Muhtasari wa Kitabu cha Vifaa - 4
Ukhalifa ni uongozi wa Waislamu wote duniani, na ni kwa ajili ya kutekeleza hukumu za Kiislamu, na kubeba da'wa ya Kiislamu kwa ulimwengu, hivyo ni kwa ajili ya kutekeleza hukumu za Kiislamu kwa wanadamu na kuzieneza miongoni mwao. Waislamu humpa bay'a yeyote wamtakaye, na wamteue yeyote wamtakaye kuwa Khalifa wao, nao ni wadhifa wa kibinadamu, na haufanani na unabii kabisa, kwani unabii ni wadhifa wa kimungu ambao Mungu humpa amtakaye ili apokee sheria yake kwa njia ya wahyi, na Nabii Muhammad, rehema na amani zimshukie, alikuwa ni mtawala aliyetekeleza sheria aliyoileta, hivyo alishika utawala na unabii, na Mungu alimwamrisha kutawala kama alivyomwamrisha kufikisha ujumbe, akasema Mtukufu: (NA UHUKUMU BAINA YAO KWA ALIYOTEREMSHA ALLAH), na akasema: (EWE MJUMBE FIKISHA ALIYOTEREMSHIWA KWAKO KUTOKA KWA MOLA WAKO), hivyo Nabii, rehema na amani zimshukie, alishika nyadhifa mbili ambazo ni unabii na uongozi wa Waislamu wote duniani. Ama ukhalifa baada ya Mtume wa Mungu, rehema na amani zimshukie, basi wanaoushika ni binadamu, nao si manabii, hivyo wanaweza kufanya yale ambayo binadamu hufanya kama vile makosa, na Mtume wa Mungu ametuarifu hilo katika kauli yake: "Hakika imamu ni ngao anapiganwa nyuma yake na anahofiwa, akiamrisha kumcha Mwenyezi Mungu, Mtukufu na Mwenye Enzi, na akafanya uadilifu basi atakuwa na ujira kwa hilo, na akiamrisha vinginevyo basi atakuwa na dhambi kwa hilo", hadithi hii inaashiria kwamba inajuzu kwa imamu kufanya makosa, kusahau na kuasi, na watu wanalazimika kumtii maadamu anahukumu kwa Uislamu, na hakumpata ukafiri ulio wazi, na maadamu haamrishi uasi.
Hakuna muda maalumu kwa uongozi wa Khalifa, maadamu anahifadhi sheria, ana uwezo wa kusimamia mambo ya dola anabakia kuwa Khalifa, kwani hadithi ambazo zimetaja bay'a zimetaja kwa ujumla na hazikuweka muda maalumu, vile vile ukhalifa wa Masahaba uliendelea mpaka walipofariki, na hilo lilikuwa ni ijmaa kutoka kwa Masahaba. Ama ikitokea na yakamfika Khalifa yale yanayostahiki kumfuta au kumfanya afutwe basi muda wa ukhalifa wake unaisha, na hilo si kuweka muda maalumu wa bay'a, bali ni kwa sababu ya kutokea kasoro katika sharti zake; kwani bay'a imewekwa kwa Khalifa kutekeleza yale aliyoahidiwa, nayo ni kufanya kazi kwa kitabu na sunna.
Ikiwa Khalifa amepoteza sharti yoyote kati ya sharti saba za uteuzi basi haijuzu kwake kisheria kuendelea na ukhalifa, na anakuwa anastahiki kufutwa, na ambaye ana uwezo wa kufanya uamuzi wa kumfuta ni mahakama ya madhila, ndio inayoamua ikiwa Khalifa amepoteza sharti yoyote kati ya sharti za uteuzi, kwani kupatikana yale yanayostahiki kumfuta Khalifa ni madhila yanayohitaji kuondolewa, na ni miongoni mwa mambo ambayo yanahitaji kuthibitishwa, hivyo ni lazima yathibitishwe mbele ya kadhi, na ambaye anahukumu kuondoa madhila ni mahakama ya madhila, na kadhi wake ndiye mwenye mamlaka ya kuthibitisha madhila na kuhukumu nayo, hivyo ikitokea na Waislamu na wenye mamlaka wakazozana basi ni lazima jambo lao lirudishwe kwa Mungu na Mtume wake, yaani kulipeleka kwenye mahakama, hili ni ikiwa Waislamu wameona kwamba ni lazima afutwe kwa kupoteza sharti mojawapo ya uteuzi lakini yeye anawazozania hilo, ama akijiuzulu mwenyewe basi jambo limekwisha.
Ni lazima kushughulika na kumteua Khalifa tangu dakika ya kwanza kukosekana wadhifa wa ukhalifa, kama ilivyotokea wakati wa kufariki Nabii, rehema na amani zimshukie, ambapo Waislamu walishughulika mara baada ya kufariki kwake kumteua Khalifa wake, na muda wa juu wa kumteua Khalifa ni siku tatu, na dalili ni kwamba Umar bin al-Khattab alipowateua watu sita katika watu wa shura kwa ajili ya wadhifa wa ukhalifa aliwawekea siku tatu, na akateua watu hamsini kuwaua wanaompinga miongoni mwao ikiwa hawataafikiana juu ya Khalifa katika muda huo, pamoja na kwamba wao ni katika watu wa shura, na ni katika Masahaba wakubwa, na hakuna Sahaba aliyempinga, hivyo hilo lilikuwa ni ijmaa. Hivyo ni lazima kwa Waislamu kushughulika na kumteua Khalifa baada ya kukosekana nafasi ya ukhalifa, na ni lazima kumteua ndani ya siku tatu, ama ikitokea na ukhalifa ukaangamizwa na wakakaa mbali na hilo, basi wamefanya dhambi, isipokuwa yule ambaye amevaa nguo ya kufanya kazi kwa bidii ili kuusimamisha pamoja na kundi lenye ikhlasi, basi yeye anaokoka na dhambi, nayo ni dhambi kubwa kama alivyobainisha, rehema na amani zimshukie "Na atakayekufa na hali shingoni mwake hakuna bay'a amekufa kifo cha kijahiliya".
Wasaidizi ni mawaziri ambao Khalifa huwateua ili kumsaidia katika kubeba majukumu ya ukhalifa, na haifai kuwaita mawaziri bila kuweka masharti, ili maana ya waziri katika Uislamu isichanganyike na maana ya waziri katika mifumo ya kidemokrasia ya kilimwengu. Na waziri wa tafwidh (kukabidhi) Khalifa humkabidhi kusimamia mambo kwa rai yake na kuyapitisha kwa ijtihadi yake kulingana na hukumu za sheria.
Khalifa anaweza kumkabidhi msaidizi wa tafwidh kumwakilisha katika sehemu zote za dola pamoja na kuangalia kwa ujumla katika kazi zote, na anaweza kumkalifisha kazi maalumu, au kwa eneo maalumu, mfano kwa majimbo ya mashariki au magharibi, na kwa kuwa Khalifa atahitaji zaidi ya waziri hasa pamoja na upana wa ukubwa wa dola, basi hili litazusha matatizo katika mawaziri kufanya kazi zao kwa sababu ya uwezekano wa kuingiliana maadamu kila mmoja wao ana kuangalia kwa ujumla na uwakilishi, hivyo sisi tuna kubali yafuatayo: katika upande wa kumkabidhi msaidizi anakabidhiwa kuangalia kwa ujumla na uwakilishi katika sehemu zote za dola, na katika upande wa kazi msaidizi anakalifishwa kazi katika sehemu ya dola, yaani majimbo yanagawanywa kati ya wasaidizi, na ama katika upande wa kuhamisha msaidizi anahamishwa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kutoka kazi moja kwenda nyingine bila kuhitajia ukabidhi mpya; kwani asili ya kumkabidhi kuwa msaidizi inajumuisha kila kazi, na yeye kwa hilo anatofautiana na liwali, kwani liwali amekabidhiwa kuangalia kwa ujumla katika sehemu fulani, hivyo hahamishwi kwenda pengine, bali anahitajia ukabidhi mpya, kwani sehemu mpya haimo katika ukabidhi wa kwanza, ama msaidizi yeye anakabidhiwa kuangalia kwa ujumla na uwakilishi, hivyo inajuzu kumhamisha kutoka sehemu moja kwenda nyingine bila kuhitajia ukabidhi mpya. Na inashurutishwa katika msaidizi wa tafwidh yale yanayoshurutishwa katika Khalifa, nayo ni kuwa mwanaume Muislamu, huru, baleghe, mwenye akili, muadilifu na mwenye uwezo katika watu wa ufanisi.
Ni lazima kwa msaidizi wa tafwidh kupeleka yale anayokusudia kusimamia kwa Khalifa, kisha kumjulisha yale aliyoyapitisha katika usimamizi, na anatekeleza ujulishaji huu maadamu Khalifa hakumzuia hilo, na hilo si kuchukua idhini, kumjulisha kwake kunamaanisha kumueleza katika jambo, na ujulishaji huu unatosha kufanya kila kilichokuja ndani yake katika maelezo bila kuhitajia kutolewa idhini ya kufanya kazi, na ni lazima kwa Khalifa kuzitazama kazi za msaidizi; kwani yeye ndiye mwenye dhamana ya raia na kurekebisha yale ambayo yanaweza kutokea kwa makosa kutoka kwa msaidizi. Ikiwa msaidizi amemjulisha Khalifa katika jambo akamkubali kisha baada ya kulitekeleza Khalifa akampinga basi anaangaliwa, ikiwa ni katika yale ambayo inajuzu kwa Khalifa kurekebisha kutokana na kitendo chake mwenyewe inajuzu kurekebisha kutokana na kitendo cha naibu wake, kama vile kuweka mpango wa kijeshi; kwani ingawa anafanya mamlaka zote za Khalifa lakini hazifanyi kwa njia ya kujitegemea bali kwa njia ya uwakilishi, na ikiwa kitendo ni katika yale ambayo haijuzu kwa Khalifa kurekebisha kutokana na kitendo chake mwenyewe basi haijuzu kurekebisha kutokana na kitendo cha naibu wake, kama vile kuweka mali katika haki yake, au hukumu aliyoitekeleza katika sura yake. Hakika msaidizi wa tafwidh hahusishiwi na idara; kwani ambao wanaendesha idara wao ni vibarua wala si watawala, lakini hili halimaanishi kwamba amekatazwa kufanya kazi yoyote ya kiutawala, lakini maana yake kwamba hakusishwi na kazi za utawala bali ana kuangalia kwa ujumla.
Hakika ambaye anawateua wasaidizi wa tafwidh na kuwafuta ni Khalifa, na uongozi wao unaisha wakati wa kufariki kwake, na hauna uendelevu isipokuwa katika kipindi cha amir wa mpito, na hawahitajii uamuzi wa kufutwa wakati huo.