Trump atishia kuishambulia Iran tena na kusimamisha kupunguza vikwazo dhidi yake
Habari:
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kusitishwa mara moja kwa hatua za kupunguza vikwazo dhidi ya Iran kujibu taarifa ya Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Khamenei, akidokeza kuishambulia tena.
Trump alisema katika mkutano na waandishi wa habari kwamba Khamenei anajua kuwa matamshi yake kuhusu ushindi katika vita ni uongo. Aliongeza kuwa atafikiria kuishambulia Iran tena ikiwa itarudi kuimarisha urani. Alisisitiza kuwa hana wasiwasi kuhusu uwepo wa maeneo ya siri ya nyuklia huko. Akieleza kuwa kile ambacho Wairani watafikiria leo ni mpango wa nyuklia. Aliitaka Iran kurudi kujumuika katika mfumo wa kimataifa "la sivyo mambo yatakuwa mabaya zaidi kwake." Aliongeza kuwa alimwokoa Kiongozi Mkuu wa Iran kutoka kile alichokiita kifo cha kutisha "na anapaswa kusema asante rais Trump."
Mapema leo, Khamenei alitoa hotuba yake ya kwanza tangu mwisho wa vita na akasema kuwa nchi yake imepata ushindi dhidi ya "taasisi bandia ya Kizayuni" na imetoa "pigo kali" kwa Marekani.
Kiongozi Mkuu wa Iran alisisitiza kuwa Marekani iliingia vitani "kwa sababu ilihisi kwamba taasisi ya Kizayuni ingeangamizwa kabisa" na akaona kuwa Marekani haikupata mafanikio yoyote kutoka kwa vita hivi.
Alisema kuwa rais wa Marekani "amezidisha ukubwa wa shambulio la Marekani" kwa sababu "alihitaji kufanya maonyesho."
Khamenei alisisitiza kuwa Marekani ilishambulia maeneo ya nyuklia "lakini haikufanikiwa sana" akionya kwamba "uchokozi wowote dhidi ya Iran utakabiliwa na kurudia kulenga kambi za Marekani." (Al Jazeera Net, 2025/06/27)
Maoni:
Masomo tunayoyapata kutoka katika Surat Al-Qasas katika Qur'ani Tukufu ni kwamba Firauni alikuwa mkuu katika ardhi na akafanya watu wake kuwa makundi, akidhoofisha kundi moja, akiwachinja watoto wao na akihifadhi wanawake wao, kisha Mwenyezi Mungu Alipotaka kuwafadhili wale waliodhoofishwa na kuwafanya viongozi na kuwafanya warithi, alimfunulia mama wa Musa kumtupa baharini na akakutwa na watu wa Firauni na akalelewa katika himaya yake ili iwe uharibifu wake mikononi mwa huyo mtoto mbarikiwa, na haya yote ni katika mipango ya Mwenyezi Mungu.
Kisha alipofikia ukomavu, Mwenyezi Mungu alimfunulia baada ya kumuua mtu miongoni mwao na akakimbilia Madyan na akawa anatafutwa, kwamba nenda kwa Firauni, hakika amevuka mipaka, lakini Firauni alikataa kufuata wito wa haki na alijivuna yeye na majeshi yake katika ardhi na walidhani kuwa hawatarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, na walitoa ahadi kwa wale walioamini kutoka kwa wachawi wa Firauni ya kukata mikono na miguu yao kinyume na kuwasulubisha kwenye mashina ya mitende, kisha Firauni na jeshi lake walimfuata Musa na wale waliokuwa pamoja naye miongoni mwa waumini, na hapa ilidhihirika miujiza ya Mungu, kwani waumini walikuwa katika hali ngumu; kwani bahari ilikuwa mbele yao na askari wa Firauni walikuwa nyuma yao, hivyo baadhi yao walisema, "Hakika tutakamatwa," Musa alijibu, "Hapana, hakika Mola wangu yuko pamoja nami, ataniongoza," Mwenyezi Mungu akamfunulia kwamba piga bahari kwa fimbo yako, ikapasuka, na kila sehemu ikawa kama mlima mkuu, na kana kwamba Mwenyezi Mungu Alitaka kumvuta Firauni na majeshi yake ili awatenganishe baharini na amwokoe Musa na wale waliokuwa pamoja naye miongoni mwa waumini.
Hadithi hii ina mazingatio na mawaidha kwetu sisi wabebaji wa Da'wah kwamba batili haijalishi inakuwa juu na inazidi, lazima iwe na mwisho, na kwamba mafirauni wa zama hizi, wakiwemo Firauni wa Marekani, ni dhaifu kuliko Firauni huyo, na kwamba kuangamia kwao kunakaribia, Mungu akipenda, na tunachopaswa kufanya ni kuchukua sababu kulingana na njia ya kisheria iliyobainishwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ, Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Sema: Hii ndiyo njia yangu, ninalingania kwa Mwenyezi Mungu kwa hoja iliyo wazi, mimi na wale wanaonifuata. Subhanallah, na mimi si miongoni mwa washirikina.﴾ Na ni lazima kwa Umma wa Kiislamu kutoka katika mkondo huu kutafuta mabadiliko ya kimsingi na wala usitegemee mashariki au magharibi kwa sababu wote ni maadui wa Uislamu na Waislamu, na kila mtu anatafuta maslahi yake, na sisi Waislamu Mwenyezi Mungu ametuneemesha kwa kanuni kuu ya Uislamu ambayo inatokana na mfumo unaoshughulikia matatizo yote ya maisha iwe ya kisiasa, kiuchumi, kijamii, kimahakama au yanayohusiana na mahusiano ya nje na nchi nyingine, na eneo la kimkakati linalounganisha mabara matatu; Asia, Afrika na Ulaya, na tuna utajiri mkubwa wa binadamu. Kwa hivyo tunawaomba Waislamu kama watu binafsi, vikundi, na watu wa nguvu na kinga kuweka mikono yao katika mikono ya Hizb ut-Tahrir; painia ambaye watu wake hawasemi uongo, na kufanya kazi nayo kuanzisha upya maisha ya Kiislamu kwa kuanzisha Dola ya Khilafa Rashida kwa misingi ya unabii na wasibadilishe neema ya Mwenyezi Mungu kwa ukafiri na kuwapeleka watu wao katika nyumba ya uharibifu, Jahannam, wataingia humo, na ni makao mabaya.
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya ofisi kuu ya habari ya Hizb ut-Tahrir
Abdullah Abdul Hamid - Jimbo la Iraq