Vito vya Thamarati
Ikiwa Mwenyezi Mungu atakunusuruni, basi hakuna atakayewashinda
Enyi majeshi katika nchi za Kiislamu: Hakika historia daima hujirudia, na nyinyi mtakapouhami Uislamu kwa kumtii Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta'ala, mtapata nusra ya Mwenyezi Mungu kwenu, kama alivyowanusuru Subhaanahu wa Ta'ala viongozi wa kijeshi Waislamu waliowatangulia, wakawashinda maadui zao licha ya matatizo waliyokuwa wakikabiliana nayo (kama vile kiongozi Khalid bin Al-Walid, Salahuddin, na Muhammad bin Al-Qasim...), basi sasa endeleeni katika nyayo za hawa viongozi wa kijeshi wema, na mtoe nusra kwa ajili ya kusimamisha Khilafa kwa manhaj ya Utume, na hamtakuwa na haja ya nusra ya yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta'ala nanyi mkiwa katika njia ya ushindi, Amesema Mwenyezi Mungu Subhaanahu wa Ta'ala: ﴿Ikiwa Mwenyezi Mungu atakunusuruni, basi hakuna atakayewashinda, na ikiwa atakuachilieni, ni nani basi atakayekunusuruni baada yake? Na kwa Mwenyezi Mungu wategemee Waumini﴾.
Mwenyezi Mungu amfikishie rehema Bwana wetu Muhammad na Aali zake na Masahaba wake wote
Na Amani iwe juu yenu na Rahma ya Mwenyezi Mungu na Baraka zake