Wanawake Lazima Watambue Udanganyifu wa Utofauti na Ujumuishaji katika Siasa za Uliberali
(Imetafsiriwa)
Habari:
Kituo cha televisheni cha Al-Islam kimejadili ripoti mpya inayofichua mifumo ya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na ubaguzi wa kitaaluma unaowaathiri wanawake Waislamu katika vyombo vya habari. Athari hii imeenea hadi masuala ya afya ya akili na imani kwa taasisi. Ripoti ilijadili jinsi mtazamo wa waandishi wa habari wanawake Waislamu unaathiriwa hasa na ukiukwaji mdogo, dhana potofu na tofauti za mishahara.
Kituo cha Ufuatiliaji wa Vyombo vya Habari, ambacho kilichapisha ripoti hiyo awali, kinafichua kuenea kwa chuki dhidi ya Uislamu, tamaduni zenye sumu katika vyumba vya habari, na athari za afya ya akili, hasa baada ya vyombo vya habari kuripoti vita vya Wayahudi dhidi ya Gaza.
Utoaji habari wa mauaji ya kimbari ulikuwa hatua muhimu kwa wataalamu wengi wanafikiria kuhusu mustakabali wao wa kitaaluma katika sekta hii, na moja ya nukuu inatoa mtazamo wa tatizo hapa.
Wanawake Waislamu wanaofanya kazi katika vyombo vya habari vya Uingereza hawapo wala si wanyonge. Wao ndio kiini cha mazungumzo ya vyombo vya habari, hata wakati taasisi zinajaribu kuwatenga, kuwabagua au kutumia uwepo wao. Matokeo yanaonyesha kwamba ingawa umri mkubwa hutoa ushawishi fulani, vikwazo vya kitaasisi mara nyingi huwalazimisha wanawake Waislamu kuzingatia ajenda kuu za uhariri, ambazo mara nyingi zinapingana na Uislamu.
Maoni:
Inaeleweka sana na taasisi za vyombo vya habari vya kimataifa kwamba miundo ya Magharibi ya uhuru au kujieleza na utofauti hutoa mahali salama kwa wanawake kutoka makundi yote ya idadi ya watu.
Tumeona jinsi watu mashuhuri wa vyombo vya habari wanakimbia mifumo yao kandamizi na kujiimarisha katika taasisi za kidemokrasia, wakidai kwamba mazingira yao ya Kiislamu yanahitaji kuwa huru zaidi.
Ripoti hii inatoa ushahidi wa wazi kwamba imani katika uhuru wa kujieleza na uwakilishi haina msingi wowote, na lazima ikatazwe. Tunaweza kuona jinsi hatua zile zile za ukandamizaji ambazo wanawake walikimbia zipo kwa wingi katika nchi ambazo zinajivunia marejeleo ya vyombo vya habari vya uliberali.
Ukweli ni kwamba hakuna nchi yoyote ya Kiislamu inayowakilisha jinsi ujuzi wa kiakili wa mwanamke Mwislamu unalindwa, kwa sababu zote zimefungwa kwa ajenda ya vyombo vya habari vya kimataifa ambayo inapingana na ukweli wa Uislamu.
Wanawaadhibu vikali wapinzani na jaribio lolote la kufichua simulizi inayotawala inayokuzwa na vibaraka kwamba sheria ya Kiislamu inanunyamazisha ujuzi wa mwanamke na kumdharau. Hii ni kujenga udanganyifu kwamba miundo ya uliberali ya kidemokrasia ya Magharibi ndiyo chaguo pekee la maendeleo.
Elimu ya mwanamke na mchango wake mkubwa katika mazingira ya vyombo vya habari vya dola ya Kiislamu vimeandikwa kihistoria, ukweli ambao Magharibi inajaribu kuficha katika matoleo yao yaliyopotoshwa na kuhaririwa ya zamani. Hapa kuna mifano michache:
• Fatima al-Fihri: Alijulikana kwa kuanzisha Chuo Kikuu cha Al-Qarawiyyin huko Fez, Morocco, ambacho UNESCO inakitambua kama taasisi ya zamani zaidi ya elimu iliyopo na inayoendelea duniani. Chuo kikuu hiki kilitoa aina mbalimbali za fani, ikiwa ni pamoja na zile zinazohusiana na mawasiliano na uhamishaji wa maarifa.
• Zainab bint al-Kamal: Msomi huyu alijulikana kwa utaalam wake katika Hadith, na kufundisha katika taasisi maarufu. Alikuwa marejeo ya kuheshimiwa, na wanafunzi walisafiri kutoka mbali kusikiliza mihadhara yake. Kazi yake inaangazia umuhimu wa wasomi wanawake katika kuhifadhi na kuhamisha maarifa ya kidini.
• Ummu Darda as-Sughra: Mtu mwingine mashuhuri, alikuwa mwanasheria na mwanazuoni wa Hadith na mcha Mungu. Alijulikana kwa elimu na hekima yake, na aliwafundisha wanaume na wanawake sawa. Ushawishi wake unaonyesha jukumu muhimu lililochezwa na wanawake katika sayansi ya kidini katika kipindi hicho.
• Wanawake wengine mashuhuri: Wanawake wengine wengi walichangia katika mandhari ya kiakili wakati huo. Kwa mfano, Aisha bint Talha, Umm Salama, na Hafsa bint Sirin walikuwa wanawake mashuhuri katika nyanja mbalimbali. Wanawake hawa, pamoja na wengine, waliunda kitambaa cha kiakili na kitamaduni cha jamii za Kiislamu.
Qur'ani Tukufu ilikiri haki ya mwanamke kupata elimu, na iliwaalika wanaume na wanawake katika Uislamu kujifunza na kutafuta elimu, na mke wa Nabii ﷺ, Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, alikuwa miongoni mwa wenye uzalishaji zaidi, na ana wasimulizi wa hadithi. ﴿Mwenyezi Mungu huwainua walio amini miongoni mwenu, na waliopewa ilimu daraja. Na Mwenyezi Mungu anajua kabisa mnayo yatenda﴾.
Lazima turudi kwenye mfumo wa Khilafah, na kuwakilisha na kulinda ujuzi wa kiakili wa mwanamke Mwislamu ili tusitegemee kamwe hatua hizi za uwongo ili kupata haki zetu katika vyombo vya habari au maisha ya kijamii.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Umrana Mohammed
Mwanachama wa Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir