Trump na Putin: Kutoka kwa Upendo hadi Chuki Ni Hatua Moja Tu
Trump na Putin: Kutoka kwa Upendo hadi Chuki Ni Hatua Moja Tu

Habari:

0:00 0:00
Speed:
October 08, 2025

Trump na Putin: Kutoka kwa Upendo hadi Chuki Ni Hatua Moja Tu

Trump na Putin: Kutoka kwa Upendo hadi Chuki Ni Hatua Moja Tu

(Imetafsiriwa)

Habari:

Putin alimtishia Trump kukata uhusiano ikiwa Ukraine itapata makombora ya Tomahawk kutoka Marekani.

Maoni:

Katika wiki mbili zilizopita, tumeshuhudia mfululizo wa ripoti za habari zinazoashiria mabadiliko katika sera ya utawala wa sasa wa Marekani kuelekea Urusi na uvamizi wake wa Ukraine.

Mnamo Septemba 23, Trump alitangaza ghafla: "Nadhani Ukraine, kwa msaada wa Umoja wa Ulaya, ina uwezo wa kupigana na kushinda, na kurejesha ardhi yake yote kwa mipaka yake ya asili."

Siku hiyo hiyo, alisema pia: "Ukraine haiwezi tu kurejesha ardhi yake yote, lakini inaweza kusonga mbele." Aliongeza: "Urusi haionekani ya kuvutia. Kwao, ilitakiwa iwe ya haraka. Inaonekana vita bado havijaisha."

Mnamo Septemba 26, alisema: "Uchumi wa Urusi unaelekea kuzimu. Wanapiga kila kitu kinachoonekana, na hawachukui ardhi nyingi sana, ikiwa ipo. Kwa kweli, wanapoteza baadhi yake."

Mnamo Septemba 29, Mjumbe Maalum wa Marekani nchini Ukraine, Keith Kellogg, alitangaza kwamba Trump alikuwa ameiruhusu Ukraine kutekeleza mashambulizi ya masafa marefu dhidi ya Urusi. Mnamo Oktoba 2, iliripotiwa kuwa Trump alikuwa amesaini agizo linaloruhusu Pentagon na mashirika ya ujasusi kuisaidia Ukraine katika mashambulizi kama hayo.

Kwa mara ya kwanza, utawala wa Trump utasaidia Ukraine katika mashambulizi ya masafa marefu. Marekani imeomba washirika wa NATO kutoa msaada kama huo kwa Ukraine. Uwezekano wa kuipatia Ukraine makombora ya Tomahawk na Barracuda unafanyiwa majadiliano.

Kwa kuzingatia habari hizi, inaweza kudhaniwa kuwa Urusi ilikataa masharti ya Amerika ya kutatua mzozo wa Ukraine.

Kama inavyojulikana, miezi kadhaa kabla ya mkutano wa marais wa Amerika na Urusi huko Alaska, Urusi ilisisitiza kama sharti la msingi kwamba Ukraine itambue Crimea na maeneo yanayokaliwa mashariki mwa Ukraine kama ya Urusi. Inaonekana kwamba Urusi, baada ya kujifunza kutokana na uzoefu mchungu wa makubaliano ya Minsk, inatambua kikamilifu kwamba mzozo mwingine wowote uliogandishwa badala ya makubaliano kwa Amerika itakuwa kama kuumwa na nyoka yule yule tena. Mnamo mwaka wa 2015, Urusi - ikiwa imeamini ahadi za Amerika za kupuuzia uvamizi wake dhidi ya Ukraine - iliingilia kati mzozo wa Syria kwa niaba ya mteja wa Amerika, Bashar al-Assad. Hii ilisababisha kuongezwa kwa utawala wa Assad nchini Syria, kwani Merika haikuwa imepata mbadala mzuri kwake bado.

Mnamo 2022, wakati Urusi ilipogundua kuwa hakuna mtu anayekusudia kutambua udhibiti wake juu ya Crimea iliyounganishwa na Donbas iliyokaliwa, ilizindua uvamizi kamili wa Ukraine.

Kufikia mwishoni mwa 2024, utawala wa Assad ulikuwa umemaliza nguvu zake na ulibadilishwa na Ahmed al-Shar'a anayeungwa mkono na Uturuki. Urusi iligundua kuwa ilikuwa imetumiwa, kwa hivyo ilifukuzwa kutoka Syria.

Tangu wakati huo, Urusi inatambua kuwa usitishaji wowote wa mapigano au kuganda kwa mzozo nchini Ukraine kutakuwa sawa na kujiua. Ndiyo maana inasisitiza sana kutambuliwa kwa udhibiti wake juu ya Crimea na Donbas.

Kuhusu msimamo wa mazungumzo wa Amerika kuhusu Ukraine, unazidi mzozo wa sasa. Kimsingi, Marekani inatumia mzozo nchini Ukraine kulazimisha Urusi kushirikiana katika kukabiliana na China.

China leo imezungukwa kutoka pande tatu na washirika wa Marekani, muhimu zaidi kati yao wakiwa Japan, Korea Kusini, India na Pakistan, pamoja na nchi nyingine za kikanda.

Muungano unaowezekana kati ya Urusi na China utaiwezesha China kuvunja mzingiro huu kamili na kufikia rasilimali kubwa za asili za Urusi, ambayo itaongeza nguvu zake za kijeshi na kiuchumi kwa kiasi kikubwa.

Msimamo wa China bado ni wa tahadhari, haiko tayari kuunga mkono Urusi kikamilifu kwa gharama ya uhusiano wake mkubwa wa kibiashara na Marekani na Umoja wa Ulaya.

Ikumbukwe kwamba Marekani inataka kuacha mlango wazi kidogo, haitafuti suluhu kamili kwa mzozo wa Ukraine, kwa sababu Urusi iliyohusika katika uvamizi wake itakuwa rahisi zaidi. Suluhu kamili ya mzozo wa Ukraine, badala ya hatua ya pamoja dhidi ya China, itaiwezesha Urusi, wakati wowote, kujitenga na Magharibi na kuikumbatia China.

Kwa upande mwingine, majeraha mapya ya Urusi baada ya kufukuzwa kwake kwa fedheha kutoka Syria yanakumbusha kwamba kukubali makubaliano mengine kama ya Minsk ni sawa na kukanyaga jembe lile lile mara mbili.

Kwa hivyo, haikuwa jambo la kushangaza kwamba Trump, mara tu mazungumzo yalipoisha, alisema: "Sasa inategemea Rais Zelensky kukamilisha kazi."

Ikumbukwe kwamba huyu ndiye Trump yule yule aliyemkemea Rais Zelensky katika Ofisi ya Oval mnamo Februari 28, 2025, akidai kwamba hana hoja za kweli na anategemea kabisa usambazaji wa silaha za Amerika.

Kwa upande wake, Ukraine, kama ilivyotarajiwa, ilikataa masharti ya Urusi ya kutambua Crimea na Donbas kama za Urusi. Mnamo Septemba 15, 2025, Waziri wa Fedha wa Ukraine, Serhiy Marchenko, alikiri kushindwa kwa mazungumzo ya amani, akisema: "Lazima tuandae jeshi na watu kwa mwaka mwingine wa vita, na hiyo itahitaji pesa zaidi."

Mnamo Septemba 19, Rustem Umerov, Katibu wa Baraza la Usalama wa Kitaifa na Ulinzi la Ukraine na Mkuu wa Wajumbe wa Ukraine, alisema: "Ukraine kwa sasa haifanyi mazungumzo na Urusi kumaliza vita."

Siku chache baadaye, kuanzia Septemba 23, Rais Trump alibadilisha hotuba yake kuelekea Urusi na uvamizi wake wa Ukraine kwa kiasi kikubwa.

Kwa kumalizia, ikumbukwe kwamba mzozo wa Ukraine unathibitisha tena kwamba nchi, na uhuru wao, rasilimali, maisha na damu, bado zimechukuliwa mateka katika mzozo kati ya mataifa makubwa.

Hata mataifa makubwa yanayojitambulisha kama marafiki na watetezi wa mataifa yaliyodhulumiwa, kwa kweli ndio wachochezi wakuu wa migogoro na wanufaika wakuu kutoka kwayo. Na kila kinachozungumziwa kuhusu haki ya watu kuamua hatima yao, uhuru, haki za binadamu, na kuwajali wanawake, wazee na watoto, si chochote ila ni pazia la sera zao za kinyama. Hali hii itaendelea hadi kurudi kwa utawala wa kweli wa kimungu wa ulimwengu unaowakilishwa na Ukhalifa wa Pili ulioongozwa kwa njia ya Utume ambao lengo lake la kweli litakuwa ni manufaa ya wanadamu wote, sio tu kauli mbiu tupu.

﴿Basi watakutungishia vichwa vyao na watasema: Ni lini hiyo? Sema: Asaa iwe karibu

Imeandikwa kwa Radio ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut Tahrir

Fadl Amzaev

Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir huko Ukraine

More from null

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Habari:

Uchunguzi wa Al Jazeera, unaotegemea uchambuzi wa picha za satelaiti, umefichua mifumo ya uharibifu wa kimfumo iliyofanywa na uvamizi huko Gaza kati ya Oktoba 10 na 30 iliyopita.

Shirika la "Sanad" la uhakiki wa habari la mtandao wa Al Jazeera limegundua operesheni za ulipuaji, ubomoaji wa kihandisi na mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na uvamizi ndani ya Ukanda huo tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. (Al Jazeera Net)

Maoni:

Baada ya kutangazwa kwa usitishaji wa vita vilivyojaa mabomu dhidi ya Ukanda wa Gaza chini ya usimamizi wa Trump na kwa makubaliano na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilikuwa wazi kuwa ilifikiwa kwa faida ya taasisi ya Kiyahudi. Hili limebainika kulingana na uchambuzi wa picha za satelaiti na ripoti za hivi karibuni za habari, kwamba jeshi la Kiyahudi lililipua maelfu ya majengo huko Gaza, haswa huko Shuja'iyya na Khan Yunis katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, na vile vile Rafah, na maeneo yaliyo mashariki mwake ambayo yalishuhudia operesheni kubwa za uharibifu.

Uharibifu mkubwa huko Gaza sio wa bahati mbaya, lakini una malengo ya kimkakati ya muda mrefu, kama vile kuharibu mazingira yanayounga mkono upinzani. Kuondoa Gaza ya miundombinu yake, shule zake na makazi yake, inafanya kuwa ngumu kwa upinzani kujipanga upya au kujenga upya uwezo wake. Hii ni kizuizi cha muda mrefu kwa kuharibu uwezekano na kulazimisha ukweli mpya ambao unaifanya Gaza kuwa dhaifu na kuiacha ikiwa imepooza kiuchumi na haifai kwa makazi, ambayo huandaa njia ya kukubali suluhisho zozote za kisiasa au kiusalama, au hata kukubali wazo la uhamishaji, kwa sababu kuacha Gaza kama kifusi, inafanya kuwa ngumu kwa ujenzi kuwa mikononi mwa watu wake pekee. Badala yake, nchi na mashirika yataingilia kati kwa masharti ya kisiasa, na uvamizi unatambua kuwa yeyote anayejenga upya ndiye anayemiliki uamuzi. Hivyo basi uharibifu wa leo ni sawa na udhibiti wa kisiasa kesho!

Kwa kweli, kuelezea makubaliano ya kusitisha vita dhidi ya Gaza kama "yenye mabomu" haikuwa bure, kwa sababu ilikuwa ya sehemu, na malengo ya madai ya kijeshi hayakujumuishwa, ambayo inaruhusu Wayahudi kuendelea na uvamizi na uharibifu kwa kisingizio cha kiusalama. Vivyo hivyo, ilifikiwa na nchi kubwa zaidi inayounga mkono taasisi bila dhamana thabiti za kimataifa, ambayo inafanya kuwa dhaifu na inakabiliwa na ukiukwaji, haswa kwa kukosekana kwa uwajibikaji wa kimataifa, ambayo inafanya taasisi ya Kiyahudi kuwa juu ya uwajibikaji.

Tutaendelea kuwa taifa lenye unyenyekevu na linalokubali, tukitazama watu waliodhoofika, waliochoka, waliopotea na wenye njaa mpaka lini?! Na juu ya yote hayo, wanaruhusiwa wakati wowote?! Hebu sote tuwe Saladin al-Ayyubi, kwa sababu Gaza leo inakumbusha taifa kwamba Saladin hakuwa tu mtu shujaa, lakini alikuwa kiongozi katika dola iliyokuwa na mradi na jeshi na taifa moja nyuma yake. Kwa hivyo, wito wa kuwa Saladin haimaanishi ushujaa wa mtu binafsi, lakini kufanya kazi ya kuanzisha dola ambayo inafanya watoto wote wa taifa kuwa askari katika safu moja chini ya bendera moja.

Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto﴾.

Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Manal Um Ubaidah

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Habari:

Kituo cha Yemen Sana'a kilirusha hewani Jumatano jioni, 2025/11/12, kipindi cha kibinadamu "Nchi Yangu", na katika sehemu ya "Tuko nanyi", kipindi kilionyesha kesi ya mwanamke ambaye alikuwa ameambukizwa ugonjwa adimu na alihitaji kusafiri kwenda India kwa gharama ya dola elfu 80, ambapo kiasi cha dola elfu 70 kilikusanywa kutoka kwa mashirika na wahisani, lakini mtangazaji wa kipindi alizungumzia sana sifa za mchangiaji wa mwisho wa dola elfu kumi, na ikawa wazi kuwa alikuwa Abdul Malik al-Houthi, na alisifu jukumu lake la mara kwa mara katika kusaidia kesi za kibinadamu ambazo zinaonekana kwenye kipindi.

Maoni:

Hakika, mtawala katika Uislamu ana jukumu kubwa, ambalo ni kutunza maslahi ya watu kwa kutumia kile kinachowanufaisha na kutoa kila kitu kinachowafariji. Kimsingi yeye ni mtumishi wao, na hawezi kufurahia maisha hadi atakapohakikisha hali zao. Jukumu hili sio ihsani au upendeleo, bali ni wajibu wa kisheria ambao Uislamu umemlazimisha, na anahesabiwa kuwa amepungukiwa ikiwa atalipuuza. Uislamu umewajibisha umma kumuwajibisha anapopungukiwa. Amani na baraka zimshukie: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, ni upuuzi kufurahia usikivu wa watawala au serikali kwa mahitaji fulani na kuita hiyo kazi ya kibinadamu, wakati kimsingi ni kazi ya kichungaji ya lazima.

Moja ya dhana hatari zaidi ambayo imekita mizizi na ubepari na utawala wake duniani ni kukataa kwa serikali kutunza watu na kuacha utunzaji wa watu kwa mashirika na vyama vya hisani vinavyoendeshwa na watu binafsi au vikundi, na watu huenda kwao mara nyingi kuwasaidia na kutimiza mahitaji yao. Wazo la vyama lilionekana kwanza huko Uropa wakati wa Vita vya Ulimwengu, ambapo familia nyingi zilipoteza wazazi wao na zikawa zinahitaji mlinzi, na serikali, kulingana na mfumo wa kidemokrasia wa kibepari, haitunzi masuala, bali ni mlinzi wa uhuru tu. Matajiri waliogopa mapinduzi ya maskini dhidi yao, kwa hivyo walianzisha vyama hivi.

Uislamu umefanya kuwepo kwa sultani kuwa wajibu wa kutunza masuala ya umma ili kuhifadhi haki zao za kisheria na kukidhi mahitaji yao sita ya msingi ambayo lazima yakidhiwe kwa watu binafsi na vikundi; chakula, mavazi na makazi lazima yatolewe na serikali kwa kila mtu mmoja mmoja, Waislamu na wasio Waislamu, na usalama, matibabu na elimu hutolewa na serikali bure kwa wote. Mtu mmoja alikuja kwa Khalifa wa Waislamu, Omar bin al-Khattab, Mungu amuwiye radhi, akiwa na mke wake na binti zake sita, akasema: (Ewe Omar, hawa ni binti zangu sita na mama yao, walishe, wavishe na uwe ngao kwao kutoka kwa wakati) Omar akasema: (Na vipi ikiwa sitafanya hivyo?!) Bedui akasema: (Nitakwenda) Omar akasema: (Na vipi ikiwa utakwenda?) Akasema: (Utaulizwa kuhusu hali yao Siku ya Kiyama, ukisimama mbele ya Mungu ama kuelekea Motoni au Paradiso), Omar akasema: (Umma huu hautapotea maadamu kuna watu kama hawa).

Enyi Waislamu: Hii sio ndoto, bali ni Uislamu ambao umefanya utunzaji kuwa wajibu kwa Khalifa wa Waislamu kwa kila mtu mmoja mmoja, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehma na amani zimshukie, alisema: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, lazima turudishe hukumu hizi na kuzifanya ziwe za utekelezaji, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyomo kwa watu mpaka wabadili yaliyomo katika nafsi zao﴾. Hivyo, kitakachobadilisha hali yetu kuwa haki na ustawi ni Uislamu.

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Sadiq al-Sarari