Jarida la Ar-Raya: Usagaji upya wa mfumo wa kilimwengu na taasisi zake tena nchini Syria
Rais wa Syria wa kipindi cha mpito Ahmad Al-Share' ameamuru agizo nambari 66 la mwaka 2025 linaloamua kuundwa kwa kamati kuu ya uchaguzi wa bunge, ambapo uamuzi huo ulijumuisha vifungu vinne, ikiwa ni pamoja na kuunda kamati kwa jina la Kamati Kuu ya Uchaguzi wa Bunge yenye wajumbe kumi na rais, na kamati hii inasimamia uundwaji wa tume ndogo za uchaguzi ambazo huchagua theluthi mbili ya wajumbe, na rais huteua theluthi moja ya wajumbe waliosalia, pia idadi ya wajumbe hufikia wajumbe 150 waliogawanywa katika mikoa yote.