wa polisi. Duran alisema katika taarifa yake: "Kama alivyosisitiza Rais wetu, Bwana Recep Tayyip Erdoğan, Msikiti wetu wa Al-Aqsa, kibla chetu cha kwanza, ni mstari wetu mwekundu" (TV 24, 2025/08/04).
Maoni:
Shirika la Kiyahudi, tangu liliponyakua Palestina mwaka 1948, limefanya mauaji na uhalifu usiohesabika, na limefanya uvamizi usio na idadi katika Msikiti wa Al-Aqsa. Mbele ya ukiukwaji huu na uhalifu huu, watawala wasaliti waoga katika nchi za Kiislamu hawajafanya chochote isipokuwa kutoa shutuma. Bali waliendeleza homa hii ya kulaani, wakitosheka kwa kuinua dozi ya kulaani kidogo ili kugeuka kuwa kulaani vikali! Tangu mwaka 1948, hawajaweza kuvuka mraba wa kulaani hata kwa hatua moja. Na walichofanya, kama nilivyotaja, ni kuendeleza kulaani ili iwe kulaani vikali, lakini waliendelea kuwa mateka katika mzunguko ule ule wa kulaani na hawakuweza kutoka ndani yake!
Na kwa sababu shirika la Kiyahudi linajua kuwa wao ni waoga na vibaraka, na kwamba hawathubutu kuligusa au hata kulikuna bila kuchukua ruhusa kutoka kwa mabwana zao huko Amerika, liliendelea kufanya mauaji na uhalifu. Na liliendelea kulichafua na kulitia unajisi Msikiti wa Al-Aqsa, kana kwamba linawaziba midomo kwa matamko yao kwamba Msikiti wa Al-Aqsa ni mstari mwekundu. Kwa hivyo tunauliza: Mstari mwekundu wa Erdoğan uko wapi? Maadamu Msikiti wa Al-Aqsa ni kibla chake cha kwanza na mstari wake mwekundu, kwa nini umevukwa kwa miaka mingi wakati wa utawala wake wa miaka 23, na bado unakanyagwa hadi leo?! Ikiwa kweli ni mstari mwekundu, kwa nini anaruhusu kuvukwa na kukiukwa utakatifu wake? Na ikiwa sivyo, kwa nini anadai kuwa ni mstari mwekundu? Hii inathibitisha kuwa tamko la Erdoğan kuhusu "mstari mwekundu" ni maneno tu, au ni hotuba kwa ajili ya matumizi ya umma tu. Kwa sababu kama inavyojulikana, maneno pekee hayakomboi nchi wala hayamzuilii adui. Kwa sababu ikiwa kweli ulikuwa mstari wake mwekundu, angeuchukulia kama suala la kuwepo na suala la maisha au kifo, na angekusanya jeshi lake kubwa lililojificha kwenye kambi zao kwa ajili yake, hata kama ingemgharimu maisha ya mamilioni.
Hakuna shaka kwamba Msikiti wa Al-Aqsa una utakatifu wake, lakini kilicho kitakatifu zaidi kuliko huo ni damu ya Muislamu, na ushahidi wa hilo ni kwamba Mtume ﷺ aliuzungumzia Al-Kaaba tukufu siku moja wakati wa twawafu akisema: «Ni jinsi gani ulivyo mzuri na jinsi gani harufu yako ilivyo nzuri! Ni jinsi gani ulivyo mkuu na jinsi gani utakatifu wako ulivyo mkuu! Na kwa yule ambaye nafsi ya Muhammad iko mikononi mwake, utakatifu wa muumini ni mkuu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko wewe; mali yake na damu yake, na tumdhani ila kheri».
Ikiwa Msikiti wa Al-Aqsa ni mstari wenu mwekundu, basi ni bora zaidi kuwa damu ya Muislamu iwe mstari wenu mwekundu. Hii hapa damu ya Waislamu inatiririka kama mito huko Gaza kwa karibu miaka miwili, na idadi ya mashahidi imefikia elfu 70. Yule ambaye hahamishi majeshi yake kwa ajili ya damu ya Waislamu, ambayo ni takatifu zaidi kuliko Al-Kaaba na Msikiti wa Al-Aqsa na ni tukufu zaidi kuliko hizo, ni ujinga kutarajia kwamba atazihamisha kwa ajili ya Msikiti wa Al-Aqsa. Wanalaani ukiukwaji wa utakatifu wa Al-Aqsa, na pia wanalaani ukiukwaji na mauaji ya kilicho kitakatifu zaidi na kikubwa kuliko huo. Wao kwa urahisi hawawezi kuvuka mraba wa kulaani.
Laiti kungekuwa kumebakia chembe ya imani au heshima au ubinadamu kwa watawala wasaliti wa nchi za Kiislamu - akiwemo Erdoğan - wangekusanya majeshi yenye nguvu ya Waislamu chini ya amri yao, kama alivyofanya Al-Mu'tasim na Muhammad bin Qasim, ili kulipiza kisasi kwa damu ya Waislamu ambayo imekuwa ikitiririka kwa miaka miwili huko Gaza, bila kusahau damu ya watu wa Yemen, Afghanistan, Pakistan, Iraq na Syria, na kutetea heshima ya wanawake wa Kiislamu waliodhalilishwa, na kuwafukuza Wayahudi walioutia unajisi Al-Aqsa sio tu kutoka Palestina bali kutoka uso wa dunia! Lakini haiwezekani! Watawala wa leo wasaliti hawastahili hata kamba ya kiatu cha viongozi mashujaa wa Khilafah. Kwa hivyo hao watakumbukwa na historia kwa ushujaa, lakini watawala wa leo na haswa Erdoğan watakumbukwa kwa usaliti, na majina yao yataandikwa katika kurasa za historia kama wasaliti kwa kalamu isiyofutika. Na aibu hii haitaondolewa ila kwa kutangaza kwao Khilafah, na kulipiza kisasi kwa damu ya Waislamu, na kukomboa maeneo matakatifu na ardhi.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Arjan Tekin Baş