NAFASI ZA MATUNDA
Ole wake anayejipa nguvu kwa neema za Mungu katika maasi yake
Alikuwa Hasan al-Basri akisema: Ufahamu ni chombo cha elimu, na elimu ni dalili ya amali, na amali ni kiongozi wa kheri, na hawaa ni chombo cha maasi, na mali ni ugonjwa wa wenye kukataa, na dunia ni soko la Akhera, na ole wote ni wa yule anayejipa nguvu kwa neema za Mungu katika maasi yake.
Adabu za Al-Hasan Al-Basri, kujinyima kwake dunia na mawaidha yake
Na Abu Al-Faraj Ibn Al-Jawzi
Mola umfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba zake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rehema za Mungu na Baraka zake