Jarida la Ar-Raya: Mkataba wa kiusalama na Mayahudi ni mteremko hatari kuelekea kwenye shimo la upotevu!
Rais wa serikali ya mpito nchini Syria, Ahmed Al-Share'a, alitoa matamshi ya kutiliwa shaka alipotangaza kuwa mazungumzo yanayoendelea na taasisi ya Kiyahudi yanaweza kusababisha mkataba wa kiusalama katika siku za usoni. Aliona kuwa mkataba kama huo ni "lazima," mradi unaheshimu umoja wa ardhi ya Syria na unakaguliwa na Umoja wa Mataifa. Pia alifichua kuwa pande hizo mbili zilikuwa zimesalia siku chache kufikia msingi wa mkataba huu mnamo Julai/Julai iliyopita, lau si mabadiliko katika Mkoa wa Suwayda ambao ulivuruga mchakato huo.