Je! Maji yanaweza kutarajiwa kutoka kwa Sarabi?!
Habari:
Umoja wa Mataifa unaamua kuendeleza mkutano wa suluhisho la mataifa mawili na Amerika inapinga. (Alarabiya.net)
Maoni:
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepitisha uamuzi wa maneno uliopendekezwa na Saudi Arabia kuhusu kuendelezwa kwa mkutano kuhusu suluhu ya amani ya suala la Palestina na utekelezaji wa suluhisho la mataifa mawili, na kwa kuzingatia habari hii, inabainika kuwa Saudi Arabia na wengine katika nchi za Waislamu wana wasiwasi juu yao wenyewe kutoka kwa watu wao kutokana na kile kinachotokea Gaza na Ukingo wa Magharibi, na wanajaribu kwa bidii kupendekeza matamko kama haya kwa watu wao kwamba wanafanya vitendo na juhudi za kidiplomasia kulingana na sheria za kimataifa ili kusimamisha ukiukwaji wa Wayahudi, labda watapunguza hasira zao na kupunguza kasi ya harakati zao za kung'oa tawala hizi kutoka mizizi yao, na kukata mkono wa Magharibi makafiri kutoka nchi zao, wakidhani kwamba bado wanaamini na maneno yao.
Hebu mfumo wa Al Saud na tawala zingine za unyonge, unyenyekevu na utegemezi zijue kwamba watu wao wamewapita zamani, na wamekata kamba zao nao baada ya kudhibitisha usaliti wao na njama zao na maadui wa Mungu dhidi ya Uislamu na watu wake, na wameona kwa macho yao jinsi tawala hizi zilivyosimama upande wa Wayahudi na kuziunga mkono kwa kila kitu wanachohitaji, hata kuwatetea na kushiriki katika kuua, kuwafukuza na kuwanyima chakula watu wetu huko Gaza, na hakuna mtu aliyebaki katika safu zao isipokuwa kila mjinga au mfaidika.
Na tawala hizi zijue kwamba umma unatazamia na unatembea kwa hatua thabiti na Mungu kuelekea kurejesha historia yake ya kwanza ambayo ilikuwa mkuu wa ulimwengu bila mshindani, kueneza Uislamu na haki popote ilipo, na hii inarudi hivi karibuni, kwa idhini ya Mungu, chini ya Ukhalifa kwa misingi ya unabii; ahadi ya Mungu Mwenyezi na habari njema ya Nabii wake ﷺ, na kwa uwepo wa Hizb ut-Tahrir ambao unafanya kazi kwa hilo, ukiunganisha usiku wake na mchana wake bila kuchoka au kuchoshwa, ukizingatia njia ya Mtume wa Mungu ﷺ katika kuanzisha dola ya kwanza ya Kiislamu, na umeandaa vifaa, na watu waaminifu, wacha Mungu na mifumo na sheria zote zilizotokana na Kitabu cha Mungu na Sunnah za Mtume wake na kile walichoongoza kwake, ukitembea kwa njia yake bila kuacha au kupotoka, na yuko, kwa idhini ya Mungu, kwenye hatihati ya kufika, ﴿Na wanasema: Ni lini hicho? Sema: Huenda ikawa karibu﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Dk. Abdul Ilah Muhammad - Jimbo la Jordan