Ubinadamu unakataa kufurahia wakati watu wetu wanakufa kwa njaa!
Katika zama za ujahiliya, ambapo nuru ya utume ilikuwa haijaenea, mtu mmoja kutoka kabila la Kikureshi alisema maneno ambayo ubinadamu uliyaweka milele, kabla ya utume kuyatakasa "Ubinadamu unakataa kufurahia wakati watu wetu wanakufa kwa njaa". Alisema hivyo alipowaona Bani Hashim, wanaume, wanawake na watoto, wakisononeka kwa njaa katika shina la Bani Talib, wakiwa wamezingirwa bila chakula wala kinywaji, huku yeye na watu wa Makka wakifurahia ufanisi. Mtu huyu na wenzake hawakungoja idhini kutoka kwa mtu yeyote, lakini hisia zao ziliamka, wakachana karatasi ya dhuluma, wakavunja mzingiro, na kusimama na aliyedhulumiwa, bila kusukumwa na itikadi, bali kwa msukumo wa kibinadamu.
Basi tuko wapi sisi kutoka kwa hao?! Na sisi leo tunawaona ndugu zetu katika itikadi na dini wakikabiliwa na janga baya zaidi ambalo historia imewahi kulijua na tunatazama, hatuchukui hatua yoyote!
Leo janga linajirudia, lakini kwa vazi ambalo labda ni kali zaidi na la kidhalimu; ambapo watoto wanakufa kwa njaa, na kipande cha mkate kinanyakuliwa kutoka midomo ya wenye njaa chini ya mzingiro mkali. Watu wote wanaangamizwa mbele ya macho yetu, na sisi tuko kati ya watazamaji, wasiojiweza, na kimya!
Janga halijafichika tena, na picha hazikanushwi tena, kwani matukio kutoka Gaza yanaonyeshwa moja kwa moja hewani: mtoto anatafuta kipande cha mkate kilichochanganywa na damu, na mama anaomboleza watoto wake, na hospitali haziwezi kutoa dawa, na nyumba zimebomolewa juu ya wakaazi wake. Iko wapi heshima yetu?!
Ni kinyume kilichoje! Kwamba mtu kutoka enzi ya ujahiliya anachukua hatua kwa msukumo wa huruma, wakati leo, katika enzi ya ustaarabu wa Magharibi na haki za binadamu, na katika kivuli cha dhamiri ya ulimwengu iliyopotoka, watu wa Gaza wanaachwa peke yao kukabiliana na kifo, njaa na uharibifu.
Tuna nguvu ya kuvunja mzingiro na kusimamisha mauaji, lakini tumekaa tuli, tumejaa ustaarabu. Kimya katika nyakati kama hizi ni usaliti na kuwaangusha jambo tukufu na jema zaidi.
Ubinadamu unakataa kufurahia wakati ndugu zetu wanakufa kwa njaa. Hebu kuwe na mabaki yetu ya heshima hiyo ya kijahili; labda itakuwa karibu na nuru kuliko ustaarabu usio na moyo.
Ziko wapi hizo jeshi za Kiarabu kutoka Gaza? Tunapotazama majeshi ya Kiarabu, tunaona majeshi makubwa, na bajeti kubwa za silaha, lakini Gaza inapoomba msaada, hakuna anayejibu! Majeshi haya yaliyoandaliwa kwa ajili ya kuilinda umma, leo yamesimama yakitazama yanayowapata ndugu zetu huko Gaza. Mwenyezi Mungu atawahisabu kwa kila kilio cha mama, na kwa kila sauti ya mtoto mchanga anayesumbuka kwa njaa kali. Mwenyezi Mungu atawauliza, enyi mliowaangusha ndugu zenu katika dini na itikadi.
Enyi majeshi ya Umma wa Kiislamu, hebu kuwe na mabaki kwenu ya hisia za mtu katika enzi ya ujahiliya, aliyetambua kuwa neema haikamiliki ikiwa jirani ana njaa. Na labda mtaendelea!
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Mu'nis Hamid - Jimbo la Iraq