Ee Fidan! Ikiwa mko tayari kwa kila dhabihu, basi songeni mbele na jeshi lenu kuelekea Palestina!
Ee Fidan! Ikiwa mko tayari kwa kila dhabihu, basi songeni mbele na jeshi lenu kuelekea Palestina!

Habari:

0:00 0:00
Speed:
November 05, 2025

Ee Fidan! Ikiwa mko tayari kwa kila dhabihu, basi songeni mbele na jeshi lenu kuelekea Palestina!

Ee Fidan! Ikiwa mko tayari kwa kila dhabihu, basi songeni mbele na jeshi lenu kuelekea Palestina!

Habari:

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Hakan Fidan, alitoa taarifa baada ya mkutano wa mawaziri kuhusu Gaza uliofanyika Istanbul kwa ushiriki wa mawaziri kutoka Indonesia, Pakistan, Qatar, Saudi Arabia, UAE na Jordan, akisema: "Tuko tayari kutoa kila aina ya dhabihu kwa ajili ya amani." Aliongeza: "Israel inakiuka usitishaji mapigano. Tangu kuanza kwa usitishaji mapigano, karibu Wapalestina 250 wameuawa." (Hurriyat, 2025/11/03)

Maoni:

Hisia za umma zimefifia kuhusu matamko matupu yanayotolewa na watawala vibaraka na watumishi, ambao hawafanyi chochote kwa Wapalestina wala kwa Waislamu, na hawasogezeki hata kidole kimoja kusimamisha mauaji na ukatili dhidi yao! Umma umezowea mikutano yao ambayo ni kama sherehe za chai na kahawa kisha wanaondoka! Umma hautarajii chochote kutoka kwao isipokuwa taarifa hizi tupu! Bali taarifa hii isiyo na maana ya Fidan, aliyoitoa baada ya mkutano wa uhaini, inaonyesha wazi ukubwa wa utata! Anadai kuwa yuko tayari kwa kila dhabihu, na wakati huo huo anakiri kwamba Wayahudi wameua takriban Wapalestina 250 tangu usitishaji mapigano! Hii ni dhabihu gani? Na iko wapi? Ikiwa mko tayari kweli kwa kila dhabihu, kwa nini hamhamishi majeshi yenu dhidi ya chombo cha Kiyahudi kujibu mauaji ya Wapalestina 250 tangu usitishaji mapigano? Hii ni pamoja na wale 67,000 waliouawa hapo awali.

Dhabihu haimaanishi kutoa matamko machache kuhusu Palestina, bali inamaanisha kuvumilia matatizo ambayo yanaweza kusababishwa na kusonga mbele kwa majeshi. Dhabihu si kuhesabu ukiukwaji na idadi ya wahanga, bali ni kubeba matokeo ya mzingiro wa kimataifa kutokana na kutuma majeshi kujibu mauaji ya Waislamu. Dhabihu ya kweli ni kutokaa kimya juu ya dhuluma, bali kuiga matendo ya Mtume ﷺ na Al-Mu'tasim. Dhabihu haimaanishi kutuma vikosi vya kulinda amani kuwalinda Wayahudi na kuimarisha chombo chao, hii si dhabihu, bali ni uhaini wa wazi.

Kwa hivyo, dhabihu ya kweli kwa ajili ya Palestina ni kwa vitendo vinavyoumiza chombo cha Kiyahudi na kuondoa uovu wake. Ama vinginevyo, ni upuuzi mtupu na hauitwi dhabihu. Kwa hivyo ikiwa kweli mnataka kutoa dhabihu kwa ajili ya umma na kwa ajili ya damu ya mashahidi wa Palestina, basi songeni mbele na majeshi yenu mara moja!

Na kwa upande mwingine, mkutano wenu huko Istanbul na maafisa vibaraka wachache kutoka nchi za Kiislamu kupitisha mpango wa usaliti wa Trump, hauthibitishi kamwe kwamba mko tayari kwa kila dhabihu. Katika mikutano isiyo na hesabu kabla ya hii, mmerudia kusema kwamba mko tayari kutoa kila kitu kwa ajili ya Wapalestina lakini hatujaona dhabihu yoyote kutoka kwenu, wala hatua yoyote ya kivitendo, isipokuwa matamko machache mnayoyatoa baada ya mkutano. Mmesahau kwa kujua na kwa makusudi mauaji ya Waislamu 67,000 huko Gaza, na kujeruhiwa kwa mamia ya maelfu. Kwa hivyo, mkutano wenu huko Istanbul haukuwa na lengo la kujadili nini kinaweza kufanywa kwa Palestina, bali kinyume chake; lengo lilikuwa kujadili jinsi ya kulinda chombo cha Kiyahudi na jinsi ya kukiunganisha katika eneo hilo kulingana na mpango mkatili wa Trump. Je, hii si ndiyo lengo la "kikosi cha amani" mnachotaka kutuma?

Inaonekana kwamba dhabihu zenu hazitolewi isipokuwa kwa ajili ya kutekeleza mpango wa usaliti wa Amerika na Trump. Lau mngewapa umma sehemu ya kumi ya kile mlichotoa au mtakachotoa kwa Amerika kama dhabihu, umma ungewakumbatia lakini kwa bahati mbaya, matukio ya Gaza yamethibitisha kwamba ninyi mko upande mmoja, na umma uko upande mwingine kabisa. Na historia ni shahidi mzuri kwamba hakuna na haitakuwepo rejea yoyote itakayotoa dhabihu ya kweli kwa ajili ya umma isipokuwa Ukhalifa. Na bila ya Ukhalifa, Waislamu wataendelea kukabiliana na maumivu makali na majanga katika kila sehemu ya dunia, kwa sababu ya watawala hawa wasaliti wanaotawala vichwa vyao. Leo Gaza, Sudan na Yemen, na Mungu anajua janga litakuwa wapi kesho!

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Arjan Tekin Baş

More from null

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Habari:

Uchunguzi wa Al Jazeera, unaotegemea uchambuzi wa picha za satelaiti, umefichua mifumo ya uharibifu wa kimfumo iliyofanywa na uvamizi huko Gaza kati ya Oktoba 10 na 30 iliyopita.

Shirika la "Sanad" la uhakiki wa habari la mtandao wa Al Jazeera limegundua operesheni za ulipuaji, ubomoaji wa kihandisi na mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na uvamizi ndani ya Ukanda huo tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. (Al Jazeera Net)

Maoni:

Baada ya kutangazwa kwa usitishaji wa vita vilivyojaa mabomu dhidi ya Ukanda wa Gaza chini ya usimamizi wa Trump na kwa makubaliano na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilikuwa wazi kuwa ilifikiwa kwa faida ya taasisi ya Kiyahudi. Hili limebainika kulingana na uchambuzi wa picha za satelaiti na ripoti za hivi karibuni za habari, kwamba jeshi la Kiyahudi lililipua maelfu ya majengo huko Gaza, haswa huko Shuja'iyya na Khan Yunis katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, na vile vile Rafah, na maeneo yaliyo mashariki mwake ambayo yalishuhudia operesheni kubwa za uharibifu.

Uharibifu mkubwa huko Gaza sio wa bahati mbaya, lakini una malengo ya kimkakati ya muda mrefu, kama vile kuharibu mazingira yanayounga mkono upinzani. Kuondoa Gaza ya miundombinu yake, shule zake na makazi yake, inafanya kuwa ngumu kwa upinzani kujipanga upya au kujenga upya uwezo wake. Hii ni kizuizi cha muda mrefu kwa kuharibu uwezekano na kulazimisha ukweli mpya ambao unaifanya Gaza kuwa dhaifu na kuiacha ikiwa imepooza kiuchumi na haifai kwa makazi, ambayo huandaa njia ya kukubali suluhisho zozote za kisiasa au kiusalama, au hata kukubali wazo la uhamishaji, kwa sababu kuacha Gaza kama kifusi, inafanya kuwa ngumu kwa ujenzi kuwa mikononi mwa watu wake pekee. Badala yake, nchi na mashirika yataingilia kati kwa masharti ya kisiasa, na uvamizi unatambua kuwa yeyote anayejenga upya ndiye anayemiliki uamuzi. Hivyo basi uharibifu wa leo ni sawa na udhibiti wa kisiasa kesho!

Kwa kweli, kuelezea makubaliano ya kusitisha vita dhidi ya Gaza kama "yenye mabomu" haikuwa bure, kwa sababu ilikuwa ya sehemu, na malengo ya madai ya kijeshi hayakujumuishwa, ambayo inaruhusu Wayahudi kuendelea na uvamizi na uharibifu kwa kisingizio cha kiusalama. Vivyo hivyo, ilifikiwa na nchi kubwa zaidi inayounga mkono taasisi bila dhamana thabiti za kimataifa, ambayo inafanya kuwa dhaifu na inakabiliwa na ukiukwaji, haswa kwa kukosekana kwa uwajibikaji wa kimataifa, ambayo inafanya taasisi ya Kiyahudi kuwa juu ya uwajibikaji.

Tutaendelea kuwa taifa lenye unyenyekevu na linalokubali, tukitazama watu waliodhoofika, waliochoka, waliopotea na wenye njaa mpaka lini?! Na juu ya yote hayo, wanaruhusiwa wakati wowote?! Hebu sote tuwe Saladin al-Ayyubi, kwa sababu Gaza leo inakumbusha taifa kwamba Saladin hakuwa tu mtu shujaa, lakini alikuwa kiongozi katika dola iliyokuwa na mradi na jeshi na taifa moja nyuma yake. Kwa hivyo, wito wa kuwa Saladin haimaanishi ushujaa wa mtu binafsi, lakini kufanya kazi ya kuanzisha dola ambayo inafanya watoto wote wa taifa kuwa askari katika safu moja chini ya bendera moja.

Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto﴾.

Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Manal Um Ubaidah

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Habari:

Kituo cha Yemen Sana'a kilirusha hewani Jumatano jioni, 2025/11/12, kipindi cha kibinadamu "Nchi Yangu", na katika sehemu ya "Tuko nanyi", kipindi kilionyesha kesi ya mwanamke ambaye alikuwa ameambukizwa ugonjwa adimu na alihitaji kusafiri kwenda India kwa gharama ya dola elfu 80, ambapo kiasi cha dola elfu 70 kilikusanywa kutoka kwa mashirika na wahisani, lakini mtangazaji wa kipindi alizungumzia sana sifa za mchangiaji wa mwisho wa dola elfu kumi, na ikawa wazi kuwa alikuwa Abdul Malik al-Houthi, na alisifu jukumu lake la mara kwa mara katika kusaidia kesi za kibinadamu ambazo zinaonekana kwenye kipindi.

Maoni:

Hakika, mtawala katika Uislamu ana jukumu kubwa, ambalo ni kutunza maslahi ya watu kwa kutumia kile kinachowanufaisha na kutoa kila kitu kinachowafariji. Kimsingi yeye ni mtumishi wao, na hawezi kufurahia maisha hadi atakapohakikisha hali zao. Jukumu hili sio ihsani au upendeleo, bali ni wajibu wa kisheria ambao Uislamu umemlazimisha, na anahesabiwa kuwa amepungukiwa ikiwa atalipuuza. Uislamu umewajibisha umma kumuwajibisha anapopungukiwa. Amani na baraka zimshukie: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, ni upuuzi kufurahia usikivu wa watawala au serikali kwa mahitaji fulani na kuita hiyo kazi ya kibinadamu, wakati kimsingi ni kazi ya kichungaji ya lazima.

Moja ya dhana hatari zaidi ambayo imekita mizizi na ubepari na utawala wake duniani ni kukataa kwa serikali kutunza watu na kuacha utunzaji wa watu kwa mashirika na vyama vya hisani vinavyoendeshwa na watu binafsi au vikundi, na watu huenda kwao mara nyingi kuwasaidia na kutimiza mahitaji yao. Wazo la vyama lilionekana kwanza huko Uropa wakati wa Vita vya Ulimwengu, ambapo familia nyingi zilipoteza wazazi wao na zikawa zinahitaji mlinzi, na serikali, kulingana na mfumo wa kidemokrasia wa kibepari, haitunzi masuala, bali ni mlinzi wa uhuru tu. Matajiri waliogopa mapinduzi ya maskini dhidi yao, kwa hivyo walianzisha vyama hivi.

Uislamu umefanya kuwepo kwa sultani kuwa wajibu wa kutunza masuala ya umma ili kuhifadhi haki zao za kisheria na kukidhi mahitaji yao sita ya msingi ambayo lazima yakidhiwe kwa watu binafsi na vikundi; chakula, mavazi na makazi lazima yatolewe na serikali kwa kila mtu mmoja mmoja, Waislamu na wasio Waislamu, na usalama, matibabu na elimu hutolewa na serikali bure kwa wote. Mtu mmoja alikuja kwa Khalifa wa Waislamu, Omar bin al-Khattab, Mungu amuwiye radhi, akiwa na mke wake na binti zake sita, akasema: (Ewe Omar, hawa ni binti zangu sita na mama yao, walishe, wavishe na uwe ngao kwao kutoka kwa wakati) Omar akasema: (Na vipi ikiwa sitafanya hivyo?!) Bedui akasema: (Nitakwenda) Omar akasema: (Na vipi ikiwa utakwenda?) Akasema: (Utaulizwa kuhusu hali yao Siku ya Kiyama, ukisimama mbele ya Mungu ama kuelekea Motoni au Paradiso), Omar akasema: (Umma huu hautapotea maadamu kuna watu kama hawa).

Enyi Waislamu: Hii sio ndoto, bali ni Uislamu ambao umefanya utunzaji kuwa wajibu kwa Khalifa wa Waislamu kwa kila mtu mmoja mmoja, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehma na amani zimshukie, alisema: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, lazima turudishe hukumu hizi na kuzifanya ziwe za utekelezaji, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyomo kwa watu mpaka wabadili yaliyomo katika nafsi zao﴾. Hivyo, kitakachobadilisha hali yetu kuwa haki na ustawi ni Uislamu.

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Sadiq al-Sarari