http://www.hizb-ut-tahrir.info/info/index.php/contents/entry_7489
حزب التحرير ولاية باكستان يوجه خطابا مفتوحا لأهل القوة في التاسع من أيار- تسجيل
More from null
Mayahudi Wanachimba Makaburi Yao Kwa Mikono Yao Wenyewe Na Watawala Waislamu Wanazuia Umma Kuwazika
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Mayahudi Wanachimba Makaburi Yao Kwa Mikono Yao Wenyewe
Na Watawala Waislamu Wanazuia Umma Kuwazika
Wakati mabomu ya chombo cha Kiyahudi na mizinga yake yakimiminika juu ya vichwa vya watu wetu huko Gaza, ambapo wanapiga majengo ya makazi, vyuo vikuu, na misikiti, na hata kusawazisha mahema na ardhi, na mifupa ya watoto na nyama yao inachanganyika na vifusi, mkutano wa aibu na fedheha ulikutana na kumalizika, mkutano wa wanyonge kutoka Waarabu na wasio Waarabu. Mkutano huo, ambao uliitwa Mkutano wa Dharura wa Kiarabu na Kiislamu na ulifanyika Doha, haukutoa zaidi ya kile kilichotarajiwa kutoka kwa wanyonge hao; kukemea na kulaani tu. Na hata kulaani huku hakukuwa kwa mashahidi waliokufa huko Doha na Gaza, bali kwa shambulio linalodaiwa dhidi ya "uhuru wa ufalme wa Doha". Baada ya idadi ya mashahidi huko Gaza kuzidi makumi ya maelfu, hawakupata hata "chembe" ya kukemewa na kulaaniwa kwao. Kinyume chake, wanyonge hao walitoa taarifa ya kukemea "uchokozi wa usaliti na uovu wa Israel dhidi ya uhuru wa Doha", huku wakipitisha taarifa ya mwisho ambayo haitoki nje ya sera ya woga ambayo wamepitisha tangu walipoteuliwa juu ya shingo za umma bora uliotolewa kwa watu katika nchi za Kiislamu.
Haijapita akilini kwa vibaraka wa Amerika miongoni mwa washiriki katika jambo hili la upuuzi kukutana pembeni mwa mkutano huo ili kusisitiza kile kinachowashughulisha, ambacho ni kupambana na Uislamu na Waislamu. Abdel Fattah al-Sisi alikutana na Shehbaz Sharif, pembeni mwa ushiriki wake katika shughuli za mkutano huo. Balozi Mohamed El-Shennawy, msemaji rasmi wa urais wa Misri, alisema kuwa Sisi alianza mkutano huo kwa kutoa rambirambi za dhati kwa serikali na watu wa Pakistani kwa wahasiriwa wa mafuriko ya hivi karibuni, na kwa wahasiriwa wa shambulio la kigaidi lililotokea mnamo Septemba 13, akisisitiza msimamo thabiti wa serikali ya Misri katika kulaani aina zote za ugaidi na itikadi kali, na kukataa kwake kabisa matukio haya yanayotishia usalama na utulivu. Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Pakistani alithamini jukumu zuri la Misri katika kutuliza hali ya mambo ya kikanda, akisifu juhudi za Cairo katika upatanishi wa kusitisha mapigano huko Gaza na juhudi zake za kupunguza mateso ya raia, pamoja na jukumu lake katika kuwezesha kufikiwa kwa makubaliano ya kuanza tena ushirikiano kati ya Iran na Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki.
Wakati damu inachemka katika mishipa ya umma kwa kile kinachotokea katika ardhi iliyobarikiwa ya Palestina, na mioyo yao inateketea kwa ajili ya ndugu zao dhaifu huko Gaza na Palestina kwa ujumla, na wakati umma unajiandaa kupigana na Wayahudi, na wakati wale waliokasirikiwa wanamkasirisha umma wa mabilioni mawili, kana kwamba hali yao inasema: "Kwa nini hamji kutuzika katika makaburi tuliyochimba kwa mikono yetu wenyewe?", katika nyakati hizi wanyonge hawa wanakutana wakati wanatawala umma ambao ungetaka kung'oa milima, ingeng'oa, vipi basi kuponda chombo cha uvamizi ambacho hakiwezi kusimama mbele ya nchi ndogo kabisa kutoka kwa nchi hizo zilizokusanyika?!
Ufafanuzi wa kitendawili hiki umekuwa ukijulikana kwa watu wote: hawa si watawala wa kweli wa umma, bali ni vibaraka wa nguvu za kikoloni za Magharibi na wafuasi wa uvamizi, na wengi wao ni Wayahudi, na kazi yao pekee ni kulinda maslahi ya Magharibi katika nchi za Waislamu, na kulinda chombo cha kansa na kambi ya kijeshi ya Magharibi iliyoendelea katikati ya nchi za Kiislamu. Pia wanafanya kazi ya kuzuia umoja wa umma wa Kiislamu na kuanzishwa kwa dola ya Kiislamu, Ukhalifa ulioongoka kwa njia ya unabii.
Kazi ya kuwafagilia na kufagilia ushawishi wa Magharibi kutoka nchi za Waislamu imekuwa ya haraka zaidi na ya lazima kuliko hapo awali, hasa kwa watu wa nguvu na ulinzi katika nchi za Waislamu, yaani majeshi na hasa jeshi la Pakistani la Mujahid Muislamu. Na imekuwa lazima kwa maafisa waaminifu ndani yake kutoa nusra kwa Hizb ut-Tahrir, kwa maana hii ndiyo kazi pekee ambayo inawaondolea lawama na kuhifadhi heshima yao ambayo imechafuliwa na viongozi wao wanyonge hawa. Ikiwa hawatofanya hivyo, watazama katika aibu na fedheha duniani kabla ya Akhera. Basi watainusuru lini Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa kuipa Hizb ut-Tahrir nusra ili isimamishe Ukhalifa ambao utahukumu kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, na kuandaa majeshi ya kukomboa ardhi iliyobarikiwa ya Palestina, na kulipiza kisasi kwa akina mama waliopoteza watoto wao, watoto na wazee, na kuzika uvamizi katika makaburi iliyochimba kwa mikono yake?
Hakika hii ni heshima ambayo haistahiliwi isipokuwa na yule anayestahili, basi nani anayestahili heshima ya kunusuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake ﷺ miongoni mwa watu wa nusra ili aokoke adhabu ya Akhera na kupata neema ya Pepo?!
﴿Enyi mlio amini! Piganeni na wale walio karibu yenu miongoni mwa makafiri, na wajue kwenu ukali, na jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu yu pamoja na wachamngu﴾
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Wilaya ya Pakistan
Iwe ni Kuhusu Mafuriko au Kashmir, au Uchumi au Ukaliaji wa India wa Mito Yetu, Tutaendelea Kungoja Hadi Lini Kinachoitwa Mfumo wa Kimataifa Utatue Matatizo Yetu?!
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Iwe ni Kuhusu Mafuriko au Kashmir, au Uchumi au Ukaliaji wa India wa Mito Yetu
Tutaendelea Kungoja Hadi Lini Kinachoitwa Mfumo wa Kimataifa Utatue Matatizo Yetu?!
Baada ya mafuriko makubwa katika maeneo ya kaskazini ya Mkoa wa Khyber Pakhtunkhwa, haswa huko Boner na maeneo ya jirani, ambapo mamia ya watu walipoteza maisha yao na nyumba, mifugo, mali na magari yalisombwa, mawimbi mapya ya mafuriko sasa yanapita kupitia Mkoa wa Punjab, kuelekea Mkoa wa Sindh. Hapo awali, mvua kubwa pia ilikumba Karachi. Tunamuomba Mwenyezi Mungu, Subhaanahu wa Ta’ala, atupe salama na afya, kwani utabiri wa mvua zaidi bado upo, huku watawala wetu hawajachukua hatua yoyote isipokuwa kuinua mikono yao na kuachia jambo hilo lote kwa mfumo wa kimataifa! Wanatoa suala zima kana kwamba ni mabadiliko ya hali ya hewa tu ambayo yako nje kabisa ya matakwa yao, na kwamba ikiwa mfumo wa kimataifa hautaingilia kati, wataachwa bila msaada, kana kwamba kulinda maisha na mali za watu sio jukumu lao bali ni jukumu la mfumo wa kimataifa!
Ama kwa watawala hawa, mateso ya mamilioni ya watu ni fursa mpya tu ya kukusanya sadaka na misaada kutoka sehemu mbalimbali za dunia chini ya kivuli cha "msaada"; pesa ambazo huishia katika hazina zao. Katika muongo uliopita, Pakistan imepokea kati ya dola bilioni 1.4 na 2 kila mwaka kama "ufadhili wa hali ya hewa". Hasa baada ya mafuriko ya 2020, ambapo Pakistan ilipokea dola bilioni 4 mwaka 2021. Tayari imewasilisha madai kwa mfumo wa kimataifa kwa ufadhili wa hali ya hewa ambao ni mara nane zaidi ya kile inachopokea sasa, ikiwa ni pamoja na dola bilioni 1 chini ya jina la "Kituo cha Ustahimilivu na Uendelevu" cha Shirika la Fedha la Kimataifa kilichotengwa kwa ajili ya kukabiliana na hali ya hewa na usimamizi wa hatari za maafa. Mnamo Januari 9, 2023, Mkutano wa Kimataifa wa Pakistan ya Kukabiliana na Hali ya Hewa ulifanyika Geneva, ambapo ahadi zilikatwa zinazozidi ombi la Pakistan la dola bilioni 8, lakini hadi leo ni chini ya 20% tu ndio imetimia. Kwa hivyo, badala ya kuchukua jukumu la kushughulikia mzozo huo, watawala wamehamisha mzigo kwa mfumo wa kimataifa, na wakajitosheleza kwa kuhamisha sehemu ya pesa zinazoingia kwenye hazina zao za kibinafsi.
Suala hili halizuiliwi tu kwa mafuriko, lakini linaonyesha maono ya kudumu ya watawala hawa, walioshawishika kwamba suluhisho la matatizo yetu liko mikononi mwa mfumo wa kimataifa, na kwamba bila wao hatuna nguvu wala uwezo wa kutatua matatizo yetu. Watawala wetu na watunga sera wanaangalia kwa mshangao mifumo ya kufanya maamuzi ya Magharibi na wanaona kushikamana nayo kama kigezo cha maendeleo, ustaarabu na taaluma, na wengi wao wamefundishwa moja kwa moja mikononi mwao. "Maono" haya haswa ndiyo yanayopa mataifa makuu njia ya kuingilia masuala yetu na kulazimisha ajenda zao kulingana na sera zao. Iwe kwa kuachia suala la Kashmir kwa Umoja wa Mataifa, au kumkabidhi Benki ya Dunia kutekeleza Mkataba wa Maji wa Indus, hii ni matokeo ya maono haya. Iwe ni nakisi ya akaunti ya sasa, au nakisi ya mapato ya serikali, au mzozo wa nishati, watawala wetu - kulingana na maono haya - wameweka ajenda na maagizo ya Shirika la Fedha la Kimataifa. Na kwa sababu ya maono haya haya, haki za makundi mbalimbali ya jamii zinaundwa kulingana na ajenda za Ulaya na Amerika, ambayo inazusha maandamano ya mara kwa mara kutoka kwa watu wa Pakistan. Hata katika taasisi muhimu zaidi za serikali, uingiliaji unafanyika chini ya jina la "mageuzi ya taasisi", kwa maagizo kutoka Benki ya Dunia au Benki ya Maendeleo ya Asia. Ama sera za kijeshi na ulinzi za Pakistan, mizozo ya mpaka, au mkakati kuelekea Afghanistan, zinasimamiwa moja kwa moja na Pentagon, Kamandi Kuu ya Marekani na Wizara ya Mambo ya Nje, huku watawala wetu wakisalia kuwa waaminifu kwao daima. Kama matokeo ya maono haya, uhuru wetu umekuwa tegemezi kwa mfumo wa kimataifa. Na cha kushangaza ni kwamba watawala hawa, kutokana na maono haya ya utumwa, wanajaribu kuficha kushindwa kwao kutatua masuala ya kitaifa kwa kusema "hili ni kadari ya Mungu"! Laiti wangekuwa na ujasiri wa kimaadili wa kukiri kushindwa kwao!
Ama katika Uislamu, Khalifa anawajibika kulinda mambo yote ya watu, na hairuhusiwi yeye kukabidhi jambo lolote katika mambo ya Waislamu kwa mamlaka ya ukafiri. Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, amesema katika Kitabu chake Kitukufu: ﴿WALA HATAWAJAALIA ALLAH MAKAFIRI KUWA NA NJIA YA KUWASHINDA WAUMINI﴾, na aya hii inawataka Waislamu waziwazi kutowezesha makafiri kuwa na mamlaka yoyote juu ya mambo yao, na inaharamisha hilo kabisa. Hakika Khalifa atakataa maono haya ya utumwa na atachukua jukumu la moja kwa moja kwa mambo yote ya Waislamu. Kwa mujibu wa nyaraka za sasa za bajeti, Pakistan inalipa Rupia trilioni 8.2 kama malipo ya riba. Khalifa atasimamisha matumizi ya nafasi hii ya kifedha katika benki kama hizo zilizoharamishwa na zisizo halali, na badala yake atazielekeza kwenye miradi ya muda mrefu ya kulinda maisha na mali za Waislamu kutokana na mafuriko na migogoro mingine. Bila kuondoa watawala hawa, na kung'oa maono ya saratani ya utegemezi ambayo wanawakilisha, hakuna njia ya ukombozi kwa Waislamu wa Pakistan.
Ofisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
Katika Wilaya ya Pakistan