Sehemu ya Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir Yazindua Kampeni ya Ulimwengu yenye kichwa: "Vita vya Sudan: Kisa cha Ukoloni, Usaliti na Kukata Tamaa"
Vita vya kikatili nchini Sudan kati ya Jeshi la Wanajeshi la Sudan linaloongozwa na mtawala wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah Al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka cha kijeshi kinachoongozwa na Mohammed Hamdan Dagalo "Hemedti", naibu wa zamani wa Burhan katika Baraza la Utawala, vimeingia mwaka wake wa tatu sasa, na kusababisha vifo vya makumi ya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaonyesha kuwa idadi ya vifo katika vita hivi visivyo na maana imefikia 150,000, huku ukatili mbaya ukifanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso na ubakaji.