Pamoja na Qur'ani Tukufu - Sura ya Al-A'raf
Pamoja na Qur'ani Tukufu - Sura ya Al-A'raf
Pamoja na Qur'ani Tukufu - Sura ya Al-A'raf
null
null
null
null
null
Ama aina ya pili: Ama uhawilishaji kivitendo, hupatikana kwa uchunguzi wa matukio na desturi zilizothibitishwa na umma, na mfano wake ni lugha: kwani mojawapo ya mambo yanayoingia katika tawaturu ya kimakna ni matumizi ya lugha na Waarabu, kwani wamezoea maneno maalum yanayoashiria maana maalum, hivyo neno ili liweze kuchukuliwa kuwa ni neno la Kiarabu lazima liripotiwe kutoka kwa Waarabu ripoti sahihi ama kwa kuhamisha mashairi, au kupitia matumizi ya lugha na wale ambao hoja yao inasimama kutoka kwa Waarabu (na hii ni aina ambayo inatofautiana kati ya tawaturu ya kimakna na kimatamshi).
Amesema Muslim bin Abid, Allah amrahamu: "Hawapati watiifu kwa Allah utamu wowote duniani mtamu zaidi kuliko upweke wa kumnong'oneza Bwana wao, wala hawapendi katika Akhera thawabu kubwa zaidi katika vifua vyao, na tamu zaidi katika nyoyo zao kuliko kumtazama Yeye"
Waislamu katika wakati wetu huu wamejaribiwa na mifumo ya usaliti ambayo inatawala na sheria za kidunia potofu ambazo Mungu hakuziteremsha, inayowaunga mkono makafiri wavamizi, inatekeleza mipango yao, inalinda maslahi yao, inaeneza utamaduni wao, inatawala na sheria zao, na inawatafuta wakati wa hatari na kuwasha moto wa vita vya ndani na fitina kati ya Waislamu na kuwadhulumu raia wao na kuwatesa vibaya na kuhujumu masuala yao na kusimama upande wa maadui zao...