Uundaji Mpya wa Kijeshi Yemen unaofadhiliwa na Saudi Arabia kushindana na Miundo inayohusiana na UAE
Habari:
Uundaji wa vikosi vipya vya kijeshi unaofadhiliwa na kuungwa mkono na Saudi Arabia katika jimbo la Shabwa kusini mashariki mwa Yemen. (Arabi 21, Julai 3, 2025).
Maoni:
Hapo awali Saudi Arabia iliunda muundo wa kijeshi kusini mwa Yemen iliyoiita ngao ya taifa, na ilipeleka vikosi hivyo huko Aden na viunga vyake (Tur al-Baha) na huko Hadramout kushindana na ukanda wa usalama ambao UAE ilianzisha huko Aden, na kushindana na vikosi vya wasomi wa Hadrami ambavyo UAE ilianzisha huko Hadramout, na leo inatangazwa kuhusu uundaji mpya wa kijeshi unaofadhiliwa na kuungwa mkono na Saudi Arabia kusini mwa Yemen katika jimbo la Shabwa haswa ili kuwafukuza vikosi vya wasomi wa Shabwa vinavyohusiana na UAE kutoka huko!
Badala ya Saudi Arabia kuandaa miundo ya kijeshi ya kuwaokoa watu wa Gaza kutoka kwa mashine ya mauti ambayo chombo cha Kiyahudi kinavuna watu wetu huko, au kuhamasisha jeshi lake kuwasaidia, inaajiri wana wa Yemen kupigana, wao kwa wao, ikichukua fursa ya umaskini mkubwa ulioenea nchini na ukosefu wa ajira ambao vijana wanapitia, na yote hayo si kwa ajili ya Yemen au hata kwa maslahi yake, bali ni kulinda maslahi ya Marekani nchini Yemen, na kuondoa ushawishi wa Uingereza ambao UAE inalazimisha kusini mwa Yemen, na hivyo wana wa kusini mwa Yemen wanajikuta katika vita kati yao wenyewe wakitumikia miradi ya Magharibi kwa pesa za Waislamu, na imekuwa wazi kuwa vikosi hivyo havitetei nchi wala dini wala hata jambo tukufu, bali ni askari watumwa wa dirham ya Imarati na rial ya Saudi wakiwa wameghafilika na adui yao halisi na masuala yao ya msingi, amesema ﷺ: «Ameangamia mtumwa wa dinari, ameangamia mtumwa wa dirhamu, ameangamia mtumwa wa al-Qatifa».
Vikosi hivi vya kijeshi vinaandaliwa chini ya macho ya mamlaka nchini ambazo hazichukui hatua na wala hazipingi uovu bali zinashiriki katika kula njama dhidi ya watu kwa kuungana na maadui zao, na imekuwa wazi leo kuwa utawala wa Saudi Arabia unatumikia maslahi ya Trump Amerika waziwazi, bali utawala huo unaunda kisu ambacho Amerika inatumia kuwachoma umma na kuligawanya taifa na kusonga mbele kuelekea mradi wa Amerika ambao ni kuifanya Israeli salama na yenye amani katikati ya umma wa Kiislamu, na vivyo hivyo Imarati ilifanya hapo awali.
Enyi watu wetu nchini Yemen: Mnapaswa kukataa miundo hii ya kijeshi ambayo itahalalisha damu ya watoto wenu kwani imeundwa kutekeleza shindano la Saudi Arabia na Imarati kusini mwa Yemen, na haina uhusiano wowote na vita vya Wahouthi au utetezi wa Yemen iliyogawanyika tayari.
Enyi vijana Waislamu: Umaskini sio hoja mbele ya Mungu ya kumuasi, kwani kupigana chini ya miradi ya upofu wa kijahiliya ni dhambi miongoni mwa dhambi kubwa, vipi ikiwa mapigano hayo ni utekelezaji wa ushindani wa kimataifa juu ya ushawishi na utajiri nchini?!
Suala la Muislamu katika maisha ni kutekeleza sheria ya Mungu na kulinda dola ya Kiislamu na kuilinda na kubeba Uislamu kwa da'wa na jihad kwa ulimwengu, kwani amani na baraka zimshukie alionya dhidi ya kujiunga na aina yoyote ya mapigano haramu: «Yeyote anayepigana ili neno la Mungu liwe la juu zaidi, basi yuko katika njia ya Mungu» Ama yale yote isipokuwa hayo yamo katika njia ya taghut, amesema Mtukufu: ﴿Na anayemkataa taghut na kumuamini Mwenyezi Mungu, basi ameshika kishikio madhubuti kisichokatika﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Abdul Aziz Al-Hamid - Jimbo la Yemen