
2025-08-17
Kushi News:
Neno la Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari siku ya Jumamosi tarehe 22 Safar 1447 Hijria, sawia na 16/08/2025 Miladia, yenye kichwa: "Wito kwa Watu wa Sudan.. Iokoeni Darfur Ili Isipatwe na Yaliyompata Kusini"
Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilitangaza siku ya Jumamosi tarehe 26/07/2025, kuunda serikali sambamba na serikali iliyopo nchini Sudan, katika mji mkuu wa Darfur Kusini (Nyala). Hatua hii ya Vikosi vya Msaada wa Haraka ni hatua ya kuendeleza utengano wa eneo la Darfur, ambalo wanalidhibiti, isipokuwa sehemu za mji wa Al-Fashir, ambao wameuwekea mzingiro mkali kwa zaidi ya mwaka mmoja, na wanafanya mashambulizi ya mara kwa mara kuuangusha, ili eneo lote la Darfur liwe chini ya udhibiti wao.
Enyi watu wa Sudan:
Msururu wa Marekani wa kuitenga Darfur ulianza miaka mingi iliyopita, kama ilivyoshikilia faili la Sudan Kusini hadi ikafikia kutengana na Kaskazini, na sasa inakwenda na mikakati ile ile ambayo ilitumika kuitenga Kusini ili kuitenga Darfur, ambapo imeanza kivitendo kwa kusaini kile kinachoitwa makubaliano ya amani mnamo 14/07/2011, na kuipa eneo la Darfur uhuru mpana, na daima suala la uhuru ni mwanzo halisi wa kuelekea katika msururu wa kupasuliwa, na licha ya kwamba; yaani Marekani, ndiyo iliyounda makubaliano haya, haikuyaona kuwa ni makubaliano ya mwisho, msemaji wa wizara yake ya mambo ya nje wakati huo, Mark Toner, alisema baada ya kusainiwa kwa makubaliano hayo: (Makubaliano haya ni hatua ya kusonga mbele kuelekea suluhisho la kudumu la mgogoro huko Darfur).
Na kinachothibitisha kwamba Marekani ndiyo iliyo tengeneza Sudan Kusini, na inajitahidi kupasua kilichobaki cha Sudan, ni kauli za Omar al-Bashir, katika mahojiano yake na shirika la habari la Kirusi Sputnik, ambayo yalichapishwa tarehe 25/11/2017, ambapo alisema: (Masuala yangu ya Darfur na Sudan Kusini yalipata msaada na usaidizi kutoka kwa Marekani, na chini ya shinikizo lake Sudan Kusini ilijitenga), na aliongeza: (Tuna taarifa sasa kwamba jitihada za Marekani ni kuigawanya Sudan katika nchi tano), kinachothibitisha kwamba Marekani ndiyo iliyo tengeneza Sudan Kusini, na sasa inajitahidi kuitenga Darfur, na ikiwa itafanikiwa - Mungu apishe mbali - basi itapasua mikoa mingine ya Sudan moja baada ya nyingine, na itafanya hivyo kuchora mipaka ya nchi tano katika nchi yenu kwa damu yenu na damu ya watoto wenu kama ilivyofanya hapo awali kwa kuitenga Kusini kwa damu ya watu wenu milioni 2 na kama inavyofanya sasa kuitenga Darfur kwa damu ya mamia ya maelfu yenu, basi amkeni enyi watu wa Sudan ili kufeli mpango huo na kuondoa kabisa mizizi ya vibaraka na wanafiki na kurekebisha mkondo wa maisha yenu.
Enyi watu wa Sudan:
Muumini haumwi mara mbili kutoka tundu moja, na tumeshaumwa kutoka tundu la Marekani kwa kuitenga Sudan Kusini, je, tutairuhusu kuitenga Darfur?! Bukhari na Muslim wameripoti kutoka kwa Abu Huraira, radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, kutoka kwa Nabii ﷺ, kwamba alisema: «Muumini HAUMWI MARA MBILI KUTOKA TUNDU MOJA».
Hakuna nchi yoyote inayoruhusu mikoa yake kupasuliwa, kwa sababu katika umoja kuna nguvu na katika utengano kuna udhaifu na unyonge, vipi ikiwa Uislamu umeifanya suala la umoja wa Umma, na umoja wa taasisi yake, kuwa suala la hatima, linalochukuliwa hatua ya uhai au mauti? Kutoka kwa Arfaja alisema: Nilisikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema: «Yoyote AKIWAFUATENI NA Jambo Lenu LOTE LIMO JUU YA MTU MMOJA, AKITAKA KUVUNJA BAKORA ZENU, AU KUTAWANYA JAMII YENU, MUUUENI».
Enyi Waislamu:
Mnawezaje kunyamazia kupasuliwa kwa nchi yenu na hamuendeshwi, na hamuifanyi umoja wa nchi yenu kuwa suala la hatima kama alivyowaamuru Nabii wenu ﷺ?! Mnamtii nani? Je, mnamtii Marekani kafiri mkoloni, au mpenzi wenu mteule, rehema na amani zimshukie?! Mwenyezi Mungu anasema: ﴿NA ALICHO KULETEENI MTUME KICHUKUENI NA ALILOWAKATAZENI LIWACHENI NA MCHENI ALLAH KWA HAKIKA ALLAH NI MKALI WA ADHABU﴾, na anasema: ﴿NA MTIIENI ALLAH NA MTIIENI MTUME NA JIHADHARINI MKIGEUKA BASI JUENI KUWA JUU YA MTUME WETU NI KUFIKISHA UJUMBE WAZI﴾.
Enyi wanahabari:
Kazi yenu ni kubwa katika kuwaelimisha watu juu ya hatari za kupasuliwa, basi fanyeni kalamu zenu, na taasisi zenu za habari kuwa mimbari ya ufahamu, mkiwafichua mipango ya makafiri wakoloni na wasaidizi wao wanaowasaidia kutekeleza njama zao dhidi ya nchi yetu na umoja wake, kwani nyinyi ni waaminifu katika kusema ukweli, na kusimama dhidi ya ubatili, Mwenyezi Mungu anasema: ﴿UMEFANYIKA UKWELI NA UONGO HAUANZI WALA HAUTARUDI﴾.
Enyi wanasiasa:
Wajibu wa kulinda umoja wa nchi, ni wajibu wenu wa kwanza, kwa kuzingatia nyinyi ni viongozi, na wakuu, na vichwa vya watu, kwa hivyo kusimama kwenu dhidi ya miradi ya kupasua na kugawanya, ndiko kunazuia, basi msiwe wasaidizi wa kafiri mkoloni, ili atekeleze kupitia kwenu njama zake, Mwenyezi Mungu anasema: ﴿WALA MSIWAELEKEE WALIO DHULUMU ISIJE IKAWASHIKENI MOTO NA HAMNA WALAJI KANDO NA ALLAH KISHA HAMTANUSURIWA﴾.
Enyi Maulamaa, enyi warithi wa Manabii:
Wajibu wenu katika kuwaelekeza viongozi na watawala, kwenye haki na usawa ni mkuu, basi msiwe vipando vyao, mkiitoa fatwa kwa wanavyovitamani, wala msinyamaze kusema ukweli haijalishi matokeo yatakuwa nini, Mtume ﷺ anasema: «Yoyote ATEYAYE ILMU ALLAH ATAMFUNGA NGAO SIKU YA KIYAMA KWA NGAO YA MOTO», na mnajua kwamba kupuuza umoja wa Umma na taasisi yake ni dhambi kubwa.
Enyi maofisa na askari:
Enyi mliyoapa kulinda umoja wa nchi yenu, mnawezaje kuruhusu kupasuliwa kwake na mnaangalia?! Kwani Mwenyezi Mungu atawauliza kuhusu ahadi yenu mliyo kata, Mwenyezi Mungu anasema: ﴿NA TEKELEZENI AHADI KWA HAKIKA AHADI ITAULIZWA﴾, basi msiruhusu kutengana kwa Darfur, na kabla ya hapo mliipuuza Sudan Kusini, basi ondoleeni dhambi kutoka shingo zenu, na simameni imara dhidi ya mpango wa Marekani, na muiendeshe jeshi kufeli mpango wa kupasua nchi yenu.
Na mjue kwamba misukosuko hii mikubwa, na njama za makafiri wakoloni zinazoendelea, hazitakuwa na kinga isipokuwa kwa kurejea kwenye Uislamu mtukufu; itikadi, na mifumo ya maisha, na hilo haliwezekani isipokuwa kwa kusimamisha dola ya Kiislamu; Khilafah, na hilo linapatikana tu kwa kuipa Nusra Hizb ut-Tahrir, ili iisimamishe kwa uongofu juu ya njia ya Utume, itakatia mizizi makafiri na kuunganisha nchi za Waislamu.
Mwenyezi Mungu anasema: ﴿ENYI MLIOAMINI ITIKIENI ALLAH NA MTUME ANAPOKUITENI KWENYE YALE YANAYOKUHUISHA﴾.
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir
katika Wilaya ya Sudan
Vyanzo: Kushi News / Abu Wadaha News
