Jueni Enyi Waislamu!
Kipindi cha Kumi na Nane
Kwamba Utawala katika enzi za mwanzo ulikuwa sehemu mbili: Utawala wa Sala na Utawala wa Kodi, na kwa hivyo tunapata vitabu vya historia vikitumia misemo miwili katika mazungumzo yao kuhusu Utawala wa Wakuu, kwanza: Uongozi juu ya Sala, na pili: Uongozi juu ya Sala na Kodi, yaani: kwamba Amiri aidha awe Amiri wa Sala na Kodi, au Amiri wa Sala pekee, au Amiri wa Kodi pekee, na maana ya neno Sala katika Utawala au Uongozi siyo kuongoza watu katika sala zao tu, bali maana yake ni Utawala juu yao katika mambo yote isipokuwa mali, basi neno Sala lilimaanisha hukumu isipokuwa ukusanyaji wa mali, basi akikusanya mtawala Sala na Kodi utawala wake unakuwa wa jumla, na wakizuia utawala wake kwa Sala au kwa Kodi utawala wake unakuwa maalum.
