Tafakari Fupi Kuhusu Aya
﴿NA Qur'ani Tumeigawanya Ili Uwasomee Watu Polepole Na Tumeiteremsha kidogo kidogo﴾
Qur'ani haikuteremshwa mara moja, bali iliteremshwa kidogo kidogo, pamoja na matukio na hali. Kwa nini? Ili kuwathibitisha Waumini, na kuwafundisha jinsi ya kwenda hatua kwa hatua katika njia ya Da'wah. Mtume ﷺ hakufanya haraka, wala hakutaka matokeo haraka, bali aliwasomea watu Qur'ani ﴿POLEPOLE﴾ yaani iliteremshwa kwa vipindi na matukio, ili mwanadamu Muumini ajengwe kwayo kwa msingi imara, na jamii ianzishwe kwa busara. Na mtindo huu wa kuteremshwa Wahyi haukuwa bure, bali kwa hekima kubwa; ili kuzithibitisha nyoyo, na kuongoza akili, na kuwalea wazee wa Uislamu juu ya uongozi na kubeba amana.
Mtume ﷺ hakuwa anatafuta matokeo ya haraka, bali alifuata njia ya ufikishaji ujumbe ulio wazi na kazi endelevu, na utekelezaji unaoonekana na alikuwa anawasomea watu Qur'ani kwa wakati sahihi, akishughulikia masuala yao, akiwaunganisha na Mwenyezi Mungu, na kuwainua juu ya ujinga, mpaka wakawa watu walioongoza ulimwengu.
Hakika aya hii inaweka mikononi mwetu kanuni kubwa katika mabadiliko ya kweli, ambayo hayawi kwa kelele za msimu, wala kwa mihemko ya kihisia, wala kwa kusubiri miujiza, bali ni kwa kusimama imara katika wazo, na mwingiliano wa ufahamu na umma, na subira katika njia ya Da'wah, na kufanya kazi ndani ya mradi wa kisiasa wa kimungu ulio wazi.
Leo, na umma unahangaika kati ya mifumo ya ukafiri, na suluhisho za kupaka rangi, na kuomba msaada kutoka kwa mfumo wa kimataifa, basi jambo la kwanza tunalopaswa kurudi kwalo ni Qur'ani na Sunna na kile kilichotokana nazo cha Ijmaa ya Masahaba na Qiyasi iliyojengwa juu ya sababu ya kisharia; tunarudi kwenye Qur'ani si kama maneno yanayosomwa tu katika mihrabu, au aya zinazosomwa wakati wa kufa, bali kama mtaala unaoelekeza hatua zetu, na kama katiba inayoongoza maisha yetu, na kama kanuni tunayojenga juu yake dola yetu.
Hakika ujenzi wa umma unakuwa kwa kuunda utu wa Kiislamu kiakili na kisaikolojia, na kuuongoza kuelekea kufanya kazi kwa bidii ili kusimamisha dola ya Kiislamu, Khilafah Rashidah juu ya manhaji ya Utume, ambayo kwayo pekee dhuluma zinaondolewa, na sharia ya Mwenyezi Mungu inatekelezwa, na uadilifu unarudishwa, na wanaodhulumiwa katika ardhi wanasaidiwa.
Kama alivyo subiri Mtume ﷺ kubeba Da'wah huko Makka, na kuwathibitisha Masahaba wake juu ya haki, na kukabiliana na ukafiri na batili kwa ujasiri, mpaka Mwenyezi Mungu akamuwezesha huko Madina, basi inatupasa sisi kutembea katika nyayo zile zile; tunabeba Uislamu kama ujumbe na mfumo wa maisha, na tunafanya kazi ya kuusimamisha katika uhalisia, hata kama njia itakuwa ndefu au dhabihu zitaongezeka, basi manhaji hii inatufundisha kwamba mabadiliko hayawi kwa haraka wala kwa ubadilishaji, bali kwa kusimama imara katika haki, na kwa kulea juu ya maana za Qur'ani, na kwa kazi iliyopangwa mpaka Mwenyezi Mungu aandae ushindi.
Na leo sisi pia tunahitaji kutembea katika njia hii: tunasoma Qur'ani kwa kuzingatia, na tunafahamu maana zake, na tunawabebesha watu kwa ufahamu, na tunasubiri kama alivyo subiri Mtume ﷺ, mpaka itakapokuja ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kuteuliwa na kuwezeshwa, na Uislamu unarudi kuongoza ubinadamu kwa dola ya Khilafah Rashidah.
Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: ﴿AHADI YA MWENYEZI MUNGU KWA WALIOAMINI KATIKA NYINYI NA KUTENDA MEMA ATAWAFANYA MAKHAIFA KATIKA ARDHI...﴾ Ahadi haitimii kwa matamanio, bali kwa kazi ya kweli ambayo Mitume waliitembea, na kwayo pekee umma unarudi kwenye nafasi yake sahihi; kiongozi si mfuasi, mshindi si dhalili, mja wa Mola wake si wa maadui zake.
Imeandikwa kwa ajili ya Radio ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Muayyad Al-Rajhi - Wilaya ya Yemen